RSS

Author Archives: dsta12

SEMINA MWEZI WA KUMI 2024 DAR ES SALAAM

HAPO CHINI NI AUDIO YA MAHUBIRI YANGU HUKO DAR ES SALAAM SEPTEMBA / OKTOBA 2024

1. ITOENI MIILI YENU IWE DHABIHU ILIYO HAI. SEHEMU 1

2.ITOENI MIILI YENU IWE DHABIHU ILIYO HAI. SEHEMU 2

3. IWENI NA NIA IYO HIYO. SEHEMU 1

4. IWENI NA NIA IYO HIYO. SEHEMU 2

5. DINI INAPINGA MAISHA YA KIROHO

6. LENGO LA UTOAJI KWENYE AGANO JIPYA

7. YATAFAKARINI HAYO

8. KRISTO NDANI YAKO

9. SEMINA YA VIJANA. SEHEMU 1

10. SEMINA YA VIJANA. SEHEMU 2

11. SEMINA YA WACHUNGAJI. SEHEMU 1

12. SEMINA YA WACHUNGAJI. SEHEMU 2

13. KUMJUA YESU

14. HAMNA MADHABAHU DUNIANI SEHEMU 1

15. HAMNA MADHABAHU DUNIANI SEHEMU 2

 

 
Leave a comment

Posted by on October 2, 2024 in Uncategorized

 

KIUMBE KIPYA KATIKA KRISTO!

KIUMBE KIPYA KATIKA KRISTO: SEHEMU 2  (SIKILIZA!)

KIUMBE KIPYA KATIKA KRISTO: SEHEMU 1

 
1 Comment

Posted by on March 26, 2024 in Uncategorized

 

MAMBO YA NDOA

Mafundisho hayo yanazingatia mambo ya ndoa. Kuyasikiliza, bonyeza tu.

MAMBO YA NDOA

 
Leave a comment

Posted by on March 18, 2024 in Uncategorized

 

SINA MASHAKA NA WEWE

SIKILIZA:

SINA MASHAKA NA WEWE – PASIPO IMANI HAIWEZEKANI KUMPENDEZA MUNGU

 
Leave a comment

Posted by on September 3, 2023 in Uncategorized

 

KWA NINI UNAKWENDA KANISANI?

SIKILIZA:

KWA NINI UNAKWENDA KANISANI? 

 
Leave a comment

Posted by on August 31, 2023 in Uncategorized

 

JUU YA MAOMBI SEHEMU 4

SOMO: MAISHA YA MAOMBI KWA MKRISTO (Part 3)

KUWAACHA WATU NA KWENDA KUOMBA!

Hili ni tendo la ajabu sana ambalo Yesu alilifanya! Lilikuwa ni fundisho kwetu! Hebu jaribu kufikiri; Kwa jinsi Yesu ambavyo ana kila kitu, LAKINI PAMOJA NA YESU NA KUWA NA KILA KITU, lakini alijua pasipo maombi yote aliyokuwa nayo HAIWEZEKANI! Yesu mwenyewe alikuwa anajua hapa bila maombi hamna kitu! Alifikia mahali anawaacha makutano halafu anakwenda kuomba. Luka 5:12-16. Hebu tusome mstari wa 16.

“Lakini yeye alikuwa akijiepua,akaenda mahali pasipokuwa na watu,akaomba.”

Hapo Yesu anawakimbia makutano na kuelekea zake kwenye maombi, japokuwa ni ngumu sana kwa baadhi ya watu kuwaacha watu na kwenda kwa kuomba katika mazingira kama haya ya Yesu, kwao ni utukufu. Ikiwa Yesu alifanya hivyo, sisi tunapaswa kufanya hivyo na kuzidi kulingana na maisha yetu na dunia ya leo, lakini leo mtu anasema hana muda wa kuomba, eti kazi zinambana, na kwa sababu nyingine zinazofanana na hizo, lakini bado mtu huyohuyo ambaye anasema hana muda wa kuomba huyo huyo unaweza kumuona katika makundi ya watu au marafiki akiongea muda mrefu, lakini hao hao wanaosema hawana muda wa kuomba ni watu hodari sana kwa kuchat, hana muda wa kuomba lakini ana muda wa kuchat na watu kwa njia ya whatsapp, muda wote anafanya kazi huku yuko whats app! Hana muda wa kuomba lakini ana muda wa kuongea na watu kwenye simu masaa na masaa, hana mua wa kuomba lakini anaangalia movie masaa na masaa; hana muda wa kuomba lakini ana muda wa kuangalia mpira …ninaweza kusema huyu hana muda wa kuongea na Mungu lakini ana muda wa kuongea na watu! Kwa sababu maombi ndiyo kuongea na Mungu.

Kuongea na watu si vibaya; si vibaya kuchat na watu kwa njia mbalimbali za mitandao, lakini ni mbaya kama tuna muda wa kufanya hivyo lakini hatuna muda wa kuomba! Ni mbaya sana! Sana ! Inatakiwa ifikie mahali tunaongea na watu lakini ukifika muda fulani tunajiepua na kwenda mahali kusikokuwa na watu au mahali ambapo tutaweza kuomba bila buguza! Hapa Yesu hakwenda kanisani! Maombi tunaomba popote pale kama mazingira hayaturuhusu kwenda kanisani, tukipata nafasi tu kidogo tu; tunaomba hata kimoyomoyo! Kuomba sio lazima iwe kanisani.

Bila maombi tutajikuta tunaishi maisha ya unafiki! Maisha ya uhitaji wa kupitiliza na kujikuta kwenye madeni wakati wote, ukiondoa maombi hata unahubiri kila siku lazima iko siku utaanguka tu! LAZIMA! Tuache mambo ya kukaa kaa na watu na kuongeaongea muda mwingi tunaumalizia kwa watu. Tena wakati mwingine mambo mengine hayana hata maana, tunaopoteza kuongea na watu ambao hata tukienda kulala hata hawajui yanayotusibu katika usingizi wetu. Hawana sifa ya kuongea na sisi kabla ya kuongea na Mungu wetu! Kama Yesu aliomba mwenye huduma kubwa kuliko huduma yako wewe ambaye unalewa na sifa za watu lakini kuomba hutaki! Sisi tutapona? Shetani alikuwa hana kitu kwa Yesu lakini bado Yesu alikuwa anaomba. Tusidanganywe na sifa zinazotoka vinywani mwa watu.
Tuweke ratiba kwamba! Kuanzia muda fulani ni muda wa maombi. Hapo hata simu ipigwe hakuna kupokea, tunakwenda mahali pasipokuwa na watu kifikra! Yesu alikwenda sehemu halisi! Lakini kama mazingira yetu hayaturuhusu kufanya hivyo, tunapaswa kwenda mbali na watu kifikra! Wakati wa kuomba ikiwezekana zima simu yako au weka silent kama simu yako ndio kila kitu! Nikiwa na maana kuna bible n.k.

Yesu naye tungesema hana muda, kwa sababu pale alikuwa kazini! Lakini alijua umuhimu wa maombi! Kama wewe huna muda usile chakula basi! Kinachokufanya ule nini wakati huna muda?

 
Leave a comment

Posted by on July 11, 2020 in Uncategorized

 

JUU YA MAFUNDISHO NA HISTORIA YA WASABATO

KUSOMA JUU YA MAFUNDISHO NA HISTORIA YA WASABATO NA KULINGANISHA NA MAFUNDISHO YA BIBLIA NA INJILI YA KWELI, TEMBEA KWA:

https://www.wasabato.com

 
Leave a comment

Posted by on June 30, 2020 in Uncategorized

 

JUU YA MAOMBI 3

Hapa sasa tunaona Ibrahimu ambavyo alikuwa anawashawishi malaika waliotumwa na Mungu kwa ajili ya kuiangamiza Sodoma na Gomora. Mwanzo18:32. “Je! Utaharibu mwenye haki pamoja na mwovu? Huenda wakawapo wenye haki hamsini katika mji, utaharibu wala hutaacha mji.Hasha usifanye hivyo,…BWANA akasema, Nikiona katika Sodoma wenye haki hamsini mjini, nitapaacha kwa ajili yao.”

Ibrahimu aliendelea kusema na wale malaika mpaka akafikia hesabu ya watu 10! Na ibrahimu akaishia hapo, kama Ibrahimu angeendelea kusihi bila shaka maangamizo yasingetokea. (Mwa 18:30-32). Zaidi sana walichokifanya malaika ni kumuondoa Lutu na mkewe na wanawe ambao inaonyesha hawakufika 10 kama wangekuwa 10 wasingetolewa ili mji uangamizwe kwa sababu Ibra alifanya maombi na yakajibiwa kwamba kwa idadi ya watu 10 tu na kama hao 10 wangekuwepo Sodoma na Gomora isingeangamizwa, wangeachwa na Mungu angetumia njia nyingine! Maana Alisema kama wamgekuwa 10 asingeuangamiza mji.    

 
2 Comments

Posted by on June 27, 2020 in Uncategorized

 

SOMO JUU YA MAOMBI (Sehemu 2)

Kwa nini tunazuiwa kuomba? Pamoja na sababu nyingine zinaonekana kama ni za msingi! ANGALIA HII!

(B) MAOMBI YANAWEZA KUBADILI MAAMUZI YA MUNGU ALIYOYAPANGA KWA TAIFA AU KWA MTU N.K.

Hii tunaipata kwa Nabii Isaya! Tusome maandiko haya kwa makini saaana! ISAYA 38:1 “Siku hizo Hezekia aliugua, akawa katika hatari ya kufa; na Isaya nabii, mwana wa Amozi, akaenda kwa mfalme, akamwambia, ‘BWANA asema hivi, Tengeneza mambo ya nyumba yako; maana utakufa,wala hutapona’.”

Ni ujumbe kutoka kwa nabii! Mungu mwenyewe hapo anasema kwamba “UTAKUFA”, hebu jaribu kufikiri! Ingekuwa wewe Mungu anakwambia hivyo ungefanyaje? Lakini mfalme huyu alijua hata kama Mungu amesema, bado ninaweza kubadili maamuzi yake kwa sasa kwa njia ya maombi! Alichokifanya mfalme ni hiki! ISAYA 38:2 “Basi Hezekia akajigeuza, akaelekeza uso wake ukutani, akamwomba BWANA..Hezekia akalia sana sana.” Hezekia alijua na aliamini kwamba maombi yanaweza kubadili maamuzi ya Mungu kabisa! Baada ya maombi hayo Angalia kilichotokea. ISAYA 38:4, “Ikawa, neno la BWANA likamjia Isaya, kusema, Enenda ukamwambie Hezekia, ‘Mimi nimeyasikia maombi yako, nimeyaona machozi yako; tazama nitaziongeza siku zako…”. Hapo kuna vitu viwili Mungu aliviangalia wakati Hezekia anaomba,

(1) Kuomba kwa imani. “Ikawa, neno la BWANA likamjia Isaya, kusema, ‘Enenda ukamwambie Hezekia, Mimi nimeyasikia maombi yako, nimeyaona machozi yako.” (ISAYA 38:4).

(2) Machozi yaliyoambata na kuomba, japokuwa wako watu huwa wanasema walokole wanalialia, tunalia ili Mungu ayapokee maombi yetu, sisi hatulii kama hao waliliao mapenzi usiku na mchana!

Maombi hapa yaligeuza maamuzi ya Mungu, nafikiri sasa unaweza kuelewa kwa nini tunazuiwa kuomba. Ndugu kama unaomba; hata kama ni nani alitamka kitu gani kwako, au katika ukoo wako kwa kulaani laana zozote zile, unakuta familia nyingine hakuna maendeleo yoyote yale pamoja na bidii zote za kufanya kazi na kusoma! Hakuna kuoa wala kuolewa n.k. Maombi yana uwezo wa kubadilisha laana na kuwa baraka na kufumua fumua kila vitu vibaya vinavyohusika kutukandamiza na kutudidimiza katika maeneo fulani fulani. Hata kama bosi alisema nitakusimamisha kazi, maombi yanaweza kubadili maamuzi ya bosi! Kama maombi yaliweza kugeuza maamuzi ya Mungu sembuse bosi ? Sembuse Rais wa nchi?
Twende kwenye mfano wa pili uone maombi ambavyo yanakitu cha kipekee.

 
2 Comments

Posted by on June 26, 2020 in Uncategorized

 

SOMO JUU YA MAOMBI 1

SOMO JUU YA MAOMBI (Sehemu 1)

Wako wakristo ambao tunashindwa kuwa na maisha ya maombi kwa sababu zifuatazo.

(1) Kukosa muda wa kuomba kwa sababu ya majukumu ya muhimu ya hapa na pale.
(2) Mazingira ya mtu anapoishi.
(3) Mwingine hajui faida za maombi wala umuhimu wake.
(4) Mwingine anasema huwa anaishiwa maneno kwa haraka anapokuwa kwenye maombi.
(5) Mwingine hapendi maombi tu!
(6) Shetani.
(7) Mwili.

Katika maombi kuna vikwazo vingi, kwa sababu maombi yana nguvu!

(A) MAOMBI YANAONGEZA UHUSIANO WA MTU NA MUNGU!

Maombi ni mawasiliano baina ya mwanadamu na Mungu au ni njia ambayo tunaweza kuwasiliana na Mungu. Tunafanya mawasiliano na Mungu kwa njia ya maombi, na kama tunavyojua kwamba! Mawasiliano yanaongeza uhusiano wa mtu na mtu, hata wewe ni shahidi katika hili! Unaweza ukawa na ndugu wengi sana au marafiki wengi sana n.k. Lakini yule ambaye atawasiliana na wewe mara kwa mara huyo ndiye anayeukuza ukaribu kupita wengine. Na pia uhusiano wa mtu unaanzishwa kwa mawasiliano na vilevile unaweza ukafa au kupungua kwa kukosa mawasiliano ya mara kwa mara na kuelekezwa kule kwenye mawasiliano ya mara kwa mara! Mawasiliano yamewafanya watu wengi kuwa karibu, kupitia mitandao yetu. Mtu alipoanza mawasilano na wewe kwa njia ya kukutumia ujumbe wa maandishi au wa picha ulipojibu! Mawasilano yakakua mwisho wake ukaribu ukaongezeka kati yako na huyo….

Tunapokuwa tunaomba mara kwa mara uhusiano wetu na Mungu unakuwa kwa kasi sana kuzidi yule asiyeomba, au yule anayeomba mara moja moja au yule anayeomba kwa viwango vya juu zaidi! Na kama tujuavyo, kadiri uhusiano wa mtu na mtu unavyokuwa na kuongekezeka ndivyo wanavyoweza kushirikishana mambo mengi saaaana!

Ndivyo inavyokuwa kwa Mungu kwetu! Kwa sababu mahusiano yetu yanakuwa na kuongezeka! Mungu hataacha kutushirikisha mambo mengi yanayoendelea ili kuyaombea au kuzuia yasitokee au kuwashauri watu n.k. Mungu atatuonyesha hata hatari iliyopo mbele yetu, kwamba! Kuna ajali mbaya itatokea na kusababisha hiki na hiki na jinsi ya kuikwepa n.k. Yakiambatana na maelekezo yake jinsi ya kufanya ambayo yatakuwa na lengo la kujenga na si kubomoa! Utakuwa na furaha na amani wakati woote hata kwenye dhiki za namna gani! Sijui nitumie lugha gani nieleweke jamani: Ili uelewe hili na kulishika kwamba! MAOMBI YANAONGEZA UHUSIANO WA MTU NA MUNGU!

Tuanze maisha ya maombi kuanzia sasa ili uhusiano wetu na Mungu ukue, anzisha mahusiano yako na Mungu kwa kuwasiliana naye mara kwa mara kwa njia ya maombi. Hata kama zamani tulikuwa na bidii ya kuwasiliana na Mungu kwa njia ya maombi halafu tukayakata mawasilano hayo! Bado tunaweza kuyaanzisha upya na kuyakuza! Pia usiache kuwasiliana na Mungu mara kwa mara kwa njia ya maombi kwa sababu kwa kutofanya hivyo utauvunja au utaupunguza uhusianao wako na Mungu!

Marco Bashiri

 
1 Comment

Posted by on June 25, 2020 in Biblia Kiswahili, Maombi, Vita vya Kiroho

 

Tags: , , ,