RSS

MASOMO MAFUPI YA KUTIA MOYO

VITA UNAVYOPITIA MAISHANI VINAKUIMARISHA. USIOGOPE.
KWA MAANA KUJIZOEZA KUPATA NGUVU…
LAANA AU BARAKA
HAPANA UCHAWI JUU YA YAKOBO
MIMI ni THAWABU YAKO KUBWA SANA
TUSEME NINI BASI?
UNAIFUATA MIUJIZA?
MWANA HATAUCHUKUA UOVU WA BABA YAKE
USIPIME UPENDO WA MUNGU KWA MUJIBU WA MAZINGIRA YAKO
YESU MWENYEWE NDIYE NJIA
VIPI TUNAYAHESABU MATESO YA MAISHA YETU?
UPENDO HAUPUNGUI NENO
SIO TAMU. NI SUMU!
BWANA HUUJARIBU MOYO
ABIGAILI NA MAMBO YA NDOA
TATIZO LENYEWE SIYO TATIZO KATIKA MAISHA YAKO YA KIROHO
‘MAMBO YOTE HAYA YAKO KINYUME NAMI.’ BALAA AU BARAKA?
BASI TORATI, KWA KUWA NI KIVULI
JE, NAWEZA KUJUA MAPENZI YA MUNGU KWA MAISHA YANGU?
KUSHINDA HILA YA SHETANI
KUSUDI LA MAJARIBU KATIKA MAISHA YAKO
JE NAWEZA KUJUA MAPENZI YA MUNGU KWA MAISHA YANGU
WEWE NI MFUNGWA WA NINI
NAYAHESABU MAMBO YOTE KUWA NI MAVI ILI NIPATE KRISTO
NIDHAMU ZA MTUMISHI WA MUNGU
JE, UNAPENDA KUWA MTU WA MUNGU
MTU AJULIKANAYE MBINGUNI

1

VITA UNAVYOPITIA MAISHANI VINAKUIMARISHA. USIOGOPE.

Mtu wa Mungu naomba nikutie moyo katika vita unavyopitia maishani. Mungu ameruhusu hivyo vita maana anajua njia ya pekee ya wewe kuendelea kuimarika katika maisha yako ya imani na mahusiano yako na Yeye ni kwa njia ya hivyo vita na hizo changamoto unazopitia maishani.

Kumbuka siku zote uwapo vitani, haijalishi hiyo vita ni kubwa kiasi gani, si kubwa ukilinganisha na vita vilivyo mbele yako katika siku za usoni. Vita vya jana vinakuandaa kwa ajili ya vita vya leo na kadhalika vita vya leo vinakuandaa kwa ajili ya vita vya kesho.

Wakati Daudi akiwa peke yake kule nyikani na kondoo za baba yake, alitokewa na dubu na simba. Daudi angeweza kukimbia maana kw a kweli ukilinganisha dubu na simba na Daudi, Daudi asingekuwa kabisa na uwezo kwa namna ya kawaida kukabiliana nao. Lakini Daudi katika ushuhuda wake kwa Sauli alisema kuwa Mungu alimwokoa na kinywa na makucha ya Dubu na Simba.Ushuhuda wa vita vyake vya jana vilikuwa kianzio vya vita vyake vya leo. Daudi aliandaliwa na vita vyake dhidi ya dubu na simba kukabiliana na Goliati maana Mungu aliyemwona alipokabiliana na dubu na simba alikuwa na uhakika kabisa kuwa ni Mungu atakayemwona atakapokabiliana na Goliati.

Usidharau vita vyako vya leo maana vinakuandaa kwa ajili ya vita kubwa zaidi kesho. Mungu anaikuza imani yako kupitia vita vyako vya leo ili iwe imara vya kutosha kwa ajili ya vita vyako vya kesho.

Usikubali kunyong’onyeshwa na pito lolote la leo.

Chukulia kama ni maandalizi kwa ajili ya mapito makubwa zaidi kesho.

Endelea kumwamini Mungu katika lile ulipitialo leo.

Katikati ya vita unavyopitia ukihakikisha haya unayafanya kwa uaminifu na nidhamu ya hali ya juu utu wako wa ndani utazidi kuimarishwa katika hali hiyo unayopitia.

Kwa hiyo hatulegei; bali ijapokuwa utu wetu wa nje unachakaa, lakini utu wetu wa ndani unafanywa upya siku kwa siku. Maana dhiki yetu nyepesi, iliyo ya muda wa kitambo tu, yatufanyia utukufu wa milele uzidio kuwa mwingi sana; tusiviangalie vinavyoonekana, bali visivyoonekana. Kwa maana vinavyoonekana ni vya muda tu; bali visivyoonekana ni vya milele. (2 KOR. 4:16-18 SUV).

Na Carlos R. W. Kirimbai

RUDI KWA MWANZO

2

KWA MAANA KUJIZOEZA KUPATA NGUVU…

Nataka niseme na sisi kidogo kuhusu mazoezi.

Sio kila mara unapomwona mchezaji anaingia uwanjani anaingia uwanjani kwa ajili ya mechi au mashindano. Mchezaji anaingia uwanjani mara nyingi zaidi kwa ajili ya maandalizi na mazoezi kuliko anavyoingia kwa ajili ya mechi au mashindano. Kiwango cha ufanisi cha mchezaji katika mechi au mashindano kinategemea sana alijiandaaje na mazoezi aliyoyafanya. Kuna mazoezi anayoyafanya mchezaji ambayo yanamwongezea nguvu. Yapo ambayo yanamwongezea pumzi. Yapo yanayomwongezea ujuzi, uwepesi na umahiri.

Ninachojaribu kusema ni ubora wa mchezaji hautokani na uwezo wake wa kucheza au kushindana bali maandalizi yake na mazoezi yake. Kadhalika katika mambo ya rohoni. Maandalizi ni muhimu mno mno mno.

Usisubiri upate shida ndo uombe.

Yapo maombi kwa kusudi la kupata majibu ya mambo mbali mbali maishani alafu yapo yale ambayo ni maandalizi na mazoezi hasa yale ambayo unalazimika kila siku kuamka kuomba. Unapotegea maombi yako binafsi au yale ya kanisani kwenu au kikundi ulichopo unajitegea mwenyewe kwenye maandalizi na mazoezi yako ya kiroho.

Kadhalika usomaji wa neno na kufunga. Vyote hivi ni mazoezi ya kiroho yanayomwimarisha na kumtia nguvu mtu wa ndani ili siku ya mechi (changamoto, taabu, shida, uhitaji) uwe upo vizuri kukabiliana.

Wengi tunafeli siku ya dhiki maana nguvu zetu ni kidogo. Hatujajijengea nidhamu ya kuomba, kusoma neno, kuhudhuria ibada, kufunga nk ambayo itamwimarisha na kumwandaa mtu wetu wa ndani kwa ajili ya siku ya uovu na vita. Kama mazoezi yalivyo ya muhimu kwa ajili ya kumwandaa mwanamichezo hodari, mahiri, mwenye ujuzi, pumzi na nguvu, kadhalika mazoezi ya kiroho ni muhimu mno kwa ajili ya kumwandaa wewe mwenye nguvu za kiroho, pumzi ya kiroho, umahiri na uweledi wa kiroho.

Acha kuendelea kupuuzia mazoezi ya kiroho.

Itakugharimu siku ya vita.

Kumbuka: Jasho jingi mazoezini, damu chache vitani. Jasho kidogo mazoezini, damu nyingi vitani.

“Kwa maana kujizoeza kupata nguvu za mwili kwafaa kidogo, lakini utauwa hufaa kwa mambo yote; yaani, unayo ahadi ya uzima wa sasa, na ya ule utakaokuwapo baadaye.” (1 Ti.4:8).

Na Carlos R. W. Kirimbai

RUDI KWA MWANZO

3

LAANA AU BARAKA (Kum.30:19)

Mtu wa Mungu tunapoyasoma maandiko ya Agano la Kale lazima tusaidiwe na Roho Mtakatifu kuyatafsiri katika muktadha wa Agano Jipya la Neema. Mungu anazishuhudiza mbingu na nchi juu yetu na kusema ameweka mbele yetu uzima na mauti, baraka na laana na anatuambia tuchague uzima ili tuwe hai sisi na uzao wetu. Hili andiko linasema nasi katika Agano Jipya la Neema kuwa unapomchagua Yesu umechagua uzima na baraka na unapomkataa unakuwa umechagua mauti na laana. Kwa wale waaminio hamna kitu kama uzima na mauti bali kuna uzima tu.

Kwa wale waliyoamua kumfanya Yesu Bwana na Mwokozi wa maisha yao hakuna laana na baraka bali kuna baraka tu. Kwa hiyo mtu wa Mungu uwe unayaangalia maandiko ya Agano la Kale na kuyasoma na kuyaelewa katika muktadha sahihi wa Agano Jipya la Neema. Tunapokosea hatujiletei laana bali tunajiletea kurudiwa na Bwana maana Mungu kwetu ni Baba na sio Baba Aliye mwepesi wa hasira yaani tukikosea tu anatulaani. Atatukemea na kuturudi ndiyo lakini kutulaani hapana maana ameshatubariki kwa baraka zote za rohoni katika ulimwengu wa roho ndani ya Kristo Yesu sio kwa sababu ya chochote tulichofanya bali kwa sababu ya kile Yesu alifanya kwa ajili yetu pale msalabani.

Yeye asiyejua dhambi alifanywa dhambi kwa ajili yetu ili sisi tuwe haki ya Mungu katika Kristo Yesu. Kristo alitukomboa toka katika laana ya Torati maana alifanyika laana kwa ajili yetu au kwa maneno mengine badala yetu, maana imeandikwa amelaaniwa kila mmoja aangikwaye juu ya mti ili baraka ya Ibrahimu itufikilie sisi mataifa kupitia Kristo Yesu. Laana zimeshachukuliwa na Yesu kwa hiyo haiwezekani wewe uliye katika Yesu ulaaniwe.

Acha kuwaza mauti na laana anza kuwaza uzima na baraka vilivyo fungu lako katika Kristo Yesu. Roho hushuhudia pamoja na roho zetu kuwa sisi ni wana wa Mungu na kama ni wana basi tu warithi turithio pamoja na Kristo. Kama tu warithi turithio pamoja na Kristo, kama Yesu hawezi rithi laana mimi siwezi kurithi laana. Kama Yesu ni mrithi wa Baraka za Baba Yake mimi pia ni mrithi wa Baraka.

Badilisha unavyofikiri.

Carlos Ricky Wilson Kirimbai

RUDI KWA MWANZO

“HAPANA UCHAWI JUU YA YAKOBO”

Katika Agano la Kale Balaamu hakuweza kuwalaani watu wa Mungu. Balaki alitaka Balaamu awalaani Israel ili kuzuia maendeleo yao, lakini Mungu Mwenyewe alimzuia Balaamu!

Mungu ni Mwamuzi wa watu Wake, siyo mwingine!

Balaamu alilazimishwa kutangaza, “Tazama, nimepewa amri kubariki, Yeye amebariki, NAMI SIWEZI KULITANGUA. Hakika HAPANA UCHAWI JUU YA YAKOBO, wala hapana uganga juu ya Israeli. Sasa habari za Yakobo na Israeli zitasemwa, Ni mambo gani aliyoyatenda Mungu!” (Hesabu 23:20,23).

Unaona? Hata kabla ya kufa kwa Yesu msalabani, haukuwa uchawi juu ya watu wa Mungu, haukuwa uganga dhidi yao! Kwa nini wahubiri wengi wa siku hizi wanawatisha Wakriso kwa mafundisho ya uongo wakidai kama mkristo akiwa na tatizo, shida, ugonjwa, mateso au kutokufanikiwa, inawezekana au hata lazima kutokana na laana – laana kutokana na babu zao, au na nchi yao au hata na shetani nkd! Sio kweli! Ni udanganyifu kabisa. Wahubiri hao wamechanganya kabisa hukumu wa Mungu juu ya watu wake katika Agano la Kale, na laana inayotoakana na uchawi! Hata katika Agano la Kale wachawi hawakuweza kuwagusa watu wa Mungu kwa uchawi na uganga wao! Mungu mwenyewe angewahukumu watu Wake! 

Baada ya kufa kwa Yesu msalabani baraka na ulinzi wa Mungu zimezidishwa kwa wingi katika Kristo Yesu! Kama tunavyofundishwa na Neno la Mungu, “Atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, ALIYETUBARIKI KWA BARAKA ZOTE za rohoni, katika ulimwengu wa roho, ndani yake Kristo.” Kama tumeokoka na “uhai wetu umefichwa pamoja na Kristo katika Mungu” (Wakol.3:3) ndipo hamna laana kutokana na shetani, na wazazi, na mababu, na wachawi au na maneno ya watu ambayo yanaweza kuyajeruhi au kuyaathiri maisha yetu katika Kristo Yesu! Amen!  Haiwezekani! Mungu apewe sifa kwa neema kuu hiyo na kwa wokovu wa ajabu! Usimruhusu mwingine akudanganye au akuchanganyike! “Katika ungwana huo Kristo alituandika huru; kwa hiyo simameni, wala msinaswe tena chini ya kongwa la utumwa.” (Wagal.5:1).

Juu ya shetani neno la Mungu linasema, “Kwa kusudi hili Mwana wa Mungu alidhihirishwa, ili azivunje kazi za Ibilisi.” (1 Yoh.3:8); kuhusu nguvu za giza, “Naye alituokoa katika nguvu za giza, akatuhamisha na kutuingiza katika ufalme wa Mwana wa pendo lake.” (Wakol.1:13).

Mafundisho hayo kuhusu laana ni kinyume cha Biblia, yanapinga moja kwa moja neno la Mungu ambalo linasema, “Kristo alitukomboa katika laana ya torati, kwa kuwa alifanywa laana kwa ajili yetu… ili kwamba baraka ya Ibrahimu iwafikilie Mataifa katika Yesu Kristo, tupate kupokea ahadi ya Roho kwa njia ya imani.” (Wagal.3:13,14). Unaona, Yesu Kristo alitukomboa katika laana ya torati ya Agano la Kale! Wapi mitume kwenye waraka zao wanafundisha au hata kutaja neno mmoja kuwa laana (haijalishi inatoaka wapi!) inaweza kuwatesa, kuwaumiza au kuwadhuru waumini – au kuzuia maendeleo ya maisha ya kiroho ya wakristo? Hamna mafundisho hayo! Wapi Bwana Yesu aliwaonya wanafunzi wake juu ya nguvu za ‘laana’? Hamna! Petro anasema, “Naye ni nani atakayewadhuru, mkiwa wenye juhudi katika mema?”

“Basi, tuseme nini juu ya hayo? Mungu akiwapo upande wetu, ni nani aliye juu yetu? Yeye asiyemwachilia Mwana wake mwenyewe, bali alimtoa kwa ajili yetu sisi sote, atakosaje kutukirimia na mambo yote pamoja naye? Ni nani atakayewashitaki wateule wa Mungu? Mungu ndiye mwenye kuwahesabia haki. 

Ni nani atakayewahukumia adhabu? Kristo Yesu ndiye aliyekufa; naam, na zaidi ya hayo, amefufuka katika wafu, naye yuko mkono wa kuume wa Mungu; tena ndiye anayetuombea.” (Warumi 8:31-34).  

Neema ya Bwana Yesu iwe kwako siku ya leo!

RUDI KWA MWANZO

5

‘‘Usiogope, Abramu. MIMI ni ngao yako na THAWABU YAKO…. KUBWA SANA.’’

Abramu alitaka kupewa mtoto wa kiume. Je, Mungu hakusema, “Mimi nitakufanya taifa kubwa na nitakubariki”? Basi, Abramu alikuwa anawaza sana juu ya hivyo; alikuwa anatumaini, anatarijia apate mtoto. Lakini Mungu alikatisha mawazo yake, tumaini lake na matarajio yake…

“…neno la BWANA likamjia Abramu katika maono: Usiogope, Abramu. MIMI ni ngao yako na thawabu yako kubwa sana.” (Mwanzo 15:1).

Kabla ya kupokea mambo yale tunayoyahesabu muhimu na ya thamani saaaana kwa maisha yetu, hata baraka za dhati, lazima tumeitengenza mioyo yetu kumdhamini na kumpenda Mungu na Mwokozi wetu kuliko yote nyingine – lazima tumhesabu Mungu thamani kiasi cha kuhesabu mambo yote nyingine si kitu kulinganisha na kumjua na kumpenda Yeye! Lazima kumhesabu siyo ‘thawabu yetu’ tu, bali ‘thawabu yetu KUBWA SANA’. Ndipo tu tutakapokuwa tayari kuipokea ‘baraka’ zingine za dhati. Je, tupo tayari kumruhusu Mungu kukatisha matarajio yetu na neno lake? Je, tupo tayari Mungu atuongoze kwa njia Yake na kutubariki kwa wakati auchaguaye Yeye? Na kufanya hiyo bila kuingojea ngojea kwa kutoksubiri ‘baraka’ ifike, bali kumpokea Bwana, na kufurahi katika Bwana kama thawabu yetu kubwa sana? Tunajua Abrahamu alikuwa na tabia ya namna hiyo, kwa sababu baadaye alikuwa tayari kutoa mwana wake wa pekee aliyempenda kama dhabihu kwa ajili ya Mungu wake!

Je, unamtafuta mchumba, unataka kuoa au kuolewa, kuwa mwimbaji, au unatafuta huduma au kufanikiwa katika kazi au biashara yako…..

‘‘Usiogope. MIMI ni ngao yako na THAWABU YAKO…. KUBWA SANA.’’

Sisemi tutapata tutakalo, lakini tutapata lile bora kabisa, duniani na kwa milele!

Haifai kama maneno haya yakizigusu hisia zetu kwa saa moja, au siku moja, au hata wiki moja. Lazima ukweli huo uingie mioyo yetu na uwe tabia yetu daima. Mungu atusaidie kwa neema Yake kuu siku ya leo tumchague awe thawabu yetu kubwa sana! Amen.

RUDI KWA MWANZO

6

TUSEME NINI BASI?

LAZIMA KILA MTU AJIBU SWALI HILI:

‘Tuseme nini basi? Je, tuendelee kutenda dhambi…’ (Warumi 6:1)

Paulo anajibu, ‘Hasha!’

Au, ‘Je, tuendelee kutenda dhambi ili neema ipate kuongezeka?

Paulo anajibu, ‘Hasha!’

Yeye anatuuliza tena, ‘Sisi tulioifia dhambi TUTAISHIJE TENA katika dhambi?’ 

Tuseme nini? Tujibu nini?

Paulo anaeleza. ‘mkijua neno hili, ya kuwa utu wetu wa kale ulisulibishwa pamoja naye, ili mwili wa dhambi ubatilike, TUSITUMIKIE DHAMBI TENA.’

Wengine wanajaribu kuleta kisingizio, udhuru au kisababu kwa kutenda dhambi kwa njia ya kunukulu 1 Yoh.1:10. Lakini Yohana anaendelea kusema katika mstari ufuatao, ‘nawaandikia haya ili kwamba MSITENDE dhambi.’. Zaidi ya hayo, anatufundisha kwamba, ‘Kila mtu aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi, …wala hawezi kutenda dhambi kwa sababu amezaliwa KUTOKANA NA MUNGU.’ (1 Yoh.3:9). 

Wakristo kweli kweli wamezaliwa kutokana na Mungu. ‘Kwa kusudi hili Mwana wa Mungu alidhihirishwa, ili AZIVUNJE kazi za Ibilisi.’ Na kazi ya Ibilisi ni nini? ‘Ibilisi HUTENDA DHAMBI tangu mwanzo.’ Kwa hiyo Yohana anafundisha, ‘atendaye dhambi ni wa Ibilisi.’ Yesu alisema kwamba, ‘Ninyi mkikaa katika neno langu, mmekuwa wanafunzi wangu kweli kweli tena mtaifahamu kweli, nayo hiyo kweli ITAWAWEKA HURU.’  (Yoh.8:32).

Watu wa dini hawakuelewa maneno ya Yesu, walifikiri DINI YAO iliwaweka huru! Lakini Yesu alieleza kwa wazi!  ‘Amin, amin, nawaambia, Kila atendaye dhambi ni MTUMWA WA DHAMBI…Basi Mwana akiwaweka huru, MTAKUWA HURU KWELI KWELI.’ Basi Yesu aliweka wazi kwamba uhuru ule ambao Yesu huwapa watu ni kuwaweka huru mbali na dhambi! Yohana na Paulo wanakubiliana na yale Yesu aliyoyasema. Paulo anasema, ‘Mungu na ashukuriwe, kwa maana MLIKUWA watumwa wa dhambi… na mlipokwisha KUWEKWA HURU MBALI NA DHAMBI, mkawa WATUMWA WA HAKI.’ (Warumi 6:17,18).

Sasa nini, au nani atakuokoa na dhambi zako; nini au nani utakuweka huru mbali na dhambi? Kifo cha mwili wako utakapokufa? Au Yesu Kristo siku hiyo hiyo? Unasemaje?

‘…utamwita jina lake Yesu, maana, yeye ndiye atakayewaokoa watu wake na dhambi zao.’ (Mat.1:21).

Kwa kweli ni wokovu mkuu! 

RUDI KWA MWANZO

7

UKIIFUATA MIUJIZA TU, YESU HATAKUWA MFALME WAKO.

Yesu alifanya muujiza. Aliwalisha waume elfu tano kutokana na mikate mitano na samaki wawili. Ndipo tunasoma, “Kisha Yesu, hali akitambua ya kuwa walitaka kuja kumshika ili wamfanye mfalme, AKAJITENGA, akaenda tena mlimani yeye PEKE YAKE.” (Yoh.6:15). Kwa nini Bwana Yesu alijitenga? Ilionekana kuwa nafasi ya ajabu awe mfalme juu ya watu!

Hapana! Watu wale walitaka kumfanya Yesu mfalme KWA AJILI YA FAIDA YAO TU ili wapate baraka za kimwili au za nje tu! Inawezekana walijiambia kama yafuatavyo: “Kumbe! Anafanya miujiza! Hatutahitaji cho chote tena! Yeye atatubariki kupita kiasi na sisi tutafanikiwa! Atabadilisha mazingira yetu! Ataondoa maadui zetu Warumi! Atatuletea mafanikio! Ataboresha maisha yetu! Biashara yetu itafanikiwa, na yote tulilolitaka, yametimizwa! Twende tumfanye mfalme!” Vivyo hivyo hayo yanatokea siku hizi. Watu wanaifuata miujiza na baraka za kimwili kuliko kumfuata Yesu na njia Yake.

Miujiza siyo tatizo. Tatizo linaweza kuwa lengo letu la kiini la kumfuata Yesu.

Bwana Yesu, Yeye aliye na macho yake kama mwali wa moto, huangalia na kuchunguza makasudi (motives) yetu kweli kweli yaliyoweza kufichwa ndani sana ya mioyo yetu! (Waebr.4:12). Watu wanaweza kusema hivi na hivi, wanaweza kuwa na hamu kwa ajili hivi na hivi, hata kumfuata Yeye, lakini Yesu anachunguza makusudi kweli kweli ya mioyo yetu! Maneno ya Yesu yanaingia mioyo yetu moja kwa moja kuuliza, “Unataka nini?” Yesu hatafuti kuwakusanya watu kujenga ‘umaarufu’ wake kupitia ‘miujiza’ au ‘upako’ wake! Kwa maneno yake na kazi yake katika maisha yetu, Yesu Kristo anachunguza chunguza mioyo yetu mpaka makasudi yetu ya kiini kabisa yamefunuliwa; mpaka tutakapotoa maisha yetu Kwake kabisa, bila masharti yoyote kwa upande wetu, bila manung’uniko yoyote; tuwe tayari tupate hasara ili tupate Kristo na uzuri usio na kiasi wa kumjua Yeye! (Wafilipi 3:8).

Je, na wewe na mimi, tunataka mfalme wa namna ileile Wayahudi kwenye Yohana 6 walivyomtaka? Kama ni hivyo, huwezi kumfuata Mwokozi Yesu Kristo! Huwezi kuwa mwanafunzi Wake – humjui, huitambui tabia Yake. Atajitenga nawe. Yesu alikataa KABISA kuwa mfalme juu ya msingi wa kujipendeza kwa watu! Alijitenga na akaenda mlimani peke Yake. Je, utamfuata pale, pale jangwani, mlimani, pale ambapo hakuna cho chote ILA YESU TU na MSALABA wake?

Je, Yesu Mwenyewe tu anatosha kwako na kwangu? Tunaimba, “Wewe tu ndiwe utoshaye.” Je, ni kweli kwako na kwangu kila siku?

Tunataka nini? Tunatafuta nini?

Yesu alisema, “Akawaambia WOTE, Mtu ye yote akitaka kunifuata, na ajikane mwenyewe, ajitwike msalaba wake kila siku, anifuate… Basi, kadhalika kila mmoja wenu asiyeacha vyote alivyo navyo, hawezi kuwa mwanafunzi wangu. (Luka 9:23; 14:33).

Hayo ni msingi wa kumfuata Yesu Kristo. Je, ninampenda Yesu kuliko baraka za kimwili, kuliko miujiza, kuliko ‘mafanikio’, kuliko huduma yangu, kuliko sifa yangu mbele ya watu, kuliko baba au mama au mume au mke au watoto wangu? Yesu alitoa maisha yake kwa ajili yetu ili atupate kabisa, kwa ndani, kwa milele. Ni Mwokozi wa ajabu anayestahili tutoe maisha yetu yawe dhabihu yalio hai mbele Yake daima.

Mungu alibariki neno lake kwa mioyo yetu!

RUDI KWA MWANZO

8

“Roho itendayo dhambi, ndiyo itakayokufa; MWANA HATAUCHUKUA UOVU WA BABA YAKE, wala baba hatauchukua uovu wa mwanawe.” (Ezekiel 18:20).

Mungu aliwakemea sana wana wa Israel kwa sababu waliamini watoto hudhurika na kuadhiriwa na dhambi za wazazi wao! Na wahubiri wengi siku hizi wanastahili kukemewa pia kwa kufundisha yaleyale, kana kwamba muumini kweli anaweza kubeba laana kutokana na dhambi za wazazi wake! Huo ni uongo kubwa ya namna gani? Mungu anaendelea kuwakemea Waisraeli, “Je! Maana yake ni nini hata mkatumia mithali hii katika Israeli, mkisema, Baba wamekula zabibu mbichi, nao watoto wakatiwa ganzi la meno? KAMA MIMI NIISHIVYO, asema Bwana MUNGU, HAMTAKUWA NA SABABU ya kuitumia tena mithali hii katika Israeli….Lakini ninyi mwasema, Kwani yule mwana asiuchukue uovu wa baba yake? Yule mwana atakapofanya yaliyo halali na haki, na kuzishika amri zangu na kuzitenda, hakika ataishi.” (Ezekiel 18:2,3,19). Kumbuka, hayo yote yalikuwa kweli kabla ya Yesu hajakufa na kufufuka! Aidha, hata katika Agano la Kale uchawi haukuweza kuathiri wala kudhuru watu wa Mungu walioongozwa naye! Sikiliza!

“Mungu SI MTU, aseme uongo; Wala si mwanadamu, ajute; Iwapo amesema, hatalitenda? Iwapo amenena, hatalifikiliza? Tazama, NIMEPEWA AMRI KUBARIKI, Yeye amebariki, nami SIWEZI KULITANGUA. …Bwana, Mungu wake, yu pamoja naye, Na sauti kuu ya mfalme i katikati yao. Hakika HAPANA UCHAWI JUU YA YAKOBO, Wala HAPANA UGANGA JUU YA ISRAELI. Sasa habari za Yakobo na Israeli zitasemwa, NI MAMBO GANI ALIYOYATENDA MUNGU!” (Hesabu 23:19-23).

Kumbuka, hayo yalikuwa kweli wakati wa Agano la Kale! Je, ni mambo gani aliyoyatenda Mungu kwa ajili yetu SASA kupitia Mwanawe Yesu Kristo? Sikiliza, “Atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, aliyetubariki kwa baraka zote za rohoni, katika ulimwengu wa roho, ndani yake Kristo.” (Waefeso 1:3).

Pamoja na hayo, neno la Mungu linatudhihirsha ukweli ufuatao: “Kristo alitukomboa katika laana ya torati…” (Wagal.3:13).

Kutokana na hayo tunaona wote wanaofundisha kuwa maisha ya Mkristo (ya kimwili na kiroho) anaweza kushambuliwa na kudhurika na laana yanatokana na uchawi au na dhambi ya wazazi, wanapinga neno la Mungu na wanakaribia kujiweka chini ya hatari ya Wagalatia 1:6-8. Kwa hiyo,

“Katika ungwana huo Kristo alituandika huru; kwa hiyo simameni, wala msinaswe tena chini ya kongwa la utumwa.”

RUDI KWA MWANZO

9

USIPIME UPENDO WA MUNGU KWA MUJIBU WA MAZINGIRA YAKO! UTAPIMA KWA UJINGA TU. Ukitaka kupima upendo wa Mungu kwako, TAZAMA KALVARI TU! Hapo hapo utatambua kiwango cha upendo wa Mungu kwa ajili yako!

“Basi imani…ni bayana ya mambo yasiyoonekana.” (Waebr.11:1).

Wengi wanaweza kumwamini na kumsifu Mungu wakati anapofanya mambo kwa ajili yao. Lakini kwa wengi ni shida kumwamini Mungu wakati INAONEKANA asipofanya cho chote kwa ajili yao. Kwa hiyo Mungu anasema, “Kama mkiisikia sauti yake leo, msiifanye migumu mioyo yenu kama mlivyofanya kule Meriba kama mlivyofanya siku ile kule Masab jangwani, ambapo baba zenu walinijaribu na kunipima, ingawa walikuwa wameyaona niliyoyafanya.” (Zaburi 95:7-9). Baada ya kutoka Misri, watu wa Mungu waliimba kwa furaha kubwa mbele ya Mungu, lakini baada ya hapo hawakupata maji ya kunywa na mara moja walimnung’unikia Musa, yaani, kwa msingi walimnung’unikia Mungu!

Kwa urahisi waliacha kumwamini Mungu. Kwa kutokuamini huku tunaifanya migumu mioyo yetu na hatutajua raha ya Mungu. Biblia inatufundisha, “kujaribiwa kwa imani yenu, ambayo ina THAMANI KUU kuliko dhahabu ipoteayo, ijapokuwa hiyo hujaribiwa kwa moto, kuonekane kuwa kwenye sifa na utukufu na heshima, katika kufunuliwa kwake Yesu Kristo.” (1 Petro 1:7). Kumwamini Mungu wakati wa shida na matatizo, hasa wakati INAONEKANA Mungu hafanyi cho chote kwa ajli yetu, NI THAMANI KUU KULIKO DHAHABU.

Shadraki, Meshaki na Abednego walijibu mfalme Nebukadneza kwa na maneno ya ajabu:

“Ee Nebukadneza, hatuhitaji kujitetea wenyewe mbele zako kuhusu jambo hili, ikiwa tutatupwa ndani ya tanuru iwakayo moto, Mungu tunayemtumikia ANAWEZA KUTUOKOA na moto, naye atatuokoa kutoka mkononi mwako, Ee mfalme. Lakini HATA IKIWA HATATUOKOA, Ee mfalme, tunataka ufahamu kwamba, HATUTAITUMIKIA miungu yako wala kuiabudu sanamu ya dhahabu uliyoisimamisha.’’ (Danieli 3:16-18).

Watu watatu hawa walimamini Mungu HAIJALISHI Mungu afanyalo au asilofanya kwa ajili yao! (Na wewe?). HIYO NI IMANI.

Shida kwa wengi ni ifuatayo: wanajua Mungu anaweza kufanya lo lote (tunaimba ‘Yote yawezekana’). Lakini kama ‘inaonekana’ kuwa Mungu hafanyi cho chote kwa ajili yao wakati wakipitia kipindi cha shida na majaribu, wanachukizwa na wanaamini Mungu amewaacha! Wanakosa kwa kufikiri dalili ya pekee ya uwepo wa Mungu nao ni ‘baraka’ (za kimwili). Wanaishi kwa ‘kuviangilia vinavyoonekana tu na siyo kwa visivyoonekana’. Kama ‘baraka’ zipo katika maisha yao, wanaamini ina maana Mungu ‘yupo’ na wanaimba kwa furaha ‘Mungu yu mwema’. Kama ‘INAONEKANA’ Mungu anawanyima watu hao baraka yake, mara moja wananungunika, kuchukizwa na kufikiri Mungu wamewaacha na hata wanawachukia, vile vile Waisraeli walivyofanya, “…mkanung’unika hemani mwenu, mkasema, Ni kwa sababu Bwana AMETUCHUKIA, ndipo akatutoa katika nchi ya Misri, apate kututia katika mikono ya Waamori, ili KUTUANGAMIZA.” (Kumbu.1:27). Mapenzi ya Mungu yalikuwa kuwabariki Waisraeli KUPITIA KIASI kwa kuwaongoza katika nchi ya Ahadi, kwa sababu ALIWAPENDA SANA! Lakini kumbe, kwa sababu HAWAKUELEWA njia ya Bwana – kwa sababu ya KUTOKUAMINI kwao! – walifikiri Mungu aliwachukia na hata alitaka kuwaangamiza!

Na sisi? Imani yetu iko wapi? Una imani kwa Bwana au kwa ‘baraka’? Tafakari swali hili kwa makini moyoni mwako kabla ya kujibu. Shadraki, Meshaki na Abednego walimwamini Mungu TU, bila kujali mazingira yao, bila kutazamia lazima Mungu abadilishe mazingira yao!

Imani yao haikutegemei na mambo Mungu aliyofanya au asiyofanya kwa ajili yao!

Na sisi? Je, tunaishi kwa ‘kuviangilia vinavyoonekana au visivyoonekana’?

Tatizo kubwa sana kwa Ayubu lilikwa hakujua SABABU ya mambo yale yaliyotokea ambayo yalimletea maumivu makali yale katika maisha yake! Hii ni changamoto kubwa kwetu pia, yaani, kupita pagumu bila kujua sababu! Kwa kweli, hii ni kujaribiwa kwa imani yetu! Kwa hiyo, tukipita pagumu tusimlaumu Mungu bali tukumbuke na tuamini kuwa anatuwazia mema tu. Mungu wetu ni mwaminifu na hawezi kutuacha, hutupa majaribu kwa sababu ametuandalia ushindi katika majaribu hayo tupitiayo. Hivyo basi tukatae kushawishiwa na shetani ili tumchukie au kumlaumu Mungu kwa sababu ya shida tunazopitia. Kumbuka Shadraki, Meshaki na Abednego! Imani yao ilijaribiwa kwa moto wa dhati! Lakini mwishoni imani yao ilimtukuza Mungu mbele ya watu wote! Itakuwa vivyo hivyo kwako kama ukiishi kwa imani, hata kama ilijaribiwa ‘kwa moto’. Siku ile imani yetu itaonekana kuwa kwenye sifa na utukufu na heshima, katika kufunuliwa kwake Yesu Kristo. Kumbuka pia, ni wapi Shadraki, Meshaki na Abednego walipokuta naye Yesu? Katika moto!

Usipime upendo wa Mungu kwa mujibu wa mazingira yako! Utapima kwa ujinga tu. Ukitaka kupima upendo wa Mungu kwako, TAZAMA KALVARI TU! Hapo hapo utatambua kiwango cha upendo wa Mungu kwa ajili yako!

“Basi IMANI ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni bayana ya mambo YASIYOONEKANA.”

“Kama mkiisikia sauti yake leo, MSIIFANYE MIGUMU mioyo yenu.”

RUDI KWA MWANZO

10

YESU mwenyewe ndiye njia. Biblia haisemi ujuzi au maarifa kuhusu Yesu ni njia. Yesu Mwenyewe ndiye Njia. “MIMI ndimi njia.” (Yoh.14:6). Yaani, tabia Yake ni njia! YESU ndiye uzima. Siyo kujifunza au kujua mambo juu ya Yesu ni uzima. YESU MWENYEWE ndiye uzima.

“Na huu ndio ushuhuda, ya kwamba Mungu alitupa uzima wa milele; NA UZIMA HUU UMO KATIKA MWANAWE (1 Yoh.5:11).

Haitoshi kuyajua mambo mengi KUHUSU Yesu Kristo. Lazima tuwe ndani Yake na Yeye awe ndani yetu. Kwa hiyo pia Paulo anasema,

“Twajua ya kuwa sisi sote tuna ujuzi. Ujuzi huleta majivuno, bali upendo hujenga.” (1Wakor.8:1);

na Yohana anasema, “Ye yote anayesema anakaa ndani Yake hana budi kuenenda kama Yesu alivyoenenda.” (1 Yoh.2:6).

Ni changamoto. Lakini imeandikwa, “Mungu ashukuriwe, anayetushangiliza daima katika Kristo, na kuidhihirisha HARUFU YA KUMJUA YEYE kila mahali kupitia sisi. Kwa maana sisi tuwe MANUKATO YA KRISTO, mbele za Mungu, katika wao wanaookolewa, na katika wao wanaopotea.” (2 Wakor.2:14,15).

Unaona? Kusudi la Mungu ndilo tuwe manukato ya Kristo mbele ya watu na mbele ya Mungu; tuidhihirishe harafu ya KUMJUA Yeye. Ni jambo la tabia, siyo la ujuzi. Inagusa halisia ya maisha yetu – kama ninamjua Yesu au ninajua juu Yake tu. Kama ninao ujuzi tu JUU YA Yesu, nitakuwa na harufu ya utupu au kiburi mbele ya watu na nitatembea kama mtu kipofu.

Uzima wa milele ni nini? Kujua mengi juu ya Yesu? Hapana. Bwana Yesu ameshaufunuliwa kwetu,

“uzima wa milele ndio huu, WAKUJUE WEWE, Mungu wa pekee wa kweli, na Yesu Kristo uliyemtuma.” (Yoh.17:3).

Je, naweza kuyajua mengi juu ya Yesu bila kumjua? Ndiyo. “Yeye asemaye, Nimemjua, wala hazishiki amri zake, ni mwongo, wala kweli haimo ndani yake.” (1 Yoh.2:4). Hatuwezi kumjua Yesu na Baba Yake isipokuwa sisi tubadilishwe siku hadi siku tufanane na mfano wa Bwana toka utukufu hata utukufu. (2 Wakor.3:18). Njia moja ya ulazima sana ambayo tunapata kumjua Yeye nidyo kupitia USHIRIKA wetu naye – tunabadilishwa na mambo yale tunayoshirikana nayo katika mioyo, akili na roho zetu! Tabia yetu na mwenendo wetu ni matokeo ya ushirika wetu – ushirika wetu iwe na mambo mabaya au mazuri. Bila shaka tunashirikiana na jambo fulani muda wote mioyoni na akilini zetu. Je, tunatumia na kushika muda ili tupate nafasi tuwe na ushirika na Baba na Mwana – siyo kuomba kwa ajili ya mahitaji tu, bali kushirikiana na Baba na Mwana katika upendo na kubadilishwa na ushirika huo! (1 Yoh.1:3). Na tutambue, Yesu Kristo alimwagika damu yake ili tuingize katika ushirika huo. Je, kipo kitu kikuu kuliko kuujua ushirika na Baba na Mwana?

Mistari hiyo ndio neno la Mungu kwangu, na neno la Mungu kwako. Nategemea mambo hayo siyo jambo geni kwetu! Kama ni jambo geni kwako, ujitoe maisha yako Mwokozi Yesu Kristo kabisa, siyo ovyoovyo, bali kwa moyo wako wote; omba unalohitaji kuomba. Na mwombe Mungu akuongoze kuingia katika ushirika Naye na akujaze na Roho Wake ili umjue kwelikweli. Paulo aliomba akisema, “siachi kutoa shukrani kwa ajili yenu; nikiwakumbuka katika sala zangu, Mungu wa Bwana wetu Yesu Kristo, Baba wa utukufu, awape ninyi roho ya hekima na ya ufunuo KATIKA KUMJUA YEYE; (Waefeso 1:16,17). Amen.

Na Yesu awe maisha na njia yetu – nyumbani, shuleni, kazini, barabarani na kanisani.

RUDI KWA MWANZO

11

Je, vipi tunayahesabu mateso ya maisha yetu? Je, tunafikiri pengine dhiki na mateso ya maisha yetu yanazidi kupita kiasi – kiasi ambacho hatuwezi kukivumilia? Ni mzigo ambao hatuwezi kuubeba, na tunakata tamaa? Je, tunazama katika mambo ya magumu ya maisha? Paulo hakusita kutangaza ukweli huu,

“Kwa maana nayahesabu mateso ya wakati huu wa sasa kuwa si kitu kama utukufu ule utakaofunuliwa kwetu.” (Warumi 8:18).

Je, mtume Paulo hakuyakuta na mateso katika maisha yake? Kinyume chake! Yeye alipata mateso zaidi ya karibu watu wote! (2 Wakor.6:48; 11:2328). Lakini aliyahesabu ‘si kitu’! Utukufu ule utakaofunuliwa kwetu ni mkuu mno kuliko mateso ya maisha yetu kiasi cha kutokuweza kulinganisha utukufu ule na mateso ya maisha yetu! Je, hiyo ni nia yetu? Utukufu ule ni wa milele! Lakini juu ya matatizo yetu, neno la Mungu linatufundisha kwamba,

“Maana dhiki yetu nyepesi, iliyo ya muda wa kitambo tu, yatufanyia utukufu wa milele uzidio kuwa mwingi sana.” (2 Wakor.4:17).

Kumbe, Paulo ni muumini wa namna gani! Anasema ‘dhiki yetu nyepesi’ na tena ‘ya muda wa kitambo tu’! Lakini hiyo siyo maneno na mtu tu – ni ukweli wa Mungu kwa mioyo yetu. Je, tunaishi kwa nia hiyo na kadiri ya ukweli huo? Haitoshi kufikiria ukweli huo kwa dakikia kadhaa, au kwa siku moja tu. Lazima ukweli huo uingie moyoni mwako kwa kina sana na kubadilisha nia yako ili uyahesabu mateso ya maisha yako kwa macho mapya! Vipi? Njia moja ni kama ifautavyo,

“tusiviangalie vinavyoonekana, bali visivyoonekana. Kwa maana vinavyoonekana ni vya muda tu; bali visivyoonekana ni vya milele.” (2 Wakor.4:18).

Lakini tunahitaji saburi na ustahimili,

“Basi msiutupe ujasiri wenu, kwa maana una thawabu kuu. Maana mnahitaji saburi, ili kwamba mkiisha kuyafanya mapenzi ya Mungu mpate ile ahadi.” (Waebr.10:35,36).

Na Paulo anatufafanulia kwamba, “Jaribu halikuwapata ninyi, isipokuwa lililo kawaida ya wanadamu; ila Mungu ni mwaminifu; ambaye hatawaacha mjaribiwe kupita mwezavyo; lakini pamoja na lile jaribu atafanya na mlango wa kutokea, ili mweze kustahimili.” (1 Wakor.10:13)

Na mwandishi wa Waraka kwa Waebrania anatutia moyo kwa maneno haya pia,

“Sasa bado hatujaona vitu vyote kutiwa chini yake, ILA TWAMWONA YEYE,’ yaani, Yesu! (Waebr.2: 8,9).

Mungu atubariki siku ya leo ili “tuweke kando kila mzigo mzito, na dhambi ile ituzingayo kwa upesi; na tupige mbio kwa saburi katika yale mashindano yaliyowekwa mbele yetu, TUKIMTAZAMA YESU.”  Amina!

RUDI KWA MWANZO

12

UPENDO HAUPUNGUI NENO

Yesu alikuwa amewapenda watu wake katika ulimwengu, aliwapenda UPEO, MPAKA MWISHO. Waume, wapendeni wake zenu, vivyo hivyo. Wake, wapendeni waume zenu, vivyo hivyo, kwani…

…upendo HUVUMILIA yote. Upendo hustahimili YOTE. Upendo hautafuti mambo YAKE. Upendo haupungui neno WAKATI WO WOTE. Kwani Mungu ni upendo.

Haiwezekani? Lakini kumbuka, tunaimba ‘Yote yawezekana.’ Na neno Lake linatuambia kwamba HAKUNA neno lisilowezekana kwa Mungu.

Je, tunatembea na Mungu?

“Neema yangu yakutosha.” Je, unadai haitoshi?

Unapaswa kujibu maswali hayo mbili kwa dhati.

Kama umejibu neema yake haitoshi, maisha ya kiroho yako wapi?

Tatizo ni nini?

Tunaimba, ‘Siyo mimi ninayeishi, bali Kristo ndani yangu!’ Lakini mke au mume wako anajua kama hiyo ni kweli nyumbani au sivyo! Tatizo ni hili: SISI tunataka KUISHI badala ya kujinyenyekeza mbele ya Mungu ili Kristo aishi ndani yetu. Tunasisitiza kushika HAKI YETU yenyewe na kutangaza ‘siyo sawa!’ Tunakataa tusife (kusulibiwa pamoja na Kristo)!

Tunaanguka katika kujihurumia. Hiyo ni jambo la kujipenda na kutokujali neno la Mungu.Tunachukizwa, kukasirika na tunapatwa na uchungu. Hiyo ni jambo la kiburi.

Hayo ndiyo matatizo ya watu. Tufanyaje?

‘Mungu HUWAPINGA wajikuzao, bali HUWAPA NEEMA wanyenyekevu.’ (Yakobo 4:6). Waumini wengi wanapungukiwa na neema kwa sababu ya hiyo, yaani, wanakataa ‘kunyenyekea chini ya mkono wa Mungu.’ (1 Petro 5:6).

Lakini maandiko yanasema, ‘..hutujalia sisi neema iliyozidi.’ (Yakobo 4:6). Au unadai siyo hivyo?

Njia yetu ni kujinyenyekea ‘chini ya mkono wa Mungu.’

Lakini tusifikiri hilo ni jambo gumu kana kwamba lazima sasa nibebe mzigo nzito kila siku! Hapana! Neno la Mungu linatangaza kwamba, “Kwa maana huku ndiko kumpenda Mungu, kwamba tuzishike amri zake; wala amri zake si nzito.” (Yoh.5:3); na Yesu amewaita watu kwa maneno hayo, “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha. Jitieni NIRA YANGU, mjifunze KWANGU; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi MTAPATA RAHA nafsini mwenu; kwa maana nira yangu ni LAINI, na mzigo wangu ni MWEPESI.”

Ungweza kwenda kwa ‘Semina ya Ndoa’ (tena?) au kununua kitabu kingine juu ya mada hiyo, na labda ‘ungejifunza’ mambo yaliyofaa. Lakini kama usipo tayari kujinyenyekea chini ya mkono wa Mungu na kupokea kwa upole neno lile lililopandwa ndani (Yakobo 1:21) katika MAMBO YALE yanayotokea nyumbani mwako kila siku, hutapata faida yo yote kupitia ‘Semina ya Ndoa’ au kitabu chochote.

Jambo hili ni muhimu sana, na hamna ‘Siri ya Ndoa yenye Furaha’, siyo jambo la kujifunza ‘mbinu wa kufanikiwa’, hata siyo jambo la saikolojia. Jambo hili linahusu uhusiano wako na Mungu na hali ya moyo wako mbele Yake! Linahusu uhusiano wako na neno la Mungu na kama utaishi sawasawa na neno Lake au la. Hiyo tu.

Twende katika njia ile ambaye Bwana Yesu ameshatutayarishia.

Upendo haupungui neno wakati wo wote kwani Upendo hautafuti mambo yake.

Mungu alibariki neno lake kwetu.

RUDI KWA MWANZO

13

SIO TAMU. NI SUMU! Picha za machafu kwenye mtandao.

“Tafuteni kwa bidii…huo utakatifu, ambao hapana mtu atakayemwona Bwana asipokuwa nao.” (Waebr.12:14).

Swali ni hili. Je, mimi ni mtu wa dini tu anayeishi dhambini, au nimezaliwa kwa Roho ya Mungu, nimewekwa huru mbali na dhambi, na ninashinda dhambi kwa neema ya Mungu? Lengo la agizo la Mungu ni ‘upendo utokao katika moyo safi.’ (1 Tim.1:5). Basi, kama tukipenda kuziona picha za machafu kwenye mtandao au mahali po pote mengine, jinsi tunavyoweza kumwona Bwana siku ile? Kama tunajifurahisha na mambo machafu kwenye mtandao, ujuzi wetu wote juu ya Injili hautaweza kutuokoa au kutusaidia siku ile. Kama tunapenda kuziona picha za machafu, hatutaurithi ufalme wa Mungu. Picha za ngono kwenye mtandao ni sumu ya kiroho! Ni dhambi kubwa sana kuziona. Itaangamiza maisha yako ya kiroho. Zinajaza akili yako na mawazo machafu, na mawazo haya yanapelekea kufanya matendo machafu – zitayaangamiza maisha yako kabisa! Kama tukicheza na dhambi hiyo, hatuwezi kuwahudumia wengine! Tunajidanganya tu. Kwa nini ‘waumini’ sio wachache wamejiunga na facebook groups zinazoonyesha picha za machafu? Siyo tamu! Ni sumu! Kila mara dhambi hutaka kuwavuta watu ikidai ni kitu kitamu! Shetani husema, “Hutakufa! Ni tamu! Utajifurahisha!” Lakini inaleta kifo! Wengine wanajidai ni wakristo lakini hatuwezi kumtumikia Bwana na kuitumikia dhambi. Inanihuzunisha sana kwamba wao wanaodai kuwa waumini wanafurahia kuangalia picha za namna hizo. [Kama mtu mwingine alilibandikisha jina lako na group kama hiyo bila wewe kuja (hiyo ni kosa la facebook), mara unapotambua, zifute tu! – vinginevyo watu wengine wanapoona facebook yako watafikiri ulijiunga kwa kusudi! ]

Bwana Yesu ameitayarisha njia ya kukusamehe, kukusafisha na kukweka huru mbali na dhambi. 

RUDI KWA MWANZO

14

“KALIBU NI KWA FEDHA NA TANURU KWA DHAHABU, BALI BWANA HUUJARIBU MOYO.” (Mithali 17:3).

Kazi ya kupata dhahabu safi kabisa ni ngumu sana na inahitaji moto mkali sana ili kuitenga na mambo mengine tusiyoyataka na yasiyofaa!  Vile vile neno la Bwana linafanya kazi ndani ya mioyo na maisha yetu kama kalibu na tanuru ili kutofautishiana kati ya maneno na hamu yetu (na yale tunayoyadai), na makusudi yetu kweli kweli ndani ya mioyo yetu! Mungu ni mwaminifu na mwenye neema, rehema na uvumilivu katika kazi hii ili tufananishwe na Mwana Wake Yesu Kristo hapa duniani. Kwa hiyo, tuziache ngao zetu za nje tulizozitengeneza na kuijenga kwa ajili ya watu ili tujionyeshe vizuri au hata tuonekane kuwa na adabu. Macho ya Bwana ni kama mwali wa moto yanayochunguza kwa kiini sana mioyo yetu. Na tumruhusu Yesu Kristo kutubadilisha kwa ndani sana, pale ambapo watu hawaoni jinsi tulivyo kweli kweli. Anaweza kufanya hivyo kama tukijinyenyekesha mbele Yake na tusipotafuta mapenzi yetu! Wengi wanadai wanamtumikia Mungu bali ukweli ni wanajitumikia wenyewe. Kama tunadai tunafanya kazi sana kwa ajili ya ufalme wa Mungu lakini ukweli ni kwamba tunaifuata njia ya kujipendeza, cheo, fahari au matekelezo ya makusidi yetu, ndipo na tuwe wazi juu ya hali ya mioyo yetu na kukiri makosa yetu makubwa na kutubu na toba ambayo itabadilisha mwelekeo wa maisha yetu na nia ya mioyo yetu. Wengi wanadhamini malengo na ndoto zao kuliko yote, wanazishika sana kana kwamba hawaiwezi kuziacha. Ingekuwa ‘kifo’ kwao kuziacha na kuyakumbatia mapenzi ya Mungu na msalaba wa Kristo Yesu. Lakini italeta uzima wa milele. Hakuna wengi walio tayari kupokea kifo cha tamani yao wawe kitu au kuwa na kitu kwa ajili ya kumfuata Yesu. Lakini kama tusipomruhusu Bwana kuutengeneza mioyo yetu wakati tulipo duniani, siku inakuja sawasawa na neno la Mungu,

“…kama mtu akijenga juu ya msingi huo (Yesu Krsito), dhahabu au fedha au mawe ya thamani, au miti au majani au manyasi, kazi ya kila mtu itakuwa dhahiri. Maana siku ile itaidhihirisha, kwa kuwa yafunuliwa katika moto; na ule moto wenyewe utaijaribu kazi ya kila mtu, ni ya namna gani. Kazi ya mtu aliyoijenga juu yake ikikaa, atapata thawabu. Kazi ya mtu ikiteketea, atapata hasara.” (1 Wakor.3:12-15).

Kwa hiyo na tujitoe kwa Bwana kwa sababu,

“BWANA hatazami katika vile vitu mwanadamu avitazamavyo. Mwanadamu hutazama katika sura ya nje, lakini BWANA hutazama moyoni.” (1 Samweli 16:7).

RUDI KWA MWANZO

15

ABIGAILI NA MAMBO YA NDOA.

Je, unafikiri mume au mke wako ni mgumu kuishi naye? Je, unamcha mungu kuliko kujipendeza mwenyewe? Abigaili hakuwa na kanisa. Abigaili hakuwa na Biblia. Abigaili hakuwa amebatizwa na Roho Mtakatifu. Lakini basi kinyume chake, Abigaili alikuwa na mume tu aliyekuwa hana adabu, tena mwovu, tena mkorofi, aliyeitwa Nabali.

Lakini Abigaili ALIMCHA Mungu. Na huyo mwanamke alikuwa mwenye akili njema, mzuri wa uso.

Katika 1 Samweli 25 tunasoma juu ya Nabali. Kondoo na mbuzi wa Nabali walikuwa na usalama wakati wote walipokaa chini ya ulinzi wa watumishi wa Daudi. Baadaye Daudi alipoomba Nabali awape watumishi wake msaada wa vyakula, Nabali akawatukana tu. Mara moja Daudi aliamua kumwua Nabali – lakini mtumishi mmoja wa Nabali aliweza kumwambia Abigaili mambo hayo. Alifanyaje Abigaili? Je, alifurahia tukio hilo? Je, aliwaza, “Hii sasa ni fursa yangu kwa Mungu ya kuniondoa toka kwa mume huyu! Sasa nitakuwa huru kutokana na mume huyu mkorofi! Bado mimi ni mrembo – kwa nini niolewe na mume kama huyu? Abigaili alifanyaje sasa ili awe huru kutokana na mume wake mwovu? Hakuna chochote! Yeye hakupaswa kusema wala kufanya lolote lile! Yeye angeweza kutulia TU pale na kumwacha Daudi aje pamoja na watu wake kumwua mumewe Nabali! Na wewe ungefanyaje?

Lakini Abigaili ALIMCHA Mungu! Hakujipendeza. Hakujitumikia. Alitaka kumpendeza Mungu na kumtumikia! Hakujifikiria yeye mwenyewe, au ajiokoe mwenyewe kutokana na hali hiyo ngumu. Hapana. Yeye alifikiria tu kumsaidia Daudi asilete hukumu juu yake kwa kujilipiza kisasi mwenyewe na kumwua mumewe. Alimwamini Mungu. Kwa hiyo alinyenyekea chini ya mikono ya Mungu na hakufikiri juu ya faraja yake mwenyewe au hali yake ngumu wala hakutafuta njia ya kutoroka kutoka katika mazingira yake ngumu. Na wewe? Aliamini kuwa kila kitu kilikuwa mikononi mwake Mungu, na kwamba iwapo mumewe inampasa kufa, basi huo ulikuwa ni wakati wake Mungu mwenyewe na wala sio kwa mkono wa mwanadamu. Hivyo Abigaili alifanyaje? Yeye aliandaa zawadi ya vyakula kwa ajili ya Daudi na hao watu wake Daudi alioandamana nao. Abigael akaondoka na kumfuatilia Daudi hukohuko njiani, “Ndipo hapo Abigaili alipomwona Daudi, … akainama mpaka nchi. Akamwangukia miguuni pake, akasema, Juu yangu, bwana wangu, JUU YANGU MIMI NA UWE UOVU; tafadhali mjakazi wako na anene masikioni mwako, nawe uyasikilize maneno ya mjakazi wako.”

Kumbe, Abigaili alikuwa yu radhi kuyatoa maisha yake kwa ajili ya mumewe mwovu! Kwa kuwa alimwamini Mungu, alitaka kumwokoa mumewe, na pia Daudi mwenyewe kutokana na hali ya kujilipiza kisasi. Abigaili hakujitafutia mlango au njia ya kutoka ili awe huru kutokana kwa mumewe mwovu. Na wewe? Aliamini kuwa kila kitu kilikuwa mikononi mwake Mungu. Ndoa yake ili kuwa mikononi mwa Mungu. Na alikataa kufanya cho chote kubadilisha hali hiyo ya maisha yake!

Je, mumeo au mkeo ni mtu mgumu sana hata unafikiri ungeshindwa kuendelea kuishi naye? Jaribu kufikiria hali ilikuwaje kwa mwanamke kuishi na mume kama Nabali!

Je, wewe ni mwamini? Je, unayo Biblia? Je, unakiamini kilichoandikwa ndani ya Biblia? Unampenda Mungu na unaamini kuwa yeye yuko pamoja nawe katika mazingira yoyote yale? Je, unatafuta kumpendeza yeye au kujipendeza wewe mwenyewe? Je, umepatwa na ubaridi au ugumu dhidi ya mumeo au mkeo kwa sababu unajisikia kuwa yeye ni mtu mgumu? Je, unamshughulikia kwa dharau na chuki? Yawezekana unataka kuniambia, “Lakini…” Lakini nini? Unataka kusemaje hapa? Unatakaje kujipa haki wewe mwenyewe – hapa hatuongelei juu ya dhambi kubwa, lakini ni kuhusu kile unachokifanya pale unapojisikia kuwa mumeo au mke wako ni mtu mgumu kwako. Je, unatafuta njia ya kuikwepa hali unayoipitia kuliko kuitafuta njia ya Mungu katika hali hiyo? Yesu ndiyo njia. Tabia yake ndiyo njia na uzima. Kama umeingiwa na ubaridi au umekuwa mgumu juu ya mumeo au mke wako, na ikiwa wewe ni mkristo, usimlaumu – sio mapenzi ya Mungu kwako uwe baridi au mgumu bali huo ni uchaguzi wako mwenyewe. Usimlaumu MTU yeyote. Utubu badala ya kuuachilia moyo wako uwe mgumu. Jinyenyekeze mwenyewe chini ya mkono wa Mungu wenye nguvu na upokee neema izidiyo – ambayo itakubadilisha WEWE  kwanza, na kisha umpende mumeo, mpende mkeo.

Abigaili hakuwa na Biblia isemayo kuwa, “mke ajinyenyekeze kwa mumewe”, wala hakuwa na Biblia inayosema, “waume wapendeni wake zenu”. Hakuwa na Biblia inayowaambia waumini wanaojikuta kwenye hali ngumu, , ‘Neema yangu YAKUTOSHA; maana uweza wangu hutimilika katika udhaifu.’ (2 Wakor. 12:9). Je, wewe unaamini mstari huu? Je utalipokea neno hili? Abigaili aliishi maisha ya namna hiyo. Je, wewe unaamini kuwa mume wako au mkeo ni mtu mgumu mno au ni mgumu kupita kiasi kwako? Lakini sikiliza neno la Mungu lisemavyo, “Lakini hutujalia sisi neema ILIYOZIDI; kwa hiyo husema, Mungu huwapinga wajikuzao, bali huwapa neema wanyenyekevu.” (Yakobo 4:6).

Ikiwa utapungukiwa na neema ya Mungu katika mahusiano yako, waweza kupata sababu toka katika mistari hii ya neno ka Mungu.

Waweza kujisomea vitabu vingi vihusuvyo ndoa, waweza pia kwenda kuhudhuria semina nyingi zihusuzo ndoa, lakini kama humwendei Mungu na kujinyenyekeza mwenyewe mbele zake kwanza, hakuna hata jambo moja kati ya hayo ufanyayo yatakayo kusaidia.

Daudi alimwambia Abigaeli, ‘ubarikiwe wewe’! Nawe pia utabarikiwa, na utafanyika kuwa baraka kwa wengine nyumbani mwako ikiwa unampenda Kristo na kumtumikia kuliko kujipendeza mwenyewe tu, ikiwa unamfuata Yeye na ‘kuipoteza nafisi yako’ kwa ajili Yake kuliko kujaribu kujiokoa maisha yako kwa kujaribu kuikimbia hali ngumu au kulalamika kuhusu hali hiyo, na kuwa mgumu na mwenye uchungu.

Kumfuata Kristo Yesu na kujikana mwenyewe kutayafanya “machungu” kuwa “matamu” katika maisha yetu. “Kujitwika msalaba wako” haimaanishi kubeba mzigo nzito! Inamaanisha kujikana mwenyewe na kumchagua Yesu na njia yake, na huku kunaleta MABADILIKO katika maisha yako. Kama neno la Mungu linavyosema, “Kwa maana huku ndiko kumpenda Mungu, kwamba tuzishike amri zake; wala amri zake si nzito”, na tena, “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha. Jitieni NIRA YANGU, mjifunze KWANGU; kwa kuwa mimi ni MPOLE na MNYENYEKEVU wa moyo; nanyi mtapata RAHA nafsini mwenu; kwa maana nira yangu ni LAINI, na mzigo wangu ni MWEPESI. (1 Yoh. 5:3; Mathayo 11:28-30).

Abigaeli hakujaribu kumbadilisha mumewe, alikabidhi uhai wake mikononi mwa Mungu na alikuwa anaridhia hukumu ya mumewe imwangukie yeye. Ikiwa Abigael angeweza kufanya hayo na kuwa kama hivyo nyakati za Agano la Kale, je, haitupasi sisi kuonyesha hata upendo mkuu na dhabihu katika mahusiano yetu sisi kwa sisi – sisi ambao tumeipokea neema na upendo wa Mungu kupitia Yesu Kristo ili kwamba uzima wake upate kudhihirishwa katika maisha yetu.

Inawezekana kabisa neno hilo siyo neno kwa wote, hata hivyo inawezekana ni neno kwa wengine.

Mungu alibariki neno lake kwa mioyo yetu.

©  David Stamen  2019  somabiblia.com

RUDI KWA MWANZO

16

TATIZO LENYEWE SIYO TATIZO KATIKA MAISHA YAKO YA KIROHO

TATIZO LENYEWE SIYO TATIZO KATIKA MAISHA YAKO YA KIROHO, BALI NAMNA YA KUSHUGHULIKIA HILI TATIZO NDIO LINAWEZA KUWA TATIZO KUBWA KWENYE MAISHA YAKO YA KIROHO.

Linapotokea jambo gumu au baya kwako, basi ugumu huo sio tatizo halisi, lakini NAMNA UNAVYOLITAZAMA hilo tatizo ndio linaweza kuwa tatizo halisi. Kwa mfano, anaweza kutokea mtu akakunenea uongo, lakini hilo linaweza kuwa SI TATIZO halisi kwako. Kama ukichukizwa, kama ukilikabili kwa uchungu au chuki au kisasi, HAPO SASA hili ndio tatizo HALISI katika maisha yako MBELE ZA MUNGU! Itaharibu maisha ya kiroho yako! Lakini ukimsamehe mapema – mara moja, bila kusita – basi kuna kuwa HAKUNA TATIZO LOLOTE! Badala yake, utakua kiroho tu! Mkumbuke Yusufu aliyesema,

“Nanyi kweli mlinikusudia mabaya, bali Mungu aliyakusudia kuwa mema.”

Mtazamo bora! Siyo tatizo kwamba ndilo tatizo, bali mtazamo wako kwenye hilo tatizo ndio tatizo. Yusufu alikuwa na mtazamo uliompendeza na kumtukuza Mungu! Yusufu alishi mbele za Mungu, kumpendeza Mungu na siyo kujipendeza mwenyewe kwa hisia ya kujihurumia, ya kuchukizwa, ya kulipa kisasi au kulalamika! Alimtegemea Mungu kabisa atamsaidia kwa wakati WAKE. Hakupa uchungu, hasira au kisasi nafasi yo yote viingie katika moyo wake! Hakulaumu mazingira yake.

Na wewe? Na mimi?

Je, unafikiri mazingira ya Yusufu yalikuwa ‘rahisi’ kwake? Hapana! Lakini hakuwalaumu watu wo wote. Hakuwalaumu ndugu zake; hakumlaumu mke wa Potifa; hakumlaumu Potifa mwenyewe. Hakuchukizwa na matendo yao dhidi yake! Hakulalamika wala kunung’unika wala hakujihurumia gerezani! HAKUJARIBU KUPIGANA NA MAZINGIRA YAKE kana kwamba hayo ndiyo ‘adui’ yake! Badala yake, alijikabidhi mikononi mwa Mungu tu! Alifanya kama ilivyoandika kwenye 1 Petro 4:19, “Basi wao wateswao kwa mapenzi ya Mungu NA WAMWEKEE AMANA ROHO ZAO.” Kama vile Daudi alivyosema, “Wakuu wameniudhi bure, Ila moyo wangu unayahofia maneno yako.” (Zaburi 119:161). Tena kwenye zaburi 119 tunasoma, “Nafsi yangu imo mkononi mwangu daima, LAKINI neno lako sikulisahau.”

“Nafsi yangu imo mkononi mwangu daima…”. Yaani, tunapokabiliwa na shida au tatizo, wewe na mimi tupo huru KUCHAGUA na kufanya lile limpendezalo Mungu au kujipendeza mwenyewe. NAMNA ya kushughulikia kila tatizo inabaki mikononi mwetu! Uchaguzi huo ni wetu! Na Mungu anaangalia tutakalofanya! Tutachagua nini? Tutachugua njia gani? Kinachompendeza Mungu ni nini? Na tusome ushuhuda wa Daudi aliyesema, “Mashahidi wa udhalimu wanasimama…Wananilipa MABAYA BADALA YA MEMA, Hata nafsi yangu ikaingia ukiwa. BALI MIMI, walipougua wao…nalijitesa nafsi yangu kwa kufunga…Nalijifanya kama kwamba NI RAFIKI AU NDUGU YANGU…Naliinama nikilia kama aliyefiwa na mamaye. Lakini nikijikwaa hufurahi na kukusanyana…” (Zaburi 35:11-15). Jambo la ajabu! Daudi alichagua kilicho bora, kilichompendeza Mungu!

Tunasoma juu ya KUSUDI LA MUNGU katika maisha ya Yusufu maneno yafuatayo:

“Walimwumiza miguu yake kwa pingu. Akatiwa katika minyororo ya chuma. Hata wakati wa kuwadia neno lake, NENO LA BWANA LILIMJARIBU.” (Zaburi 105:18,19). Kumbe! Unaona? Hapo gerezani lile lililomjaribu Yusufu lilikuwa neno la Bwana! Huo ndio mtazamo wa kiroho, mtazamo wa Biblia (the biblical or spiritual perspective)! MUNGU alikuwa anamjaribu Yusufu gerezani. Yusufu atafanya nini sasa? Je, atajaribu kufuata njia ya kurudisha mabaya kwa waliomuonea na kumkosea? Je, atatafuta kutengeneza njia yake mwenyewe kujiokoa kutoka katika hali hiyo ya mateso? Au atajiweke mikononi mwa Bwana na kumtegemea Yeye?

Katika uongozi wa Mungu, ‘adui’ hakuwa Potifa wala mke wake wala Farao. Mambo yote yaliyotokea katika maisha yake yalitokana na uongozi na mapenzi ya Mungu – AU Mungu alitumia nia ya wengine ili kutekeleza mapenzi yake NDANI ya moyo wa Yusufu KWANZA, na katika maisha na mazingira yake. Mungu apewe sifa; naye Mungu afanya hivyo kwa ajili ya utukufu wa jina lake lenyewe, mwanadamu asijisifu mwenyewe kana kwamba amefanya kitu! Na Mungu anafanya hivyo ili TUKUE KATIKA KUMJUA YEYE kwa ndani zaidi, ili UHUSIANO WETU NAYE UIMARISHE – na tufanane naye hapo duniani! Hali ya uhusiano wetu na Mungu ni ya thamani na muhimu zaidi SANA kuliko hali ya mazingira yetu! Kimsingi, Mungu anashughulikia hali ya moyo yako kuliko mazingira yako. Ya kwanza ni jambo la milele! Ya pili litapita hivi karibuni!

Na sisi tunatambua kwamba Yusufu hakupigana na mazingira yake ili kujiokoa mwenyewe. Hakupigana vita vyake mwenyewe. Hakutumia ‘mkono wa mwili’ kujiokoa kutoka katika mazingira na mateso yake! Hakutafuta kulipa kisasi. Alimngojea Mungu. Alimwamini Bwana. Yeye ‘hakusahau neno la Mungu’ kwake, kama tulivyosoma hapo juu! Aliishi kwa neno la Mungu tu.
Unakumbuka Yusufu alipojaribiwa na mke wa Potifa alale naye lakini alijibu,

“Nifanyeje ubaya huu mkubwa nikamkose Mungu?”

Na matokeo ya mwenendo huo nzuri? Alitupwa gerezani! Lakini Yusufu hakusahau neno la Bwana kwake. Alimngojea Mungu tu! Hakupigana na mazingira yake. Hakulalamika gerezani wala hakunung’nyika. Jambo la ajabu! Alijua Mungu ni juu yote! Aliishi kwa neno la Mungu lisemalo, ““Usiseme, Mimi nitalipa mabaya; Mngojee Bwana, naye atakuokoa.” (Mithali 20:22).

Hii ni imani ambayo pengine yaweza kuonekana haibadili mazingira yetu mara moja, au pengine haitabadilisha mazingira yetu kabisa, lakini hii ndiyo IMANI INAYOTUBADILISHA SISI WENYEWE katika mazingira yetu!

Je, ‘unapigana’ na mazingira yako; je, unatafuta njia yako mwenyewe ili kujiokoa kutoka katika mapito magumu; je, unamruhusu Shetani kukujaribu utengeneze ‘njia mkato’ kwa sababu unapungukiwa na imani ya kumtegemea Mungu na kumngojea ili akuokoe KWA NJIA YAKE na kwa WAKATI WAKE? Je, untafuta tafuta kwa nguvu yako KUTAWALA juu ya mazingira yako, au kuwatawala wengine ili mapito magumu unayoyapitia yaishie sasa hivi?! Kama ni hivyo, bila shaka unapungukiwa na AMANI na FURAHA kwelikweli kwani unatafuta kutengenza njia yako mwenyewe.

Ukiniuliza je, ni lazima nipokee kila jambo linalotokea kana kwamba linatokana na Mungu – najibu, kimsingi hiyo siyo msingi au mzigo wa ujumbe huo. Kwenye mafundisho hayo tunajifunza kumtegemea Mungu haijalishi yanayotokea au yasiyotokea; tunajifunza badala ya kutengeneza njia yetu wenyewe kujiokoa sawasawa na mapendeleo yetu, kujitoa wenyewe kwake Mungu, kujinyenyekeza kwake, kujiweka mikononi mwake na kumtegemea kwa mioyo yetu yote – na katika hali hiyo kujilinda mioyo yetu katika upendo wa Mungu na neema ya Mungu! Tunajifunza kutoka katika maandiko hayo namna ya kushughulikia na mapito magumu na kutengeneza mtazamo wa namna gani watu wanapotukosea. Petro anatushauri kwa ukweli huu juu ya Yesu, “Yeye alipotukanwa, HAKURUDISHA matukano; alipoteswa, hakuogofya; bali ALIJIKABIDHI KWAKE YEYE ahukumuye kwa haki.” (1 Petro 2:23). Hapo tunafundishwa kutokurudisha mabaya wala kufikiri mawazo mabaya watu wanapotukosea.

UNARUDISHA nini moyoni mwako au kwa matendo watu wanapokukosea au kukuonea vibaya? Mtu akikupiga shavu la kuume, utafanyaje? Utarudisha nini kwake? Utachugua nini? Neno la Mungu linatufudisha,
“Mtu awaye yote asimlipe mwenziwe mabaya kwa mabaya.” (1 Wathes.5:15).

Sisi lazima tuwe “watu wasiolipa baya kwa baya, au laumu kwa laumu; bali wenye kubariki; kwa sababu hayo ndiyo mliyoitiwa ili mrithi baraka.” (1 Petro 3:9).
Kinachopendeza Mungu ni nini? Tunasoma,

“Maana huu ndio WEMA HASA, mtu akivumilia huzuni kwa kumkumbuka Mungu, pale ateswapo ISIVYO HAKI. Kwa maana ni sifa gani kustahimili, mtendapo dhambi na kupigwa makofi? Lakini kustahimili, mtendapo mema na kupata mateso, HUU NDIO WEMA HASA mbele za Mungu. Kwa sababu ndio mlioitiwa…” (1 Petro 3:19-21).

Hiyo ndiyo mtazamo wa kiroho. Hiyo ndiyo vigezo vya Mungu.

Tatizo lenyewe siyo tatizo katika maisha yako, bali namna ya kushughulikia hili tatizo au namna unavyolitazama hilo tatizo ndio linaweza kuwa tatizo halisi!

RUDI KWA MWANZO

17

‘MAMBO YOTE HAYA YAKO KINYUME NAMI.’ BALAA AU BARAKA?

Kibinadamu tungeweza kusema kuwa mambo mabaya yamemtokea Yakobo. Alimpoteza mtoto wake mmoja. Na tena akatokewa na ukame wa kutisha. Kisha mwanae mwingine akawa amechukuliwa utumwani. Ndipo alipofikiria kuwa anaweza kuwapoteza wanaawe wote iwapo atawapeleka Misri tena, na kwa huzuni alipiga kelele..

“Yakobo baba yao akawaambia, ‘Mmeniondolea watoto wangu! Yusuphu hayuko, wala Simioni hayuko, na Benjamini mnataka kumchukua nae. MAMBO HAYA YOTE YAMENIPATA MIMI. (Mwanzo 42:36)
‘Mambo yote haya yako kinyume nami.’ Hiyo ilikuwa maana ya maneno yake, na hivyo Biblia ya KJV (Kiingereza) inavyotafsiri mstari huo. Je umewahi kujiliwa namna hii? Ukweli ni kwamba MUNGU MWENYEWE NDIYE ALIYE KUWEMO KATIKA MAZINGIRA HAYO YOTE YA YAKOBO. Mungu alikuwa kazini ilikuletea baraka kubwa Yakobo, pamoja na familia yake yote. Kile ambacho Yakobo alikuwa anakiona kama ni adui, kama ni tishio, kama ni hatari kwake, kumbe ilikuwa ni uhalisia wa mkono wa Mungu mwenyewe katika kumwongoza kuelekea kwenye BARAKA KUBWA. Wakristo wengine wanapoingia katika matatizo huanza kwa urahisi tu kumlaumu shetani, au pale mambo yanapokuwa hayafanyiki kama wanavyopenda yawe. Wanavurugikiwa badala ya kujitoa maisha yao kama dhabihu iliyo hai kwake Mungu katika mazingira yao ili kwamba ipate kuthibitisha kile kilicho chema, chenye kukubalika na mapenzi makamilifu ya Mungu katika maisha yao (Warumi 12:2).

Paulo alitangaza ukweli huo, “…Kristo yu hai ndani yangu, na uhai nilio nao sasa katika mwili ninao katika imani ya mwana wa Mungu,ambaye alinipenda akajitoa nafsi yake kwa ajili yangu.(Wagalatia 2:20)
Paulo aliishi kwa imani. Kwa imani ya namna gani? Kwa imani katika mwana wa Mungu? Ndiyo, lakini ni zaidi ya hiyo; aliishi siku kwa siku akiamini katika mambo yote kwamba Yesu Kristo alimpenda na akajitoa yeye mwenyewe kwa ajili yake, pasipo kujali chochote kinachoweza kutokea! Hii ni imani ambayo pengine yaweza kuonekana haibadili mazingira yetu mara moja, au pengine haitabadilisha mazingira yetu kabisa, lakini hii ndiyo IMANI INAYOTUBADILISHA SISI WENYEWE katika mazingira yetu! Ni imani inayoushinda ulimwengu. Ni imani inayotufanya sisi kuvumilia katika majaribu na matatizo na hutuleta katika ufahamu halisi kuona kuwa Kristo anaishi ndani yetu, na huyafanya mambo yote yafanye kazi kwa uzuri! Ni imani ambayo hutubadilisha sisi na kumtukuza Mungu. Ni imani inayompendeza Mungu!

Sasa inakuwaje basi baadhi ya waamini wanafikiri mara moja kuwa Mungu hapendezwi nao kwa sababu tu eti mambo yao wakati mwingine hayaendi sawa au kwa sababu wanakutana na shida? Hiyo siyo imani. Hizo ni imani za kishirikina. Bila sababu yoyote tunafikiri kuwa majeshi ya giza fulani yapo kinyume nasi na kwamba yanataka kutuadhibu.Tunapokuwa tunafanya aina hii ya hofu na mitazamo ya hasi, tunakuwa hatumheshimu Mungu.
Paulo alivunjikiwa na jahazi mara tatu. Je hii inamanisha kuwa Mungu alikuwa kinyume naye? Je Mungu alikuwa anamwadhibu? Bibilia iko wazi kwamba jibu lake ni ‘Hapana’. Paulo anasema,
“…twajua yakuwa kaika mambo yote Mungu hufanya kazi pamoja na wale wampendao katika kuwapatia mema yaani wale walioitwa kwa kusudi lake..”(Warumi 8:28)

Kwa hiyo Paulo aliweza kusema, “Najua kudhiliwa, tena najua kufanikiwa; katika hali yo yote, na katika mambo yo yote, nimefundishwa kushiba na kuona njaa, kuwa na vingi na kupungukiwa. Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu.” (Wafilipi 4:12,13)

Paulo alikutana na matatizo pamoja na majaribu mengi lakini ushuhuda wake na mafundisho yake ni kuwa TUNAJUA kuwa mambo yote hufanya kazi pamoja kwa wema kwa wao wampendao Mungu! Hii ni yenye nguvu. Hii huingia moja kwa moja kwenye mizizi ya mahusiano yetu pamoja na Mungu. Je, kumtumaini Mungu kwetu kuna zama ndani zaidi kuliko yale yanayotutokea au yasiyotutokea? Je, imani ni kumwamini Mungu katika kufanya mambo tu? Ni zaidi ya hapo. Kujaribiwa kwa imani yetu ni kitu cha thamani kuliko hata dhahabu (1 Petro 1:7). Imani ni kumwamini Mungu pale ambapo hakuna chochote kinachotokea, au mambo yanapoonekena kutuendea vibaya. Hii ndiyo imani ya kweli, inaingia ndani zaidi kuliko mazingira ya aina yoyote. Tunashawishika kikamilifu kuhusiana na wema Wake na umaminifu KULIKO MAZINGIRA YOYOTE yanayotufanya tutie shaka pendo lake kwaajili yetu. Hii ndiyo imani. Matokeo ya imani hiyo hiyo katika maisha yako na yangu ni amani kubwa sana na ushupavu mioyoni mwetu wakati tunapokutwa na shida au balaa. Wasikilize watu hawa watutu toka katika Agano la Kale.

“Kama ni hivyo, Mungu wetu tunayemtumikia anaweza kutuokoa na tanuru ile iwakayo moto, naye atatuokoa na mkono wako ee mfalme. BASI KAMA SI HIVYO, ujue ee mfalme, SISI HATUTAKUBALI KUITUMIKIA MIUUNGU YAKO wala kuisujudia hiyo sanamu ya dhahabu uliyoisimamisha, (Danieli 3:17-18).

Ni mistari ya ajabu namna gani hii! Ndiyo tunajua kuwa Mungu aweza kutuokoa sisi kutoka katika moto huu uwakao, wanasema. LAKINI HATA KAMA HATAFANYA HIVYO, haitabadilisha lolote! Tutaendelea kumwabudu Yeye BILA KUJALI KITAKACHOTOKEA. Baadhi ya wakristo wanaanza kumtiliashaka Mungu na pendo lake eti kwa kuwa tu haonyeshi kuingilia mazingira yao. “Yeye ni mwenye nguvu zote, kwa nini hafanyi lolote? Je, ni kweli anatupenda?” Haya ni aina ya mawazo yanayozalishwa na kutokuamini, na yanaungwa mkono na shetaani. Meshak, Shadraki na Abdinego wao hawakusita, wala hawakukaribisha mawazo kama hayo, pasipokujali kilichowatokea wao waliendelea kumwabudu Mungu. Hii haiwezi kutengenezwa au kuiga! Imani hii inatoka ndani kabisa ya moyo wa mtu. Inatokana na kuendelevu wa kumjitoa na kumpenda mwokozi wetu kila siku, kwa ajili ya utukufu wa Mungu! Ndiyo sababu Paulo anasema,

“Wala si hivyo tu, ila na tufurahi katika dhiki pia, tukijua yakuwa dhiki, kazi yake ni kuleta saburi, na kazi ya saburi ni uthabiti wa moyo, na kazi ya uthabiti wa moyo ni tumaini, na tumaini halitaharishi, kwa maana PENDO LA MUNGU LIMEKWISHA KUMIMINWA NDANI YETU na Roho Mtakatifu tuliye pewa sisi.” (Warumi 5:3-5).

Ni ule uzoefu wa kupita katika matatizo ndio unaotufundisha sisi kuweka mategemeo yetu tumaini letu katika Mungu, na hii hutusababishia sisi kumjua kwa undani zaidi kuwa yeye ni Mwaminifu, Mwema na wakutegemewa! Ni imani hiyo iliyotokana na majaribu hayo, hiyo ni yenye thamani zaidi kuliko dhahabu. Imani hii inamtukuza Mungu na haitoi nafasi kwa shetani.

Ayubu alipokutwa na balaa, je, alimpima au kumhukumu Mungu au upendo wake sawasawa na mambo yale yaliyompata? Hapana. Katika kupoteza mali yake yote na watoto wake wote, alimwabudu na kumtukuza Mungu tu! Tunasoma maneno yafuatayo, “Ndipo Ayubu akainuka…na kuanguka chini, na KUSUJUDIA…akasema, Bwana alitoa, na Bwana ametwaa; jina la Bwana na libarikiwe.” (Ayubu 1:20,21). Imani hiyo ni ya thamani sana”. Hiyo siyo jambo la ‘kuamini kitu’ tu, bali inatuonyesha kwa wazi ule UHUSIANO Ayubu alio nao na Mungu! Alimwamini Mungu pasipo kujali mazingira; aliamini na kutegemea Uaminifu wa Mungu; hakulaumu tabia ya Mungu, badala yake aliitukuza tabia ya Mungu. Hiyo haitokei kwa ghafla! Sisi tumeitwa tumwamini na kumpenda Mungu kila siku, haijalishi mambo yanayotokea au yasiyotokea – kuishi bila kuona shaka juu ya pendo lake kwako; bila kufikiri Mungu ni kinyume nawe. Badala yake kuwa na hakika juu ya Uaminifu wa Mungu na juu ya tabia Yake.

Mungu aliwaahidi Waisraeli kuwapatia nchi inayo miminika maziwa na asali, na watu wa Mungu walikusudia kufurahia huku wakimwona Mungu akiwafanyia mambo kwa niaba yao, kwa kuwafungulia njia katika bahari ya shamu na kuwashindia dhidi ya Wamisri. Lakini mara tu shida ilipowajia waliangukia katika kutokuamini, na sio tu walimlaumu Musa, bali walimlaumu Mungu mwenyewe kwa kusimama kinyume nao. Wao walimshtaki Mungu hata kusema kuwa Mungu aliwachukia wao na kwamba amewaleta hadi jangwani ili kuwaangamiza humo! (Kumb.1:27) Hapo ndipo kutokuamini kwaweza kutuleta sisi kama tutairuhusu! Je kukoje moyoni mwako?
Kwa sababu ya kutokuamini kwao Waisraeli wengi hawakuweza kuingia katika nchi ile ya ahadi. Walimpima Mungu kwa kujilinganisha na mazingira yao kwa nje. Lakini Mungu amekwisha kuridhia pendo lake kwa ajili yetu, na amelionyesha pendo lake kwa kutukomboa kutoka katika nguvu za adui! Hatupaswi kumpima Mungu kwa mazingira ya nje. Tunapaswa kumtegemea yeye kwa sababu ya kile ambacho amekwisha kukifanya kwa ajili yetu. Na kwa sababu yeye ni Mungu. Mazingira yetu yanayobadilikabadilika, hayambadilishi Yeye! Wala imani yetu katika yeye isibadilike kwa sababu tu eti mazingira yetu ni magumu.

Kama unataka kumpima Mungu kwa kuangalia mazingira yako kwa nje, basi mpime yeye kwa mazingira haya – PALE CALVARI! Kama unataka kufahamu jinsi Mungu anavyojisikia kukuhusu wewe, tazama pale MSALABANI. Mungu alitoa kitu cha thamani zaidi ambacho angeweza kutoa kwa ajili yako – alimtoa mwanae pekee. Alitupenda sisi zaidi hata akamtoa mwanae pekee Yesu Kristo afe pale Calvari!

“Bali Mungu aonyesha pendo lake yeye mwenyewe kwetu sisi, kwa kuwa Kristo alikufa kwa ajili yetu, tulipokuwa tungali wenye dhambi” (Warumi 5:8).

Haya ndiyo mazingira yanayoonyesha pendo la Mungu kwa ajili yetu. Ni tukio kubwa zaidi ambalo halijawahi kutokea! Umpime Mungu kwa mazingira hili, yaani ya msalaba, na mazingira mengine yote yawayo katika maisha yako utayaona na macho mapya! Kwa hiyo Paulo anaenda mbali zaidi katika kusema kuwa…

“Kwa maana nayahesabu mateso ya wakati huu wa sasa kuwa si kitu, kama utukufu ule utaofunuliwa kwetu”(Warumi 8:18)

Kila siku maisha yetu yanapaswa kuwa ni dhabihu iliyo hai ya upendo, kutafakari, utii, sifa na kumtegemea Mungu kikamilifu yeye aliyetupenda na ambaye huyafanya mambo yote yafanye kazi kwa wema. Paulo aliishi namna hiyo na hata alidiriki kusema…

“Basi tuseme nini juu ya hayo? Mungu akiwapo upande wetu ni nani aliye juu yetu? (Soma Warumi 8:31-37)

Uitazame msalaba ukaone kuwa Mungu ni kwa ajili yako, yupo kazini ka ajili ya kila mazingira, ILI KUKUFANANISHA WEWE NA MIMI KWA SURA YA MWANAE. Hili ni jambo lenye utukufu; hili ni jambo jema lile alilofanya Mungu ndani yetu, yaani, tufananishwe na mfano wa Mwana Wake! Hicho ndicho kinachosemwa katika Warumi 8:29 ambao unafuatia baada ya ule mstari wa 28. Yawezekana unajiuliza, ni jambo gani jema laweza kutoka katika mazingira yenye shida? Jibu la Biblia ni, ‘Yesu Kristo.’ Yesu Kristo ndani yako tumaini lenye utukufu!

Usifikiri kuwa Mungu yu kinyume nawe. Jikabidhi kwake, ujitoe kwake, pasipo masharti. Yeye anakupenda, na kama ilivyo kuwa kwa Yakobo, ni vilevile kwako wewe. Ataendelea kufanya kazi katika maisha yako ili kukuletea baraka timilifu katika Kristo Yesu. Mungu hayupo pale ili kutimiza matarajio na ndoto zetu za binafsi, au hata mipango yetu. (Utatambua na kujua mapenzi YAKE kwa ajili ya maisha yako ikiwa unafuata agizo la neno la Mungu katika Warumin 12:1,2). Yeye hufanya kazi ili kutubariki katika Kristo Yesu. Kwa vyovyote shetani yupo kazini, na hufanya mambo kujaribu kuangamiza kazi za Mungu, na kuwanyanganya watu wa Mungu ule urithi wao ulimo katika Kristo Yesu. Lakini wewe utaweza tu kuelewa nini ni nini katika maisha yako, na katika mazingira yako pale tu utakapojitoa maisha yako kama dhabihu iliyo hai kikamilifu na pasipo malalamiko au masharti kwa Mungu kila siku! Vinginevyo unaweza kujikuta wewe mwenyewew ukipambana kinyume na Mungu, huku ukifikiria labda ni shetani katika mazingira yako, kama vile ilivyo kuwa kwa Yakobo.
Yusufu mwana wa Yakobo alipitia katika kuushuhudia uovu mwingi kinyume naye, na mazingira ambayo kwa uhakika yalikuwa magumu na yasiyo ya haki – alichukiwa na hatimaye akauzwa utumwani na ndugu zake yeye mwenyewe, alisingizwa na mke wa bosi wake, pasipo haki akatupwa gerezani, lakini mwisho wa hayo yote, yeye alisema nini?

“nanyi kweli mlikusudia mabaya, bali Mungu aliyakusudia kuwa mema, ili itokee kuokoa taifa kubwa kama ilivyo leo.” (Mwanzo 50:20).

Ni maneno ya ajabu ya jinsi gani! Hakuna uchungu. Hakuna malalamiko. Yusufu aligundua mkono wa Mungu katika mazingira yake yote. Na wewe? Sio mambo yote yaliyomtokea Yusufu yakuwa sawa; mambo yasiyo kweli yalimtokea Yusufu. Alipitia katika mambo ya mateso, alivumilia na kuwa mnyenyekevu, lakini alikabidhi maisha yake na roho yake kwa Mungu katika mambo yote na akamwabudu Mungu. Hakupambana au kufanyia ushawishi katika mazingira yake ili kupata kile alichotaka apate. Mungu alifanya kazi kwa niaba yake ili kumletea utimilifu wa baraka.

Basi na Mungu afanye hivyo katika maisha yetu yote.

RUDI KWA MWANZO

18

“BASI TORATI, KWA KUWA NI KIVULI cha mema yatakayokuwa, wala si sura yenyewe ya mambo hayo…” (Waebr.10:1).

Unaweza kuandaa meza nje ya nyumba yako na ukaandaa juu yake vyakula vizuri kama nini! Jua linawaka na huleta kivuli cha meza ile pamoja na chakula, kinaonekana ardhini. Sasa unaweza kujaribu kukila kile kivuli cha meza na vyakula vyake ambavyo vinaonekana pale ardhini chini ya ile meza HALISIA YENYE VYAKULA! Kitatokea nini!? Ukijaribu kumega tonge lako kwenye kile kivuli, mkono wako hautaambulia kitu, au utaishia kumega tonge la mchanga tu kwenye mkono wako! Je, unaweza kuishi kwa jinsi ya namna hii? Utawaita rafiki zako pamoja na majirani na kuwaambia, “Karibuni tule kivuli cha chakula hiki kizuri sana!” Kwa vyovyote hutafanya hivyo kwa maana utakufa! Ikiwa utajaribu kuishi kutokana na kivuli cha chakula, UTAKUFA. Tendo la kula vivuli vya vitu halisia, haitakuweka hai! Lakini sasa hivyo ndivyo vilevile wanavyofanya wahubiri hawa wanapotutaka tufuate mifumo ya majukumu ya nje ya kidini tu – kwa mfano, kuziweka wakfu shamba au nyumba; kuufuata mfumo wa dini wa kuondoa ‘laana’ katika ardgi, shamba, duka au nyumba. Wanayaua maisha ya kiroho ya wale wanaowahubiria. Mambo ya nje/kimwili ya Agano la Kale yalikuwa ni KIVULI tu kinachoonyesha UHALISIA na NGUVU ya kiroho ambayo Kristo angetupatia kutokana na kifo chake na ufufuo wake!

Yesu ametuondoa kutoka kwenye kivuli na sasa ametuingiza kwenye uhalisia, uhalisia wa maisha yake mwenyewe yaliyomo ndani yetu.

Mambo mengi ambayo Mungu aliwaagiza Waisrael wayafanye yalikuwa ni kiwasilisho cha Kristo na kile ambacho anakuja kutufanyia – ilikuwa ni KIVULI na kiini cha kweli cha nguvu ya maisha halisia ya kiroho ambayo Kristo yalikuwa anaenda kutuletea kupitia wokovu wake. Kristo yeye mwenyewe ni chakula chetu – ile mana ambayo Waisrael waliila, na yale maji waliyokunywa yaliyotoka kwenye mwamba kule jangwani – na hiyo nayo yote ilimwakilisha Yesu. (1Wakor.10:1-4). Kwa nini wengi sasa wanataka warudi nyuma kula vivuli, au mavumbi ya ardhini? Kwa nini basi mtu ahubiri kivuli wakati kile kitu halisia kinapopatikana?

Injili aliyoihubiri Paulo ilimwinua Kristo na kazi ya msalaba, siyo mambo ya mfumo wa nje!

Mtu mmoja aliuliza kama ninalikataa Agano la Kale! Ni swali la mshangao mkubwa sana hilo! Je, Paulo mtume naye alilikataa Agano la Kale kwa sababu tu yeye aliyaandika mambo haya kwenye waraka wa Wagalatia? Lakini ebu ngoja nikuulize, je, unaamini kwamba unahitajika kutahiriwa ili uwe Mkristo wa kweli? Kama huamini hivyo, KWA NINI basi huamini? Je, unaleta ng’ombe au mbuzi au kondoo kanisani siku za jumapili, au mara moja kila mwaka ili kuwachinja kwa ajli ya msamaha wa dhambi zako? Kama hufanyi hivyo, KWA NINI basi hufanyi? Je, unaishika siku ya sabato kama vile wayahudi wanavyofanya? Kama hufanyi hivyo, KWA NINI basi huyafanyi hayo? Na kama huyafanyi mambo kama hayo, huyafanyi kwa sababu wewe unalikataa Agano Jipya? Kwa vyovyote hulikatai Agano la Kale, lakini kinyume chake, sisi hatufanyi hayo kwa sababu TUNAIAMINI Biblia. Biblia NZIMA, kwamba ni neno la Mungu. Hatuyafanyi mambo hayo kwa sababu Yesu Kristo alikufa pale Kalvari kutuokoa kutokana na dhambi zetu na kutukomboa kutoka kwenye laana ya sheria!

Je,mtume Paulo anasemaje kuhusu watu wale wanaotaka kuturududisha nyuma kwenye kufuata sheria na taratibu za kidini na kuishi kivulini?

“Nastaajabu kwa kuwa mnamwacha upesi hivi yeye aliyewaita katika neema ya Kristo, na kugeukia injili ya namna nyingine wala si nyingine, lakini wapo watu wawatabishao na kutaka kuigeuza Injili ya Kristo. Lakini ijapokuwa sisi au malaika wa mbinguni atawahubiri ninyi injili yoyote isipokuwa hii tuliyowahubiri, na alaaniwe, kama tulivyotangulia kusema, na sasa, nasema tena, mtu awaye yote akiwahubiri ninyi injili yoyote isipokuwa hiyo mliyoipokea, na alaaniwe!” (Waalatia 1:6-8).

Hii ni lugha nzito sana! Anawaambia kwamba wale wafundishao mambo haya wanawasumbua tu, na kuizuia Injili ya Kristo! Kuanza kutii na kuyafuata mambo ya kiinje ya sheria za Musa ilikuwa ni kuwaondoa watu mbali na neema ya Kristo na kuwaingiza kwenye dini zao wao wenyewe – ambazo Paulo anaziita “injili nyingine”. Na kama utasoma vizuri ule mstari wa 8, utaweza kukubaliana nami kuwa hakuna hata mmoja ambaye angependa kuishi chini ya hukumu ya mstari ule! Kosa la fundisho hili ni hatari kiasi kwamba haliwezi kuwa hatari zaidi! ……………….

Hiyo ni sehemu tu ya somo liitwalo JUU YA MFUMO WA KUIWEKA WAKFU KWA BWANA ARDHI AU NYUMBA YAKO. Unaweza kusoma somo zima kupitia link ifuatayo:

https://somabiblia.com/juu-ya-mfumo-wa-kuiweka-wakfu-ardhi-au-nyumba-yako/

RUDI KWA MWANZO

19

JE, NAWEZA KUJUA MAPENZI YA MUNGU KWA MAISHA YANGU?

Tunaweza kumshukuru Mung kwani Yeye hajaficha mapenzi Yake juu yetu! Paulo anasema,

“Maana haya ndiyo mapenzi ya Mungu, KUTAKASWA KWENU, mwepukane na uasherati.” (1 Wathes.4:3).

Je, unataka kufanikiwa, unapenda kutimiza ndoto yako au lengo lako? Lakini haya yote hayana maana, ni bure tu kama ukianguka kwenye dhambi ya uzinzi, au dhambi nyingine ya siri? Siku hizi, wengi wanajitahidi sana wafanikiwe. Je, unajitahidi kufanakiwa katika kutakaswa kwako? Je, inawezekana wengi hawajajali mapenzi ya Mungu ya dhati katika maisha yao siku hizi ili waweze kuifuate ndoto zao tu, wakidai ‘ndoto’ zao ni ‘mapenzi ya Mungu’? Mambo mengine yote katika maisha yetu ni BURE tu kama tukifuata anasa ya mwili, kuona mambo machafu kwenye mtandao au kujiunga na facebook group ya picha za ngono.Haya ndiyo mapenzi ya Mungu, KUTAKASWA KWENU, kuishi maisha ya UTAKATIFU kwa MOYO SAFI!

Tuendeleeni! Paulo anafundisha kwamba, “FURAHINI siku zote; OMBENI bila kukoma; SHUKURUNI kwa kila jambo; maana HAYO NI MAPENZI YA MUNGU kwenu katika Kristo Yesu.” (1 Wathes.5:18).
Mapenzi ya Mungu kwa maisha yangu ni nini? Hayo ni mapenzi ya mungu kwangu! Tunaweza kumshukuru Mungu sana kwani alidhihirisha mapenzi yake kwa ajili ya masiha yetu kwa wazi! Kabla ya mambo mengine yote, Mungu amedhihirisha mapenzi yake juu maisha yangu na maisha yako ni tufurahi siku zote, tuombe bila kukoma na kumshukuru katika kila jambo! Kwa hiyo, usizunguke zunguke, usitafute tafute ukijiuliza ‘mapenzi ya Mungu katika maisha yangu ni nini?’, ila ‘pokea kwa upole neno lile lililopandwa ndani, liwezalo kuziokoa roho yako’. (Yakobo 1:21).

Je, naweza kujua MWITO wa Mungu kwa maisha yangu? Ndiyo, naweza! Paulo anatujulisha kwamba, “Mungu…alituokoa akatuita kwa MWITO MTAKATIFU si kwa kadiri ya matendo yetu sisi, bali kwa kadiri ya makusudi yake yeye na neema yake.” (2 Tim.1:9). Na Petro anathibitisha ukweli huo, “…kama yeye aliyewaita alivyo mtakatifu, ninyi nanyi IWENI WATAKATIFU KATIKA MWENENDO WENU WOTE…” (1 Petro 1:15).

Paulo anatusihi, “mwenende kama inavyoustahili WITO WENU MLIOITIWA; kwa UNYENYEKEVU wote na UPOLE, kwa UVUMILIVU, mkichukuliana katika UPENDO;” (Waefeso 4:1,2)! Siku hizi wengi wanatafuta waitalo ‘kusudi’ la maisha yao wakati hawajali MWITO WA MUNGU ambao tayari ameshaudhihirisha kwetu kupitia neno lake! Je, tunafurahia zaidi kufuata ‘kusudi letu’ na kutimiza ‘ndoto yetu’ kuliko kufuata na kuishi sawasawa na neno la Mungu na kutumiza mwito wetu unaotokana moja kwa moja na Mungu?

Katika Waebrania tunaambiwa jambo la ajabu juu ya mwito wetu, “Kwa hiyo, ndugu watakatifu, wenye kuushiriki MWITO WA MBINGUNI, mtafakarini sana…Yesu.” (3:1). Hii ni neema kubwa sana kwetu; tumeitwa na mwito wa mbinguni, tuwe kama Yesu Kristo ulimwenguni humu! Sawasawa na mafundisho ya Yohana, “…kama Yeye alivyo, ndivyo tulivyo na sisi ulimwenguni humu.” (1 Yoh.4:17). Na Paulo anaeleza ukweli mkuu sana, “Kwa maana sisi tu MANUKATO YA KRISTO, mbele za MUNGU, katika wao wanaookolewa, na katika wao wanaopotea; katika hao wa pili harufu ya mauti iletayo mauti; katika hao wa kwanza harufu ya uzima iletayo uzima.” (2 Wakor.2:15,16). Huo ndio mwito mkuu, siyo ndiyo? Je, tunautafuta mwito kuu kuliko huo? Kama ni hivyo, labda Mungu ataongea nasi kama vile alivyoongea na Baruku aliposema, “Je! Unajitafutia mambo makuu? Usiyatafute!” (Jer.45:5).

Sisi tumeitwa tuwe HARUFU YA KRISTO mbele za Mungu KWANZA na KWA KIMSINGI. Tunaishi mbele ya Mungu kwanza, siyo mbele ya watu. Bila kuwa harufu ya Kristo MBELE YA MUNGU, hatuwezi kuwa baraka kweli kweli kwao wengine! Kama ilivyoandikwa katika Kitabu cha Kutoka sura ya 29, Mungu aliwaagiza makuhani watoe, “wana-kondoo wa mwaka mmoja wawili SIKU BAADA YA SIKU DAIMA. Mwana-kondoo mmoja utamchinja asubuhi; na mwana-kondoo wa pili utamchinja jioni …IWE HARUFU NZURI,… Itakuwa ni sadaka ya kuteketezwa MILELE…MBELE YA BWANA. HAPO NITAKAPOKUTANA NANYI, ili ninene na wewe HAPO.” (29:38-42). Kumbe, Mungu Baba yetu anakutana nasi mahali pa madhabahu ya dhabihu naye anatazamia tutoe maisha yetu yawe harufu ya Yesu Kristo mbele Yake, ‘asubuhi na jioni’, yaani, wakati wote! Yesu Kristo ni Mwana-Kondoo wa Mungu! Na mahali pale pale pa sadaka anatutakasa ili tumtimikie tulipo. (“…nitaitakasa…hiyo madhabahu; pia Haruni na wanawe NITAWATAKASA, ILI WANITUMIKIE katika kazi ya ukuhani.” 29:44). Jambo la ajabu! Kwa hiyo Paulo anasema, “Basi, ndugu zangu, nawasihi, kwa huruma zake Mungu, ITOENI MIILI YENU IWE DHABIHU ILIYO HAI, TAKATIFU, YA KUMPENDEZA Mungu, ndiyo ibada yenu yenye maana. Wala msiifuatishe namna ya dunia hii; bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia zenu, MPATE KUJUA HAKIKA MAPENZI YA MUNGU aliyo mema, ya kumpendeza, na ukamilifu.” (War.12:1,2).

Basi, usijisumbue kwa ajili ya mapenzi ya Mungu mawazoni mwako. Kwa kimsingi sasa unaijua njia. Njia ni Yesu Kristo. Fanya kama Paulo alivyofanya; uwe na fikra ya Paulo aliyesema,

“Ndugu, sijidhanii nafsi yangu kwamba nimekwisha kushika; ila NATENDA NENO MOJA TU; nikiyasahau yaliyo nyuma, nikiyachuchumilia yaliyo mbele; NAKAZA MWENDO, NIIFIKILIE mede ya THAWABU YA MWITO MKUU wa Mungu katika Kristo Yesu. Basi…na tuwaze hayo.” (Wafilipi3:13,14). Lile usilolijua, subiri tu mbele Yake, na kwa wakati wake utalijua. Yatoe maisha yako yawe dhabihu iliyo hai, yawe harufu ya Kristo mbele Yake kila siku, bila kuitafuta njia yako mwenyewe, na neno la Mungu linatuambia utapata kujua hakika mapenzi ya Mungu, hatua kwa hatua na kwa wakati wake! Na kumbuka Paulo alilosema katika mstari unaofuata, yaani, “Kwa maana kwa neema niliyopewa namwambia kila mtu aliyeko kwenu ASINIE MAKUU KUPITA ILIVYOMPASA KUNAI.” Mungu akubariki!

RUDI KWA MWANZO

20

KUSHINDA HILA YA SHETANI

Hila na mbinu za Shetani na jinsi ya kuzishinda. Vita vya Kiroho kweli kweli.

Mungu amesema, “Mimi ndimi BWANA Mungu wako aliyekutoa Misri, kutoka nchi ya utumwa. Usiwe na miungu mingine ila mimi. Usijifanyie sanamu ya kuchonga katika umbo la kitu cho chote kilicho juu mbinguni au duniani chini au ndani ya maji.” (Kutoka 20:2-4).

Hila ya Shetani ndiyo kupotosha tabia ya Mungu mawazoni mwetu; mbinu za Shetani ndiyo kuharibu sura ya kweli ya Mungu mioyoni mwetu ili tusiamini Mungu, ili tusiamini wema, neema na rehema zake, ili tusiamini Yesu anaweza kutuokoa kabisa! Shetani anajaribu kutushawishi kwamba Mungu ni dhidi yetu (na hata kwamba watu wengine ni dhidi yetu!), kwamba Mungu ametuacha au hata Mungu anatuadhibu kwa ajili ya jambo fulani. Kusudi la Shetani ni tusitambue jinsi Mungu alivyo kweli kweli!

Mwanzoni Shetani alikuja bustani adanganye Eva, kumvuta afanye dhambi. Shetani anakuja na anaongea na maneno kama haya mioyoni mwetu, “Inaonekana tamu sana, siyo ndiyo? Unapenda hiyo, siyo ndiyo? Unahitaji hiyo, siyo ndiyo? Jambo hili litakuletea furaha, raha na anasa! Inavuta sana, siyo nidyo? Huwezi kupinga! Chukue tu! Fanya tu! HUTAPATA HASARA!” Mawazo haya yote ni udanganyifu tu! Shetani anataka ufanye dhambi tu na kukutenga na Mungu! Mawazo haya siyo mawazo yako tu. Shetani mwenyewe anajaribu kuyaingiza mawazo hayo moyoni mwako ili uamini uongo wake na usiamini Mungu!

Lakini hila za Shetani zinakwenda kwa ndani zaidi. Shetani anajaribu kupanda mbegu ya uovu – ya kutokuamini – ndani ya mioyo yetu. Alimwambia Eva,

“Hakika HAMTAKUFA, kwa maana Mungu anajua ya kwamba siku mtakayokula matunda ya mti huo, mtafumbuliwa macho, nanyi mtakuwa kama Mungu.” (Mwanzo 3:4,5).

Unaona? Shetani anataka kutushawishi kwamba Mungu ni mwongo (‘hamtakufa’) na Mungu hataki tuwe kama Yeye! Lakini hayo yote yalikuwa kinyume cha ukweli! Mungu alikuwa amesema, “Na tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu.” (Mwanzo 1:26). Hila na mbinu za Shetani ni kukushawishi kuwa Mungu ni dhidi yako, anakunyima baraka Zake, amekuacha peke yako na hata Mungu anakuadhibu. Hilo ndilo lengo lake. Kwa hiyo neno la Mungu linasema, “Angalieni, ndugu zangu, usiwe katika mmoja wenu MOYO MBOVU WA KUTOKUAMINI, kwa kujitenga na Mungu aliye hai.” (Waebr.3:12).

Mara Adamu na Eva walipofanya dhambi, walianguka gizani kabisa (‘siku utakapokula matunda ya mti huo utakufa hakika’ – Mwanzo 2:17) na mara moja Shetani aliendelea kazi yake kwa KUPOTOSHA TABIA YA MUNGU mioyoni mwao! Adamu na Eva walijificha mara moja! Kwa nini? Kwa sababu walifikiri Mungu atakapokuja atawahukumu, kuwaponda na kuwaharibu! Walifikiri kwamba sasa Mungu hawapendi na Yeye ndiye kinyume chao na dhidi yao. (Je, umewahi kujisikia vivyo hivyo?) Walitetemeka kwa hofu! Mawazo haya siyo toba mioyoni mwao! Mawazo hayo yanatokana na Shetani! Mawazo haya ni matokeo ya kupokea maongo (sumu) ya Shetani anayepotosha sura ya Mungu ili tufikiri Mungu ndiye dhidi yetu! Mbinu za Shetani ni tutekwe nyara na mawazo na hisia za kukatiliwa – anataka tubaki peke yetu tusiende kwake Bwana!

Kwanza Ibilisi anakuja kutuvuta tufanye dhambi. Mara alipofaulu kufanya hivyo, anaanza kutushitaki kwa kali, kutulaumu na kuponda dhamira yetu ili tujisikie hatufai kabisa na tumekataliwa kabisa! Je, umewahi kupatwa na mawazo ya namna hiyo? Kwa uongo wake Shetani anataka tujisikie tumetengwa na Mungu bila tumaini na hatuwezi kwenda Kwake aliye Mwokozi wetu kwa sababu Yeye ni dhidi yetu.

Adamu na Eva waliweza kufikiri na kusema, “Kumbe, tulikosa kabisa, tulifanya dhambi mbele ya Mungu. Kwa kweli Mungu alifanya yote vizuri na alitubariki kupita kiasi na yule nyoka alitudanganya! Haya, na twende kwake Mungu na tukiri dhambi zetu mbele Yake. Na tuiname mbele Yake na tutobe! Mungu ni Mwema na Mwenye huruma, inawezekana atatusamehe!”

Haya ni toba! Haya ni imani! Waliweza kufanya hivyo – lakini sumu (uongo) ya Shetani ambayo inapotosha tabia (sura) ya Mungu machoni pa watu iliingia sana mioyoni mwa Adamu na Eva na iliwaongoza kutokumwamini Mungu na kuamini Mungu ni kinyume chao! Hiyo nidyo hila na kazi ya Shetani. Hilo ndilo lengo lake – ufikiri Mungu hakupendi na hata anakuchukia; kufikiri Mungu ni dhidi yako, ujazwe na hisia na fikra za kukatiliwa! Ibilisi anataka kuharibu imani yetu kwake Yesu na kutuweka gizani ambopo hatuamini Mungu. Tukiendelea kuamini Mungu ni kinyume chetu, ndipo hatutaweza kupokea msaada kutoka Mungu (ila Yeye ni juu yote na anaweza kufanya apendalo) kwa sababu tupo hali ya kutokuamini! Tukumbuke maandiko yasemalo,

“pasipo imani haiwezekani kumpendeza (Mungu).” (Waebr.11:6).

Kwa sababu hiyo, Waisraeli walizunguka jangwani miaka arobaini! Angalie ni wapi kutokuamini kwa Waisraeli kuliwapeleka! Sikilize maneno yao!

“Ni kwa sababu Bwana AMETUCHUKIA, ndipo akatutoa katika nchi ya Misri, apate kututia katika mikono ya Waamori, ili KUTUANGAMIZA.” (Kumbu.1:27).

Kumbe! Mungu alikuwa amefanya miujiza huku Misri na jangwani kwa ajili ya watu Wake ili kuwaokoa kwa sababu aliwapenda sana. Alikuwepo miongoni mwa watu Wake, akawatangulia mchana ndani ya wingu mfano wa nguzo, na usiku, ndani ya moto mfano wa nguzo! HATA HIVYO, kutokuamini kwao kuliwapeleka kuamini Mungu aliwachukia na akatengenza mazingira yao ili kuwaangamiza! Kwa kweli hiyo ni ‘moyo mbovu wa kutokuamini’. Tusifuate mfano wao! Hasa kwa sababu sasa ‘Mungu ameonyesha pendo lake Yeye Mwenyewe kwetu sisi, kwa kuwa Kristo alikufa kwa ajili yetu’!

Hiyo ni mbinu za Shetani, kama nilivyosema, kupotosha tabia ya Mungu mawazoni mwetu na mioyoni mwetu tusiamini Mungu na atufanye mioyo yetu iwe ugumu! Kwa hiyo maandiko yanasema, “Kwa hiyo, kama anenavyo Roho Mtakatifu, Leo, kama mtaisikia sauti yake, MSIFANYE MIGUMU MIOYO YENU, Kama wakati wa kukasirisha, SIKU YA KUJARIBIWA KATIKA JANGWA.” (Waebr.3:7,8).

Lakini, na tutambue mafundisho ya neno la Mungu – sisi hatuwezi kumlaumu Shetani! Mungu hakumlaumu Shetani kwa ajili ya kutkuamini na dhambi za watu Wake jangwani! Maandiko yanasema juu ya watu Wake jangwani, “wengi sana katika wao, Mungu hakupendezwa nao,” (1 Wakor.10:5). Na kama tulivyosoma, Mungu aliwalaumu watu Wake kwa ajili ya ‘moyo mbovu wa kutokuamini’ wao.

“Tena ni akina nani aliochukizwa nao miaka arobaini? Si wale waliokosa? Tena ni AKINA NANI aliowaapia ya kwamba hawataingia katika raha yake, ila wale walioasi? Basi twaona ya kuwa hawakuweza kuingia kwa sababu ya KUTOKUAMINI KWAO.” (Waebr.3:17:19).

Unaona, watu wa Mungu walichukua jukumu mbele ya Mungu juu ya dhambi zao – hawakuweza kumlaumu Shetani! Shetani yupo. Lakini Mungu ametupa neno Lake na anatazamia TUISHI KWA NENO LAKE na TUZIPINGE HILA ZA SHETANI! Alitazamia Adamu na Eva wafanye hivyo bustanini; alitazamia Waisraeli wafanye hivyo jangwani; na Bwana hutazamia tufanye hivyo maishani mwetu.

Ni wazi Mungu alimruhusu nyoka aingie bustanini awajaribu Adamu na Eva. KWA KUSUDI Mungu aliwaacha watu Wake jangwani waone njaa! Kwa nini? Tusikilize Mungu Mwenyewe alilosema juu ya hayo,

“Nawe utaikumbuka njia ile yote Bwana, Mungu wako aliyokuongoza miaka hii arobaini katika jangwa, ili AKUTWEZE, KUKUJARIBU kuyajua YALIYO MOYONI MWAKO, kwamba UTASHIKA AMRI ZAKE, AU SIVYO. Akakutweza, AKAKUACHA UONE NJAA, akakulisha kwa mana, usiyoijua wewe wala baba zako hawakuijua; APATE KUKUJULISHA YA KUWA MWANADAMU HAISHI KWA MKATE TU, BALI HUISHI KWA KILA LITOKALO KATIKA KINYWA CHA BWANA.” (Kumbu.8:3,4).

Unaona? Ni kusudi la Mungu tujaribiwe ili TUKUE katika imani, haki na utakatifu. Mambo mengi yanatokea, siyo kutuadhibu au kutuangamiza, ila kutupeleka TUKUE katika imani na katika Kristo Yesu. Ndio maana maandiko yanasema, “Ndugu zangu, hesabuni ya kuwa ni furaha tupu, mkiangukia katika majaribu mbalimbali; mkifahamu ya kuwa kujaribiwa kwa imani yenu huleta saburi. Saburi na iwe na kazi kamilifu, mpate kuwa wakamilifu na watimilifu bila kupungukiwa na neno.” (Yakobo 1:2-4). Na tena, “mfurahi katika dhiki pia; mkijua ya kuwa dhiki, kazi yake ni kuleta saburi; na kazi ya saburi ni uthabiti wa moyo; na kazi ya uthabiti wa moyo ni tumaini.” (Warumi 5:3,4).

Je, baada ya kubatizwa kwake, Yesu aliongozwa na ROHO MTAKATIFU nyikani KWA SABABU GANI? Biblia inatusema kwa wazi! “Kisha Yesu alipandishwa na Roho nyikani, ILI AJARIBIWE NA IBILISI.” (Mathayo.4:1). Na Luka anasema, “Yesu, hali amejaa Roho Mtakatifu…akaongozwa na Roho muda wa siku arobaini nyikani, akijaribiwa na Ibilisi. Na siku hizo alikuwa hali kitu; hata zilipotimia, aliona njaa.” (Luka 4:1,2). Kwa siku arobaini Yesu hakula kitu (siku mmoja kwa kila mwaka Waisraeli walizunguka jangwani, yaani, 40).

Na tutambue ukweli huu, Yesu aliongozwa na Roho Mtakatifu ili ajaribiwena Ibilisi. Pia, na tutambue ukweli ufuatao: Yesu alikuwa hali AMEJAA ROHO alipoongozwa nyikani ili ajaribiwa na Ibilisi, lakini baada ya kujaribiwa na Shetani, Biblia inasema kwamba, “Yesu akarudi KWA NGUVU ZA ROHO, akenda Galilaya…” (Luka 1:1-14). Aliingia nyikani AMEJAA Roho, alitoka kwa NGUVU za Roho! Unaona? Unatambua kitu?

KUSUDI la majaribu ni TUKUE katika imani, haki, utakatifu – tuchague yaliyo mema na tukatae yaliyo mabaya; tuchague Yesu na tujikane wenyewe; tumpendeze Mungu badala ya kutupendeza wenyewe, tuishi kwa neno la Mungu na kuupinga uongo wa Shetani, siku hadi siku katika mambo yote. Kwa njia hiyo tunakua katika Kristo Yesu na tunaanza kuishi kwa nguvu za Roho! Wengi hawaishi kwa nguvu za Roho, kwa msingi siyo kwa sababu ya Ibilisi, ambaye ‘kama simba angurumaye, huzunguka-zunguka, akitafuta mtu ammeze,’ bali kwa sababu hawaishi kwa neno la Mungu, hawazipingi hila za Shetani zisiingie mioyo yao! Wengi wetu wanapenda kumshambulia Shetani na kupaza sauti katika maombi yetu, lakini kwa wengi wetu ni wakati tuache kumlaumu Shetani kana kwamba yeye ni sababu ya kosa letu, au yeye ni kisingizio cha dhambi zetu! Ni wakati tutambue tabia ya kweli ya vita vyo kiroho yetu na kupinga na kusimama dhidi ya hila za Shetani! Naomba usinielewe vibaya – hapo ninaongelea mawazo yanayotaka kuingia akili na mioyo yetu. Ninaongelea majaribu yale ya kila siku yanayokupata na ‘yaliyo kawaida ya wanadamu.’ Tunasoma juu ya majaribu hayo katika 1 Wakorintho 10. Na mwanzo wa sura hiyo unashughulika na nini? Inashughulika na kutokuamini na kutokutii kwa Waisraeli jangwani!

Yesu alimshinda Shetani kwa njia gani? Je, alipaza sauti kumfukuza Shetani? Je, alimkemea kwa hasira ili kumfunga na kumtupa shimoni? Hapana! Bwana Yesu alisema tu, “Imeandkiwa…” na tena ‘Imeandikwa…” na tena, “Imeandikwa…” Yaani, Yesu aliishi kwa neno la Mungu! Yesu alinukuu mstari ule tuliousoma hapo juu akimwambia Shetani, “Imeandikwa, Mtu hataishi kwa mkate tu, ila kwa kila neno litokalo katika kinywa cha Mungu.”

Ni muhimu sana kuelewa yale yaliyoyaandikwa kwa wazi wakati Yesu alipokuwepo nyikani. Shetani alipokuja kumjaribu Yesu, lakini Bwana Yesu hakumshambulia Shetani kwa maneno! Yesu hakupaza sauti yake au kupiga kelele ili kumfukuza Shetani atoke nyikani! Ni wazi Bwana Yesu hakujaribu ‘kuifunga’ nguvu za Shetani. Hapana! Aliishi, alisimama kwa neno la Mungu tu! Shetani anakuja kuchochea kutokuamini juu ya upendo wa Mungu na uwezo wa Mungu mioyoni mwetu kwa maneno kama haya: ‘Je, Mungu wako yupo wapi? Je, anakupenda kwa kweli? Kwa nini Mungu alikuacha katika mahitaji yako? Angalia mazingira yako na niambie uwezo wa Mungu upo wapi? Kama wewe ni Mwana wa Mungu, fanya hivi au hivi!’

Ibilisi alikuja kwake Yesu na alitaka kuchochea mawazo kama hayo; Ibilisi alikuja kwao Waisraeli jangwani kuchochea mawazo hayo; nyoka alikuja kwao Adamu na Eva kuchochea mawazo hayo; na ibilisi anataka kuja kwetu na mawazo hayo ili kuchochea kutokuamini ili tusiamini upendo na uwezo wa Mungu. Hivyo ni vita vya kiroho kweli kweli ya kila siku! Tufanye nini katika vita vya kiroho? Na tufanye vile vile Yesu alivyofanya! Tusimame kwa neno la Mungu!

Watu wengi wanafikiri ‘vita vya kiroho’ ni jambo la kupaza sauti katika maombi yao na kumkemea Shetani na ‘kuifunga’ nguvu yake. Hatuna hata mstari mmoja kwenye Biblia unaotuonyesha maombi kama haya. Wengi wanakosa katika kusoma Waefeso 6:12 kwani wanafikiri ni lazima KUOMBA dhidi ya ‘falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho.’ Lakini Paulo hafundishi hivyo kama tutaona hapo chini.

Kosa la Adamu na Eva siyo kwamba hawakuomba dhidi ya ‘majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho’! Kosa la Waisraeli siyo hawakuomba dhidi ya ‘majeshi ya pepo wabaya’. Walikosa na walifanya dhambi kwa sababu WALIRUHUSU MAWAZO MAOVU KUINGIA MIOYONI MWAO; waliruhusu uongo wa Shetani kuharibu ukweli na sura ya Mungu ndani ya akili na mioyo yao – na walianguka katika kutokuamini na kutokumtii Mungu. Hawakupinga mawazo maovu ya Shetani yasiinge mioyoni mwao – hawakuishi kwa neno la Mungu. Ni rahisi kupaza sauti dhidi ya Shetani katika maombi yetu. Ni kitu kingine kuishi siku hadi siku kwa neno la Mungu tunapojaribiwa na majaribu ‘yaliyo kawaida ya wanadamu’!

Yesu alimpinga Ibilisi, alimshinda Shetani, KWA KUSHIKA NA KUISHI KWA NENO LA MUNGU! – hakuathiriwa na mawazo ya adui. Hiyo ni njia yetu, yaani, tusimame dhidi ya hila za Shetani kwa kusimama kwa neno la Mungu (Waefeso 6:11), tuzitunze akili na mioyo zetu ili tusiadhiriwe na mawazo ya Ibilisi. Hiyo ndiyo ni ‘vita vya kiroho’ kweli kweli. Tusipozipinga hila hizo za Shetani kwa namna hiyo, bila shaka itaharibu maisha yetu ya kiroho. Ni kwa sababu ya hiyo watu wengi hawaishi kwa nguvu ya Roho Mtakatifu – wanahangaika, hawana amani na hawana furaha – fikra zao zimeadhiriwa na uongo wa Shetani!

Baada ya kuzipinga hila za Ibilisi nyikani kwa neno la Mungu, maandiko yanasema,

“Kisha Ibilisi AKAMWACHA.” (Mathayo 4:11). Na maandiko yanasemaje juu yetu? Yanasema,

“Basi mtiini Mungu. MPINGENI Shetani, naye ATAWAKIMBIA.” (Yakobo 4:7).

Tunakutana na ukweli huo tena na tena katika neno la Mungu:

“Mwe na kiasi na kukesha; kwa kuwa mshitaki wenu Ibilisi, kama simba angurumaye, huzunguka-zunguka, akitafuta mtu ammeze. Nanyi MPINGENI huyo, mkiwa THABITI KATIKA IMANI.” (1 Petro 5:8,9). Tunazishinda hila za Shetani kwa imani yetu katika neno la Mungu.

Kwa msingi, vita hivyo vinahusu yanayotokea mioyoni na akilini mwetu, katika fikra zetu! Kwa hiyo Paulo anatufundisha,

“Maana ingawa tunaenenda katika mwili, hatufanyi vita kwa jinsi ya mwili – maana silaha za vita vyetu si za mwili, bali zina uwezo katika Mungu hata KUANGUSHA NGOME – tukiangusha MAWAZO na kila kitu kilichoinuka, KIJIINUACHO JUU YA MAARIFA / UKWELI YA MUNGU; na TUKITEKA NYARA KILA FIKIRA IPATE KUMTII Kristo.” (2 Wakor.10:3-5).

Unaona? Ni vile vile kama nilivyosema kwenye mwanzo wa somo hili. Tangu mwanzo Shetani (Ibilisi, nyoka) anataka kujenga ngome za mawazo ya uongo katika akili zetu. Na tunajua kwamba ‘ngome’ ni kitu chenye nguvu sana! Shetani anajaribu kujenga ngome ya mawazo ya kutokuamini na kiburi pamoja na hisia za kutamani YANAYOJIINUA juu ya ukweli ya Mungu na tabia Yake na yanayotaka kutawala juu ya fikra zetu ili tusiamini Mungu, ili tusimjue Mungu, ILI TUSITAMBUE JINSI MUNGU ALIVYO KWELI KWELI! Hiyo ni lengo la Shetani. Tena ni Shetani anayeshambulia AKILI NA MIOYO zetu na MAWAZO ya kumpinga Mungu. Ndio maana tunatakiwa kuchukua silaha za vita vyetu zinazo uwezo KATIKA MUNGU kuangusha mawazo hayo yote, yaani, kuangusha ngome ile, na ‘kukiteka nyara kila fikra ipate kumtii Kristo!’ Ni vita vinavyotokea katika mioyo na akili zetu. Je, ni nini itakayotawala katika mioyo yetu, katika fikra zetu – hila ya Shetani au neno la Mungu?

Ni Waefeso sura ya 6 inayotutoa maelezo na mafundisho zaidi juu ya vita hivyo.

“Hatimaye, mzidi kuwa hodari katika Bwana na katika uweza wa nguvu Zake. VAENI SILAHA ZOTE za Mungu ili kwamba mweze KUZIPINGA HILA za Shetani.” (Waefeso 6:10,11).

Paulo anatuhimiza hapo kwa ukweli ule ule aliotaja kwenye 2 Wakorintho sura ya kumi. Katika vita hivyo tunatakiwa kutumia silaha zote za Mungu kuzipinga hila za Shetani na kuangusha MAWAZO yajiinuayo juu ya ukweli wa Mungu na yanayotuzuia tusimjue Mungu jinsi alivyo! Kwa sababu mashambulio yanatokana na Shetani, lazima silaha zetu ni za Mungu, za kiroho, si za mwili. Paulo anaendelea kueleza ukweli huo,

“Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho.” (Waefeso 6:12).

Kwa hiyo, ndugu zangu, tufanyaje? TUOMBE dhidi ya ‘falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho’ sawasawa na mafundisho ya watu wengi? HAPANA! Hata kidogo! Paulo hasemi hivyo, hafundishi hivyo! Paulo anafafanua kwamba vita vyetu ni vya kiroho si vya kimwili na KWA HIYO ni lazima TUVAE silaha zote za MUNGU! Sikilize Paulo asemalo kwenye mstari ufuatao,

“KWA SABABU HIYO twaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kushindana siku ya uovu, na mkiisha kuyatimiza yote, kusimama.” (Waefeso 6:13).

Je, silaha zetu ni ‘maombi dhidi ya ‘majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho’? Hapana. Hasemi hivyo, hafundishi hivyo. Silaha zetu ni nini basi? Paulo anafafanua kwa wazi,

“Basi simameni, hali mmejifunga KWELI viunoni,

na kuvaa DIRII YA HAKI kifuani,

na kufungiwa miguu utayari tupatao kwa INJILI YA AMANI;

ZAIDI YA YOTE MKIITWAA NGAO YA IMANI, AMBAYO KWA HIYO MTAWEZA KUIZIMA MISHALE YOTE YENYE MOTO YA YULE MWOVU.

Tena ipokeeni CHAPEO YA WOKOVU, na upanga wa Roho AMBAO NI NENO LA MUNGU.” (Waefeso 6:13).

Mafundisho ya Paulo juu ya ‘vita vya kiroho’ inahusu mwendo wetu wa kiroho na nidhamu yetu mbele ya Mungu, yaani, jinsi ya kusimama katika haki, utakatifu na imani katika maisha yetu ya kila siku tunapokutana na mashambulio yanayotokana na Shetani! Hataji maombi juu ya ‘majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho.’ Silaha hizo za Mungu zinatukinga na mashambulio ya Shetani; zinatunza akili zetu (chapeo ya wokovu) na mioyo yetu (dirii ya haki). Naomba tusome yafuatayo kwa makini sana kwani yanahusu somo hili kwa ndani sana: Paulo anaposema ‘zaidi ya yote’ anatushauri nini? Anatuhimiza tuitwae NGAO YA IMANI! Ukweli huu unahusu somo hili moja kwa moja; unahusu vita vya kiroho yetu moja kwa moja! Ngao ya imani ni silaha yetu ya muhimu na yenye nguvu! Kama Yohana anavyosema,

“Kwa maana kila kitu kilichozaliwa na Mungu huushinda ulimwengu; na huku ndiko kushinda kuushindako ulimwengu, hiyo imani yetu.” (1 Yoh.5:4).

Lakini tunajua imani (chanzo chake ni kusikia; na kusikia) huja kwa neno la Mungu. Kwa hiyo Paulo anatuambia tuutwae upanga wa Roho ambao ni NENO LA MUNGU!

Sasa tupo hapo mwanzo tena! Mungu alitazamia Adamu na Eva waishi kwa neno Lake ambalo alikuwa amewaambia – alitazamia kwa kuamini neno Lake wazipinge hila za Shetani bustani na kusimama dhidi ya uongo wake. Mungu alitazamia watu wake Waisraeli washike na kuishi kwa neno Lake (‘upanga wa Roho’) jangwani na kuizima mishale yote ya yule mwovu kwa imani (‘ngao ya imani’) na kutokuruhusu uongo wa Shetani kuiathiri mioyo yao! Bwana Yesu alitumia neno la Mungu tu kumpinga Shetani nyikani.

Vita vya kiroho kwa msingi vinahusu kuyapinga au kuyaangusha mawazo ambayo Shetani anataka kuchochea moyoni mwetu yajiinuayo juu ya tabia ya Mungu na yanayotupeleka kutokumwamini Mungu na wokovu Wake! Mawazo yale yanakuja kama mishale kukata tamaa kabisa na kutupeleka kujihurumia, kunung’unika, kukasirika na wengine na kuchockea kiburi moyoni mwetu kwa upande moja, na kwa upande mwingine kukufanya ujisikie Mungu ni kinyume chako, amekuacha na anakuadhibu. Kwa msingi mawazo hayo yanaathiri mioyo yetu ili tusitambue Mungu wala matendo Yake katika maisha yetu, na tusimjue Mungu jinsi alivyo. Kwa hiyo ni muhimu sana tuvae silaha zote za Mungu! Na silaha hizo zinazingatia, ‘ngao ya imani’ na ‘upanga wa Roho’. Pia zinazingatia ‘chapeo ya wokovu’. Chapeo kinalinda nini? Kinalinda kichwa chako! Na kichwa ni mahali ambapo mawazo yetu tunatokea!

Baada ya kuvaa silaha zetu zote, je, Paulo sasa anatuelekezea kuomba dhidi ya ‘majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho’? Hapana! Tunaposimama katika imani tukivaa silaha zote anatuelekezea tuombe kwa namna ya ifuatayo,

“kwa sala zote na maombi mkisali kila wakati katika Roho, mkikesha kwa jambo hilo na kudumu katika KUWAOMBEA WATAKATIFU WOTE; pia na KWA AJILI YANGU mimi, nipewe usemi kwa kufumbua kinywa changu, ili NIIHUBIRI kwa ujasiri ile siri ya INJILI.” (Waefeso 6:18,19).

Hakuna mahali mmoja katika Biblia ambapo tunasoma kwamba hata muumini mmoja katika maombi yake anaomba dhidi ya Shetani, falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, na juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho. Hata Danieli hakuomba juu ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho – yeye aliomba kwa ajili ya kazi ya Mungu na watu wa Mungu tu! Na kwenye mistari hiyo tunaona vile vile, yaani, Paulo anatuelekeza tusimame imara katika Bwana ili tuweze kuomba kwa ajili ya WATAKATIFU wote – yaani, kwa waumini wote katika Kristo – na kwa ajili ya kazi ya Mungu na Injili!

Kwa nini nilinukulu Kutoka 20:2-4 hapo juu? Kwa sababu Mungu amejidhihirisha kadiri ya ifuatayo:

“BWANA, BWANA, Mungu MWENYE HURUMA na NEEMA, ASIYE MWEPESI WA HASIRA, MWINGI wa UPENDO na UAMINIFU…” (Kutoka 34:6).

Hiyo ndiyo tabia au ‘sura’ ya Mungu, lakini Shetani anataka kuchora ‘sanamu’ mawazoni au ‘kichwani’ mwako; anajaribu kubadilisha ‘sura’ ya Mungu, kumfanya Mungu aonekane kama mtu mkali machoni pako, kama Mungu ndiye mbali nawe na dhidi yako! Hiyo ni mbinu za Ibilisi kila siku!

Lakini hiyo siyo jambo la kumlaumu Shetani, kumtumia kama kisingizio cha dhambi zako au kutokuamini kwako! Mungu ametupa silaha ili tuzipinge hila hizi za Shetani!

Kama nilivyosema, kwanza Ibilisi anakuja kutuvuta na kutushawishi tufanye dhambi. Lakini mara tunapokosa, anabadilisha mbinu yake na anaanza kwa nguvu kutulaumu, “Onaona, hufai! Hufai kabisa! Umekosa tena! Hupendi Mungu kwa kweli. Mungu hakupendi! Ulikosa mara nyingi. Huwezi kushinda dhambi hiyo! Huna uwezo kushinda! Wewe ni mwenye udhaifu! Utashindwa tu! Wewe si kitu! Wengine wanashinda na wanabarikiwa lakini siyo wewe kwa sababu Mungu siyo kwa upande wako!” Kwa maneno na mawazo haya Shetani anataka kukata tamaa kabisa ili tusiamini Mungu, ili tusiende kwake Yesu mara moja tupate neema na msamaha na kuwekwa huru mbali na dhambi!

Mawazo yanayotoka kwake Shetani yanatusukumu MBALI na uwepo ya Bwana, tujisikie peke yetu kabisa. Huduma ya Roho Mtakatifu ni tofauti sana na kazi ya Ibilisi! Kama tukikosa au tukishindwa, Roho ya Mungu anaongea kwa sauti ya pole sana kwa dhamira yetu! Biblia inasema Roho ya Mungu ni kama HUA. Siyo kama mtu mkubwa mkali ambaye anakuja kutupiga na fimbo! Bwana apewe sifa kwa neema Yake! Roho hatupondi, hatusukumu au kutufukuza mbali na Mungu! Roho ya Mungu anatujulisha kosa letu lakini pamoja na hiyo anatuonyesha Yesu ndiye Mwokozi na Msaada wetu, yaani, kwa huduma Yake, Roho ya Mungu anatuvuta tuje kwa Bwana, na tuje mara moja! Na Roho ya Mungu anaongea nasi kwa neno la Mungu! “Roho wa kweli, atawaongoza awatie kwenye kweli yote; kwa maana hatanena kwa shauri lake mwenyewe, lakini yote atakayoyasikia atayanena, na mambo yajayo atawapasha habari yake. Yeye atanitukuza mimi.” (Yoh.16:13,14).

Unaona, huduma na mawazo ya Shetani yanakusukuma na kufukuza mbali na Bwana, na kinyume chake, huduma na sauti ya Roho ya Mungu inakuvuta kwa Bwana upate msamaha, rehema na neema ya Mungu mara moja na kutuweka huru mbali na dhambi! Bwana asifiwe kwa neema kama hiyo kuu! Na hiyo siyo kwamba tufanye dhambi tena ila tupate faraja na neema ili tumwamini Mungu tushinde kwa neema ya Bwana na kwa nguvu za Roho Yake! Usikate tamaa! Kila mara nenda kwa Bwana; mwamini Yeye kwa moyo wako wote; soma neno lake; chukua muda uwe pamoja na Baba na Mwana; mpende Bwana kwa moyo wako wote na ujitoe kwake kabisa kila siku.

“Basi, tuseme nini juu ya hayo? Mungu akiwapo upande wetu, ni nani aliye juu yetu? Yeye asiyemwachilia Mwana wake mwenyewe, bali alimtoa kwa ajili yetu sisi sote, atakosaje kutukirimia na mambo yote pamoja naye? Ni nani atakayewashitaki wateule wa Mungu? Mungu ndiye mwenye kuwahesabia haki. Ni nani atakayewahukumia adhabu? Kristo Yesu ndiye aliyekufa; naam, na zaidi ya hayo, amefufuka katika wafu, naye yuko mkono wa kuume wa Mungu; tena ndiye anayetuombea. Ni nani atakayetutenga na upendo wa Kristo? Je! Ni dhiki au shida, au adha, au njaa, au uchi, au hatari, au upanga? Kama ilivyoandikwa, ya kwamba, Kwa ajili yako tunauawa mchana kutwa, Tumehesabiwa kuwa kama kondoo wa kuchinjwa. Lakini katika mambo hayo yote tunashinda, na zaidi ya kushinda, kwa yeye aliyetupenda.” (Warumi 8:31-37).

© David Stamen 2017 somabiblia.com

RUDI KWA MWANZO

21

KUSUDI LA MAJARIBU KATIKA MAISHA YAKO

Je, baada ya kubatizwa kwake, Yesu aliongozwa na nani nyikani? Neno la Mungu linatufundisha aliongozwa na ROHO MTAKATIFU nyikani. Aliongozwa nyikani kwa sababu gani? Biblia inatusema kwa wazi! “Kisha Yesu alipandishwa na Roho nyikani, ILI AJARIBIWE NA IBILISI.” (Math.4:1).

Na Luka anasema, “Yesu, hali amejaa Roho Mtakatifu…akaongozwa na Roho muda wa siku arobaini nyikani, akijaribiwa na Ibilisi.”

Basi, Yesu alikuwa hali AMEJAA ROHO alipoongozwa na Roho Mtakatifu nyikani ili ajaribiwa na Ibilisi, lakini baada ya kujaribiwa na shetani, Biblia inasema kwamba, “Yesu akarudi KWA NGUVU ZA ROHO, akenda Galilaya…” (Luka 1:1-14).

Aliingia nyikani amejaa Roho, alitoka kwa nguvu za Roho!

KUSUDI la majaribu ni TUKUE katika maisha ya kiroho yetu, katika imani, haki, utakatifu na katika upendo wetu kwake Mungu – tuchague yaliyo mema na tukatae yaliyo mabaya; tuchague Yesu na tujikane wenyewe; tumpendeze Mungu badala ya kutupendeza wenyewe, siku hadi siku katika mambo yote. Kwa njia hiyo tunakua katika Kristo Yesu na tunaanza kuishi kwa nguvu za Roho. Tunaweza kuanzisha vizuri, lakini tunaendeleaje?

Tutapita majaribu. Lakini majaribu siyo adui yetu. Tatizo lenyewe siyo tatizo. Tatizo kwa dhati linatokeza usipojidhughulisha na tatizo kama unavyopaswa! Ndiyo maana Yakobo anasema,

“Ndugu zangu, hesabuni ya kuwa ni FURAHA tupu, mkiangukia katika majaribu mbalimbali; mkifahamu ya kuwa kujaribiwa kwa imani yenu huleta saburi. SABURI NA IWE NA KAZI KAMILIFU, MPATE KUWA WAKAMILIFU na watimilifu bila kupungukiwa na neno.” (Yakobo 1:2-4).

Mungu anataka tuwe na mtazamo wa namna huo.

Je, unafikiri Bwana alishtuka kuona kwamba Ibilisi aliingia bustani ya Edeni? Sidhani! Mungu alimpa Ibilisi nafasi kuingia bustani ili awajaribu Hawa na Adamu, vile vile alivyomruhusa Shetani kumjaribu Yesu nyikani. Sikiliza neno la Mungu kwao watu wake jangwani, “Nawe utaikumbuka njia ile yote Bwana, Mungu wako aliyokuongoza miaka hii arobaini katika jangwa, ili akutweze, KUKUJARIBU, KUYAJUA YALIYO MOYONI MWAKO, kwamba utashika amri zake, au sivyo. Akakutweza, AKAKUACHA UONE NJAA, akakulisha kwa mana, usiyoijua wewe wala baba zako hawakuijua; APATE KUKUJULISHA ya kuwa mwanadamu haishi kwa mkate tu, bali huishi kwa kila litokalo katika kinywa cha Bwana.” (Kumbu.8:2,3).

Unaona? KWA KUSUDI Mungu aliwaacha watu wake waone njaa! Kwa nini? Kuyajua yaliyo moyoni mwao, kama wangeshika amri zake au sivyo; kama wangemwamini Mungu au sivyo; kama wanampenda Mungu KULIKO MAMBO YOTE MENGINE, haijalishi yanayotokea au yasiyotokea katika mazingira yao! Na Bwana Yesu alipita jaribu lilelile nyikani naye hakunung’unika – alinukuu mstari uleule ya Kumbu.8:3! Aliishi KWA NENO LA MUNGU! Alisimama kwa neno la Mungu; alikataa kushawishiwa na maongo ya Shetani; hakulalamika ili Mungu amwondoe Shetani au mazingira yale ambyo MUNUG MWENYEWE ALIPANGA KWA AJILI YAKE MAJIRA ILE! Kwa hiyo Biblia inasema, “Basi mtiini Mungu (au umnyenyekee Mungu). Mpingeni Shetani, naye atawakimbia.” (Yakobo 4:7).

Inawezekana watu wengi hawatumbui mkono au uongozi wa Mungu katika maisha na mazingira yao, katika majaribu yao. Wanalalamika kana kwamba Bwana amewaacha au wanapenda kumlaumu Shetani badala ya kumpinga! Badala ya kujitoa kwake Mungu na kujikana, wanachagua kujipendeza, kujifurahisha au kujihurumia! Badala ya kupinga maongo ya Ibilisi na kuizima mishale yote yake yenye moto, wanalalamikia mazingira yao tu.

Tatizo katika bustani ya Edeni, tatizo katika jangwa la Sinai kimsingi halikuwa shetani, halikuwa upungufu wa vitu au chakula – lilikuwa kutokuamini na kutokutii ya Adamu na Hawa, ya Waisraeli! Walilalamika na kushindwa NA MAMBO YALEYALE AMBAYO MUNGU MWENYEWE AMESHAYAPANGA KWA AJILI YAO ILI WAKUE – katika maisha ya kiroho yao – KUPITIA YAO NA KUIMARISHIWA NAYO!

Ndiyo maan imeandikwa, “na mfurahi katika dhiki pia; mkijua ya kuwa dhiki, kazi yake ni kuleta saburi, na kazi ya saburi ni uthabiti wa moyo; na kazi ya uthabiti wa moyo ni tumaini; na tumaini halitahayarishi…” (Warumi 5:3-5). Lengo la dhiki na majaribu ni kuwa tukue katika maisha ya kiroho yetu.

Miaka mingi iliyopita nilipofundisha katika kanisa fulani huko Dar Es Salaam juu ya Warumi 5:3, mtafsiri wangu alinidakiza akiniambia, “Watu hawapendi kusikiliza ujumbe wa namna huo!” Kumbe! Watu wa Mungu huchukizwa na neno Lake! Na sisi? Lakini hata mfalme Daudi katika Agano la Kale alikiri, “Umenifanyizia nafasi wakati wa shida…” (Zaburi 4:1).

Na neno hili lenye maana sana liingie mioyoni mwetu, “Jaribu halikuwapata ninyi, isipokuwa lililo KAWAIDA ya wanadamu; ILA MUNGU NI MWAMINIFU; ambaye hatawaacha mjaribiwe kupita mwezavyo; lakini pamoja na lile jaribu atafanya na mlango wa kutokea, ili mweze kustahimili.” (1 Wakor.10:13). Hasemi ataliondoa jaribu lile haraka haraka. Anasema ‘pamoja na lile jaribu atafanya na mlango wa kutokea’, basi tukumbuke Yakobo alilosema, “Saburi na iwe na kazi kamilifu, mpate kuwa wakamilifu na watimilifu bila kupungukiwa na neno.”

Lakini Mungu hajatuacha peke yetu! Neno la Mungu linatutia moyo kwa kutufundisha,

“Basi, iwapo tunaye kuhani mkuu aliyeingia katika mbingu, Yesu, Mwana wa Mungu, na tuyashike sana maungamo yetu. Kwa kuwa hamna kuhani mkuu asiyeweza kuchukuana nasi katika mambo yetu ya udhaifu; bali yeye alijaribiwa sawasawa na sisi katika mambo yote, bila kufanya dhambi. Basi na tukikaribie kiti cha neema kwa ujasiri, ili tupewe rehema, na kupata neema ya kutusaidia wakati wa mahitaji.” (Waebr.4:14-16).

Kwa hiyo tusishangae ila tuyatafakari na kuyapokea maneno ya Petro aliposema, “Mnafurahi sana wakati huo, ijapokuwa sasa kwa kitambo kidogo, ikiwa ni lazima, mmehuzunishwa kwa majaribu ya namna mbalimbali; ili kwamba kujaribiwa kwa imani yenu, AMBAYO INA THAMANI KUU KULIKO DHAHABU ipoteayo, ijapokuwa hiyo hujaribiwa KWA MOTO, kuonekane kuwa kwenye sifa na utukufu na heshima, KATIKA KUFUNULIWA KWAKE YESU KRISTO.

Mungu atubariki na neno Lake.

© David Stamen 2017 somabiblia.com

RUDI KWA MWANZO

22

JE, NAWEZA KUJUA MAPENZI YA MUNGU KWA MAISHA YANGU?

Tunaweza kumshukuru Mung kwani Yeye hajaficha mapenzi Yake juu yetu! Paulo anasema,

“Maana haya ndiyo mapenzi ya Mungu, KUTAKASWA KWENU, mwepukane na uasherati.” (1 Wathes.4:3).

Je, unataka kufanikiwa, unapenda kutimiza ndoto yako au lengo lako? Lakini haya yote hayana maana, ni bure tu kama ukianguka kwenye dhambi ya uzinzi, au dhambi nyingine ya siri? Siku hizi, wengi wanajitahidi sana wafanikiwe. Je, unajitahidi kufanakiwa katika kutakaswa kwako? Je, inawezekana wengi hawajajali mapenzi ya Mungu ya dhati katika maisha yao siku hizi ili waweze kuifuate ndoto zao tu, wakidai ‘ndoto’ zao ni ‘mapenzi ya Mungu’? Mambo mengine yote katika maisha yetu ni BURE tu kama tukifuata anasa ya mwili, kuona mambo machafu kwenye mtandao au kujiunga na facebook group ya picha za ngono.Haya ndiyo mapenzi ya Mungu, KUTAKASWA KWENU, kuishi maisha ya UTAKATIFU kwa MOYO SAFI!

Tuendeleeni! Paulo anafundisha kwamba, “FURAHINI siku zote; OMBENI bila kukoma; SHUKURUNI kwa kila jambo; maana HAYO NI MAPENZI YA MUNGU kwenu katika Kristo Yesu.” (1 Wathes.5:18).

Mapenzi ya Mungu kwa maisha yangu ni nini? Hayo ni mapenzi ya mungu kwangu! Tunaweza kumshukuru Mungu sana kwani alidhihirisha mapenzi yake kwa ajili ya masiha yetu kwa wazi! Kabla ya mambo mengine yote, Mungu amedhihirisha mapenzi yake juu maisha yangu na maisha yako ni tufurahi siku zote, tuombe bila kukoma na kumshukuru katika kila jambo! Kwa hiyo, usizunguke zunguke, usitafute tafute ukijiuliza ‘mapenzi ya Mungu katika maisha yangu ni nini?’, ila ‘pokea kwa upole neno lile lililopandwa ndani, liwezalo kuziokoa roho yako’. (Yakobo 1:21).

Je, naweza kujua MWITO wa Mungu kwa maisha yangu? Ndiyo, naweza! Paulo anatujulisha kwamba, “Mungu…alituokoa akatuita kwa MWITO MTAKATIFU si kwa kadiri ya matendo yetu sisi, bali kwa kadiri ya makusudi yake yeye na neema yake.” (2 Tim.1:9). Na Petro anathibitisha ukweli huo, “…kama yeye aliyewaita alivyo mtakatifu, ninyi nanyi IWENI WATAKATIFU KATIKA MWENENDO WENU WOTE…” (1 Petro 1:15).

Paulo anatusihi, “mwenende kama inavyoustahili WITO WENU MLIOITIWA; kwa UNYENYEKEVU wote na UPOLE, kwa UVUMILIVU, mkichukuliana katika UPENDO;” (Waefeso 4:1,2)! Siku hizi wengi wanatafuta waitalo ‘kusudi’ la maisha yao wakati hawajali MWITO WA MUNGU ambao tayari ameshaudhihirisha kwetu kupitia neno lake! Je, tunafurahia zaidi kufuata ‘kusudi letu’ na kutimiza ‘ndoto yetu’ kuliko kufuata na kuishi sawasawa na neno la Mungu na kutumiza mwito wetu unaotokana moja kwa moja na Mungu?

Katika Waebrania tunaambiwa jambo la ajabu juu ya mwito wetu, “Kwa hiyo, ndugu watakatifu, wenye kuushiriki MWITO WA MBINGUNI, mtafakarini sana…Yesu.” (3:1). Hii ni neema kubwa sana kwetu; tumeitwa na mwito wa mbinguni, tuwe kama Yesu Kristo ulimwenguni humu! Sawasawa na mafundisho ya Yohana, “…kama Yeye alivyo, ndivyo tulivyo na sisi ulimwenguni humu.” (1 Yoh.4:17). Na Paulo anaeleza ukweli mkuu sana, “Kwa maana sisi tu MANUKATO YA KRISTO, mbele za MUNGU, katika wao wanaookolewa, na katika wao wanaopotea; katika hao wa pili harufu ya mauti iletayo mauti; katika hao wa kwanza harufu ya uzima iletayo uzima.” (2 Wakor.2:15,16). Huo ndio mwito mkuu, siyo ndiyo? Je, tunautafuta mwito kuu kuliko huo? Kama ni hivyo, labda Mungu ataongea nasi kama vile alivyoongea na Baruku aliposema, “Je! Unajitafutia mambo makuu? Usiyatafute!” (Jer.45:5).

Sisi tumeitwa tuwe HARUFU YA KRISTO mbele za Mungu KWANZA na KWA KIMSINGI. Tunaishi mbele ya Mungu kwanza, siyo mbele ya watu. Bila kuwa harufu ya Kristo MBELE YA MUNGU, hatuwezi kuwa baraka kweli kweli kwao wengine! Kama ilivyoandikwa katika Kitabu cha Kutoka sura ya 29, Mungu aliwaagiza makuhani watoe, “wana-kondoo wa mwaka mmoja wawili SIKU BAADA YA SIKU DAIMA. Mwana-kondoo mmoja utamchinja asubuhi; na mwana-kondoo wa pili utamchinja jioni …IWE HARUFU NZURI,… Itakuwa ni sadaka ya kuteketezwa MILELE…MBELE YA BWANA. HAPO NITAKAPOKUTANA NANYI, ili ninene na wewe HAPO.” (29:38-42). Kumbe, Mungu Baba yetu anakutana nasi mahali pa madhabahu ya dhabihu naye anatazamia tutoe maisha yetu yawe harufu ya Yesu Kristo mbele Yake, ‘asubuhi na jioni’, yaani, wakati wote! Yesu Kristo ni Mwana-Kondoo wa Mungu! Na mahali pale pale pa sadaka anatutakasa ili tumtimikie tulipo. (“…nitaitakasa…hiyo madhabahu; pia Haruni na wanawe NITAWATAKASA, ILI WANITUMIKIE katika kazi ya ukuhani.” 29:44). Jambo la ajabu! Kwa hiyo Paulo anasema, “Basi, ndugu zangu, nawasihi, kwa huruma zake Mungu, ITOENI MIILI YENU IWE DHABIHU ILIYO HAI, TAKATIFU, YA KUMPENDEZA Mungu, ndiyo ibada yenu yenye maana. Wala msiifuatishe namna ya dunia hii; bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia zenu, MPATE KUJUA HAKIKA MAPENZI YA MUNGU aliyo mema, ya kumpendeza, na ukamilifu.” (War.12:1,2).

Basi, usijisumbue kwa ajili ya mapenzi ya Mungu mawazoni mwako. Kwa kimsingi sasa unaijua njia. Njia ni Yesu Kristo. Fanya kama Paulo alivyofanya; uwe na fikra ya Paulo aliyesema,

“Ndugu, sijidhanii nafsi yangu kwamba nimekwisha kushika; ila NATENDA NENO MOJA TU; nikiyasahau yaliyo nyuma, nikiyachuchumilia yaliyo mbele; NAKAZA MWENDO, NIIFIKILIE mede ya THAWABU YA MWITO MKUU wa Mungu katika Kristo Yesu. Basi…na tuwaze hayo.” (Wafilipi3:13,14).

Lile usilolijua, subiri tu mbele Yake, na kwa wakati wake utalijua. Yatoe maisha yako yawe dhabihu iliyo hai, yawe harufu ya Kristo mbele Yake kila siku, bila kuitafuta njia yako mwenyewe, na neno la Mungu linatuambia utapata kujua hakika mapenzi ya Mungu, hatua kwa hatua na kwa wakati wake! Na kumbuka Paulo alilosema katika mstari unaofuata, yaani, “Kwa maana kwa neema niliyopewa namwambia kila mtu aliyeko kwenu ASINIE MAKUU KUPITA ILIVYOMPASA KUNAI.” Mungu akubariki!

© David Stamen 2014 somabiblia.com

RUDI KWA MWANZO

23

WEWE NI MFUNGWA WA NINI?

Mtume Paulo alikwepo gerezani wakati alipoandika barua kwao watakatifu waliopo Efeso. Katika sura 4 mstari 1 anajiita ‘mfungwa katika Kristo Yesu.” Hakusema yeye ni mfungwa wa serikali, au mfungwa wa Kaisari, au mfungwa wa mazingira yake, au mfungwa wa shetani! Alikiri ukweli uliomo moyoni mwake, yaani, yeye ndiye mfungwa wa Kristo Yesu! Huo ndio mtazamo wa kiroho! Hakujali vifungo vyake, hakujali gereza, hakujali mazingira yake; ni kama alitangaza kwa watu wote, “Mimi ni mfungwa wa Bwana! Mazingira haidhuru kwangu!”

Sasa, ndugu yangu, kijiji sio gereza lako! Wewe sio mfungwa wa kijiji chako, au wa ndoa yako, au wa kazi yako, au wa mazingira yako, au wa wivu ya ndugu zako! Bwana asifiwe! Anatupa neema zaidi! Huwezi kusema, ‘Mazingira haya, au upungufu wa jambo hili, au mtu yule, au ndugu huyo vinanizuia kukua kiroho, zinanizuia nisiendelee mbele katika Bwana.’ Hapana! Siyo kweli! Kama wakristo, sisi tu wafungwa wa Bwana tu – tumtumikie Yesu katika kila mazingira – kuishi kijijini au kutoka, tufanye kama wafungwa wa Bwana kama Yeye anavyopenda – kadiri ya mapenzi Yake, siyo ya kwangu.

‘Yupo mtu fulani mgumu kazini kwangu anayezuia maisha ya kiroho!’ Hiyo siyo kweli. Kazi yako siyo gereza lako, na kama mfungwa wa Bwana unapswa kumwonyesha yule neema na msamaha na usiwe mfungwa wa uchungu au ugumu au hasira moyoni mwako, kwa sababu ‘Mungu huwapinga wajukuzao bali huwapa neema wanyenyekevu.’ Kama Paulo anavyosema sehemu ile ile katika Waefeso sura ya nne, “Basi, mimi niliye MFUNGWA WA BWANA, nawasihi mwenende kama inavyostahili WITO WENU mlioitiwa. iweni WANYENYEKEVU kabisa na WAPOLE, mkiwa WAVUMILIVU, mkichukuliana KWA UPENDO.” Hiyo ilikuwa nia au ‘mtazamo’ wa Paulo! Wengine (hasa mjini) wanatafuta ‘mtazamo’ mzuri ili waboreshe maisha yao au kufikia lengo lao wapate ‘mafanikio’! Lakini nia ya Paulo ilikuwa “Mimi niliye mfungwa wa Bwana – sina mapenzi yangu ya binafsi, sina malengo yangu ya binafsi; namtumikia Bwana, natafuta mapenzi Yake tu, na goali (malengo) yangu ndiyo, ‘nimjue Yeye na uweza wakufufuka kwake, na ushirika wa mateso Yake.’ Mambo nyingine yote ni ‘mavi’ kwangu!” Nia ya Paulo ilikuwa kuhesabu mambo yote kama ‘mavi’ ili apate Kristo! Sasa, lengo (goali) la Paulo ni lengo letu? Na tunahesabu yote kama ‘mavi’ ili tupate Kristo? Hatupo kanisani sasa! Huwezi kusema ‘Amen’ kwa mdomo mbele ya watu. Upo peke yako, jibu kwa kweli moyoni mwako.

Au labda yote siyo ‘mavi’ kwako, na mafundisho ya ulimwengu wa biashara na wahubiri wahamasishaji (‘motivational speakers’) watokao Magharibi/Ulaya wafundishao juu ya ‘mafanikio’ yanayokuvuta. Mafundisho haya ya kibinadamu na filosofia ya ulimwengu huo yameingiza makanisani na yanaharibu maisha ya kiroho ya weeeengi.

Usinielewe vibaya. Sisemi hatuwezi kufanya kazi kwa bidii au kuweka mipango juu ya kazi yetu. Haya ni vizuri, lakini na tumtumikie Bwana Yesu kiasi cha kutokuruhusu cho chote kutuchukua MATEKA, hata kama ni jambo ‘nzuri’! Umjue Bwana Yesu ni lengo lako kiasi cha kutokujali jambo lo lote lile kutawala katika maisha yako au katika mawazo yako – siyo pesa, wala cheo, wala sifa ya watu, wala biashara, wala malalamiko juu ya mazingira yako! Kama Paulo alivyosema, “Vitu vyote ni halali kwangu, lakini si vitu vyote vyenye faida. Vitu vyote ni halali kwangu,” lakini SITATAWALIWA NA KITU CHO CHOTE.” 1 Wakor.6:12.

Ndoa yako siyo gereza lako! Kama unayo shida hiyo, ni nafasi kukua katika neema na upendo wa Mungu. Sisemi hivyo cha kiurahisi! Maisha ni maisha (life is real) na tunapaswa kila siku kuchagua tuwe mfungwa wa hasira na uchungu au ugumu wa moyo, au kuchagua tuwe mfungwa wa Bwana, yaani, SINA UHURU, sina haki kukasirika mpaka usiku, sina haki kuruhusu uchungu, ugumu, chuki, wivu au kutokusamehe ziingize moyo wangu! Mimi ndimi mfungwa wa Bwana! Nimewekwa huru kumpenda jirani yangu! “Kwa maana kwangu mimi, kuishi ni Kristo na kufa ni faida.” (Wafil.1:21). Hiyo ndiyo Injili yenye nguvu ya Mungu kubadilisha maisha yetu tuwekwa uhuru kweli kweli!

“Aaaaah, kama mazingira yangu yangekuwa tofauti!” Amke ndugu! Usijidanganye! Usilalamike, badala yake, “itoeni miili yenu iwe dhabihu iliyo hai, takatifu na inayompendeza Mungu, hii ndiyo ibada yenu yenye maana.”

Je, unataka kuoa au kuolewa? Kumbuka, wewe ni ‘mfungwa wa Bwana’ ili usifanye mapenzi yako bali mapenzi ya Mungu! Ndugu yangu, dada yangu, ‘umngoje Bwana’. Usitafute njia ya mkato (‘short cut’) kwa kuwa unafikiri umesubiri kupita kiasi! Usimjalie Shetani kukushawishi kwamba huwezi kupinga au kukataa anasa ya dhambi! Usimjalie kuharibu maisha yako duniani na kwa milele! Umngoje Bwana kwa moyo wako wote. Ujimtoe maisha yako kabisa! Kwa wakati mzuri atakubariki! Ni jambo la kuhuzunishwa sana kwamba wengi wanaanguka mahali hapa. Mimi nilioa kwa umri wa miaka thelathini na tano, na Mungu alinitunza kwa neema na nguvu Yake mpaka wakati ule ule, na mpaka sasa hivi pia! Ndiyo, pengine ni lazima ufe, kama tulivyoona, “Kwa maana kwangu mimi, kuishi ni Kristo na kufa ni faida.” Maisha siyo mchezo! Kama hatuchukii nafsi yetu wenyewe, hatuwezi kuwa wanafunzi wa Yesu! Umngoje Bwana!

Kama wewe na mimi ni wafungwa wa Bwana, tupo uhuru! Tupo uhuru kumtumikia Yeye kwa neema, unyenyekevu na upendo katika mazingira yote. Kwa hiyo Paulo anasema, “Furahini katika Bwana sikuzote! Paulo alisema, “Naweza kuyafanya mambo yote katika Yeye anitiaye nguvu.” Je, aliweza kufanya nini kwa nguvu ya Bwana? Anatueleza kwa wazi! “Kwa maana nimejifunza kuridhika katika hali yo yote. Ninajua kupungukiwa, pia ninajua kuwa na vingi. Nimejifunza siri ya kuridhika katika kila hali, wakati wa kushiba na wakati wa kuona njaa, wakati wa kuwa na vingi na wakati wa kupungukiwa. Naweza kuyafanya mambo yote katika Yeye anitiaye nguvu” (Wafil.4:11,12). Siku hizi wengi wanakimbilia ‘manafikio’! Paulo alimfuata Yesu na kwa hiyo aliridhika katika hali yo yote! Na mimi, na wewe? Faida kubwa ni nini? Tena Paulo anatuambia, “Lakini utauwa na kuridhika ni faida kubwa.” Mungu apewe sifa kwa mafundisho wazi kabisa! Usiwe mfungwa wa ‘mafanikio’!

Tunaimba, “Yesu unatosha.” Ni kweli? Unataka nini? Unatafuta nini? Maisha yanatuongoza tuchague kila siku. Ndugu, tuchague ile iliyo bora! Na tuwe mfungwa wa Bwana!

© David Stamen 2015 somabiblia.com

RUDI KWA MWANZO

24

NAYAHESABU MAMBO YOTE KUWA NI MAVI, ILI NIMPATE KRISTO

Je, ikoje kwako wewe juu ya jambo kama hilo? Huo ni mtazamo wako kwa dhati?

Nilifundisha juu ya ukweli huo kwa wanachuo kikuu na nilizingatia hata Digrii (Shahada) yangu chini ya kichwa ya mambo ya ‘mavi’. Wengi wao walishtuka. Na baada ya kipindi kile kiongozi wa vijana alinijulisha kuwa wanachuo hawakupenda nitumie lile neno ‘mavi’! Sasa hapo ikawa ni zamu yangu kushtuka! Nilimwambia wanachuo wale baadae kuwa ‘Mavi’ ni neno la kibiblia! Na kwamba alikuwa ni Roho wa Mungu aliye mwongoza Mtume Paulo kulitumia NENO HILO katika muktadha huu! Mungu analitumia neno hilo KWA UTHABITI WA MAKUSUDI HAYA. Yaani, kutuonyesha sisi kuhusu mtazamo au fikra zetu zinavyopaswa kuwa kwa mambo mengine yote ya kidunia pale tunapoyalinganisha na mambo ya kumjua Kristo. Na Paulo aliyahesabu kuwa ni mavi! Na ni nini hasa muktadha wa habari hii katika sura ya Wafilipi sura ya 3. Hapo mtume Paulo alikuwa anaongelea kuhusu MALEZI yake aliyokulia nayo pamoja na ELIMU yake kama Mfarisayo, lakini kisha anaendelea kusema kuwa anayahesabu MAMBO YOTE kuwa kama MAVI ili kwamba AMPATE KRISTO YESU. Je, tunaweza kushuhudia lilelile?

Kuna maneno mengi nyakati hizi za leo yahusuyo mtu kuwa na “malengo”, “goli” au “maono” kwa ajili ya maisha yake, au kuwa na fikra chanya au mtazamo nzuri, na mara nyingi sana watu wasemapo mambo hayo huzungumzia mambo yahusuyo hapa duniani, mambo ya kimwili na mafanikio ya biashara na siyo ya kiroho.

Mtume Paulo anasema, “natenda NENO MOJA tu; nikiyasahau yaliyo nyuma, NIKIYACHUCHUMILIA yaliyo mbele; NAKAZA MWENDO, niifikilie MEDE YA THAWABU YA MWITO MKUU WA MUNGU KATIKA KRISTO YESU.” (mistari 13,14). Hiyo ndiyo SHAUKU KUBWA ya mtume Paulo, na ndilo lengo lake lenye utukufu! Hiyo ndiyo ‘goli’ yake na ‘mtazamo nzuri’ wake!

Anasema, natenda neno moja TU! Unaona hapo! Jambo MOJA tu ndilo lililokuwa LINASUKUMA maisha yake; alijidhughulisha na GOLI KUU MMOJA; katika maisha yake ALIFILISIWA NA TAMAA KUBWA MNO, ili “amjue YEYE, na uweza wa kufufuka kwake, na ushirika wa mateso yake, akifananishwa na kufa kwake.” (mstari 10).

Je, hilo ndilo lengo lako? Je, hilo ndilo lengo lako KUU? Je, unayahesabu mambo yote kuwa kama sio kitu kwako, NI KAMA MAVI, ukiyalinganisha na kumjua Kristo? Je, moyo wako unakuambiaje? Kwa hiyo Mungu mwenyewe anatangaza, “Mwenye hekima asijisifu kwa sababu ya hekima yake, wala mwenye nguvu asijisifu kwa sababu ya nguvu zake, wala tajiri asijisifu kwa sababu ya utajiri wake; bali ajisifuye na ajisifu kwa sababu hii, ya kwamba ANANIFAHAMU MIMI, NA KUNIJUA, ya kuwa mimi ni Bwana.” (Yer.9:23,24).

Je, tunampenda Bwana kuliko mambo mengine yote? Ni nini inayokusukumu katika maisha yako? Unafilisiwa na shauku ya namna gani? Moyo wako unakuambiaje?

Au unafikiri kuwa mambo haya yalikuwa tu kwa ajili ya mitume pekee? Hapana! Ebu basi usikilize mstari unaofuatia baada ya hapo, “Basi sisi tulio wakamilifu na tuwaze hayo.”

Paulo anatuhamasiha na kutuhimiza tuwe na mtazamo uleule ambao alikuwa nao! Huo ndio matazamo unaofaa!

Bwana Yesu alisema ukweli huu, “lakini kinatakiwa KITU KIMOJA TU, na Mariamu AMELICHAGUA fungu lililo jema, ambalo HATAONDOLEWA.” (Luka 10:42). Je, umelichagua fungu lipi kama kipaumbele katika maisha yako? Je, unafilisiwa na mtazamo upi maishani mwako?

Kama unataka kutimiliza kusudi la Mungu kwako hapa duniani na ile ya umilele, basi ndipo inakupasa uwe na mtazamo (attitude) uleule ambao ulikuwemo kwa mtume Paulo. Ukilinganisha na kumjua Yesu Kristo na uweza wake katika maisha yako, basi mambo yote mengine ni kama mavi.

Nilimaliza masomo yangu ya Chuo Kikuu mwaka 1975. Miezi michache tu baadae Digrii (Shahada) yangu ya Chuo Kikuu ilipoletwa nyumbani sikuwepo nyumbani. Rafiki yangu mmoja alinipigia simu akinipasha habari kuwa Cheti changu cha Digrii kimewasili. Nilimwambia yule ndugu kuwa, “Weka hayo mavi kabatini.” Hii ni hadithi ya kweli.

Sasa, mimi siidharau Digrii yangu, hata kidogo. Ninamshukuru Mungu sana kwamba aliniwezesha kufaulu mitihani yangu. Lakini ile Digrii yangu haikumaanisha chochote kwangu binafsi, yaani, haikunifanya mimi nionekane ni mtu wa tofauti na wengine, na wala haikunifanya nijisikie, au hata nianze kufikiri kuwa mimi ni mtu wa maana zaidi kuliko mtu mwingine. Kulinganisha na kule kumjua Yesu, haikumaanisha kitu chochote kile kwangu. Ile digrii haikunibadilisha mimi kwa namna yoyote ile iwayo, wala mimi siwaangalii watu wengine kwa namna ya utofauti eti kwa sababu tu ninayo digrii, kuwadharau watu wengine eti kwa sababu tu ninayo digrii – hii ingekuwa ni dhambi.

Digrii yangu itapita, lakini kumjua Yesu kwa dhati na nguvu ya ufufuo wake ndani yangu ni kitu ambacho hakitapita kamwe. Kumjua Kristo, kumpenda na kumtii yeye ndilo jambo pekee linaloweza kunibadilisha kwa namna inayompendeza Mungu. Nikiyafikiria yale yote ambayo Kristo aliyonifanyia, moyo wangu wenye shukrani utamfikiria Yeye tu, na kumjua yeye kuwa ni hazina kuu niliyonayo ambayo hailinganishwi na kitu chochote cha duniani hapa, iwe ni elimu yangu au cheo ambacho naweza kuwa nacho katikati ya watu wengine!.Mtume Paulo anasema, “Nayahesabu mambo yote kuwa kama mavi.” Je, dhamira yako inashuhudia ukweli huo maishani mwako?

TAFADHALI USINIELEWE VIBAYA. Unaona, mavi nayo yanafaa – mavi hutumika kama mbolea. Hivyo ninazo shukurani mbele zake Mungu kwamba Shahada yangu ya Chuo Kikuu ilinisaidia kupata kazi! Ukweli huo tunaoongelea kwenye somo hili haumaanishi kwamba hatujali wajibu na majkumu ya masomo, ya kazi, ya biashara nkd zetu hapo duniani – hapana, hata kidogo, ni kinyume chake. Aidha, najua wengi wanajitahidi sana waweze kwenda Chuo Kikuu ili wapate kazi nzuri na sisemi chochote dhidi ya hiyo! Lakini kama tukifanya ‘Jambo moja’ kama Paulo alivyofanya, ndipo tutakuwa na uhakika kuwa Mungu atatuongoza katika NYAKATI ZAKE kwa mambo ya hapa duniani yahusuyo kile tunachokwenda kukifanya katika maisha yetu nyakati zijazo. Kwa sababu imeandikwa, “Maana tu KAZI YAKE, tuliumbwa katika Kristo Yesu, tutende matendo mema, ambayo TOKEA AWALI Mungu aliyatengeneza ILI TUENENDE NAYO.” Na tena, Mungu “ambaye alituokoa akatuita kwa mwito mtakatifu, SI KWA KADIRI YA MATENDO YETU sisi, BALI KWA KADIRI YA MAKUSUDI YAKE yeye na neema yake. Neema hiyo tulipewa katika Kristo Yesu tangu milele.” (Waefeso 2:10; 2 Tim.1:9).

Ndiyo, Mungu atatuongoza katika maisha yetu kuhusiana na kile tunachosomea na aina ya kazi tutakayoipata. Mambo haya yote ni mazuri na ni ya lazima – lakini uwe mwangalifu kwamba malengo yako kwa ajili ya mambo hayo yawe yanayotokana na nema yake Mungu itendayo kazi katika maisha yako, ili kwamba usipoteze kusudi lake Mungu mwenyewe katika maisha yako – yote kwa pamoja hapa duniani na hata umilele.

Basi, kwa hiyo, UNAFISILIWA na tamaa YA NAMNA GANI? UNAPATWA NA shauku YA NAMNA GANI? UNASUKUMWA na MALENGO YAPI katika maisha yako? Je, unayahesabu mambo yote kuwa mavi ili upate Kristo? Je, umepatwa na shauku kumjua Yesu na nguvu Yake katika maisha yako KULIKO MAMBO YOTE na goli yote na ndoto zote nyingine? Moyo wako unakuambiaje?

Kama lengo lako na shauku yako kwa ajili ya mambo ya dunia hii vinapita lengo lako na shauku yako ya kumjua Yesu Kristo, basi jihadharini usipoteze ya ile ya pili PAMOJA NA ILE YA KWANZA! Baraka za dhati za Mungu katika kila sehemu ya maisha yetu zinatokana NA UHUSIANO WETU NA MUNGU – “Utafuteni KWANZA ufalme wake, na haki yake; na hayo yote mtazidishiwa.”

© David Stamen 2018

RUDI KWA MWANZO

25

NIDHAMU ZA MTUMISHI WA MUNGU

“Hata mtu akishindana katika michezo HAPEWI taji, asiposhindana KWA HALALI. Yampasa mkulima mwenye taabu ya kazi kuwa wa KWANZA wa kupata fungu la matunda (au ‘…kuwa wa kwanza KUONJA matunda yale…’). Yafahamu sana hayo nisemayo, kwa maana Bwana atakupa akili katika mambo yote.” (2 Tim. 2:5-7).

Ujuzi hautoshi katika huduma. Ujuzi tu hautawatosheleza wasikilizaji. Haifai mkulima kuuza matunda yake kwa wengine pasipo kwanza yeye mwenyewe kuyala matunda ya kazi yake ili atambue kama yanafaa au la! Kama matunda ya maisha yako hayafai, utawafundishaje wengine? Haifai kuwalisha watu wa Mungu na ‘ujuzi’ wangu tu; kuwalisha na fikira na nadharia (ideas and theories) tu pasipo kwanza neno la Mungu kutimizwa katika maisha ya binafsi yangu kwa kadiri ipasavyo! Lazima mimi mwenyewe kwanza niwe ninaishi maisha ya Kristo kadiri ipasavyo. Matunda ya kiroho ambayo ni kupitia Yesu Kristo lazima yatokeze katika maisha yangu kwanza ili nisiwalishe watu wa Mungu na ujuzi tu! Hapo hamna njia ya mkato (short cut) katika huduma ya Bwana – au hata katika maisha ya Mkristo. Yesu mwenyewe alijaribiwa jangwani! Aliongozwa na Roho nyikani hali AMEJAA Roho Mtakatifu ili ajaribiwe na Ibilisi, lakini tutambue kuwa baada ya siku arobaini akarudi Galilaya kwa NGUVU za Roho! Hali kadhalika, lazima sisi sote tupite au kutembea katika njia ya nidhamu ya kiroho na majaribu. Tusiposhindana kwa halali, hatupewi taji. Na maisha hayo ya nidhamu ya kiroho na kimwili hayaishii baada ya muda tu, bali lazima yawe sehemu ya maisha yetu mpaka mwisho, kama Paulo alivyosema,

“Je! Hamjui, ya kuwa wale washindanao kwa kupiga mbio, hupiga mbio WOTE, lakini apokeaye tuzo ni MMOJA? Pigeni mbio NAMNA HIYO, ili MPATE.Na kila ashindanaye katika michezo HUJIZUIA KATIKA YOTE; basi hao hufanya hivyo kusudi wapokee taji iharibikayo; bali sisi tupokee taji isiyoharibika. Hata mimi napiga mbio VIVYO HIVYO, si kama asitaye; napigana ngumi vivyo hivyo, si kama apigaye hewa; bali NAUTESA mwili wangu na kuutumikisha; ISIWE, nikiisha kuwahubiri wengine, MWENYEWE niwe mtu wa kukataliwa.” (1 Wakor. 9:24-27).

Mtumishi wa Mungu wa dhati, anawalisha watu wa Mungu na neno la Mungu – ila ni lile neno la Mungu ambalo linatokana na uhusiano wake na Mungu! Kimsingi inapaswa lile analolihubiri litokane na maisha yake ya kiroho mbele ya Mungu na nidhamu yake ya kiroho na kimwili – kimsingi analohubiri lisiwe ni jambo la ‘ujuzi’ ambao ameukusanyika kutoka katika vitabu tu au kwenye shule ya Biblia! Hafai kuwajaza watu ujuzi tu! Mtumishi wa Mungu wa kweli amefanywa na Mungu kuwa mhudumu wa Agano Jipya – SIYO WA ANDIKO BALI WA ROHO. (2 Wakor. 3:6). Anahudumia kwa nguvu za Roho, na kwa Roho, sio tu kwa sababu ameshabatizwa na Roho Mtakatifu bali kwa sababu anatembea na Bwana kila siku naye anabadilishwa siku hadi siku kutokana na uhusiano wake na Mungu (2 Wakor.3:18).
Sisemi lile neno analohubiri ni tofauti na mafundisho ya Biblia, hapana, hata kidogo; ila analohubiri limejaribiwa katika maisha ya binafsi yake na kwa hiyo kwake kimsingi siyo jambo la ‘ujuzi’ bali linatokana na uzoefu wake wa dhati MBELE YA BWANA. Mwishoni, ‘kipawa’ au ‘karama’ peke yake havitoshi (Mathayo 7:22,23)! Lazima huduma yetu inatokana na nidhamu ya kiroho, ya kimwili na majaribu vivyo hivyo ilivyokuwa katika maisha ya Kristo Yesu! Kwa hiyo Paulo alimwandikia Timotheo,

“Usiache kuitumia KARAMA ile iliyomo ndani yako, uliyopewa kwa unabii na kwa kuwekewa mikono ya wazee. UYATAFAKARI hayo; UKAE katika hayo; ili KUENDELEA KWAKO kuwe DHAHIRI kwa watu wote. JITUNZE nafsi yako, na mafundisho yako. DUMU katika mambo hayo; maana kwa kufanya hivyo utajiokoa nafsi yako NA WALE WAKUSIKIAO PIA.”

Na tukumbuke kuwa Daudi aliweza kumshinda kwa uhodari tele Goliathi kwa sababu KWANZA kutokana na uzoefu wake mwenyewe alishamwua simba na dubu – na hayo hayakutokea ‘mbele ya watu’ bali katika maisha yake ya binafsi ‘mbele ya Bwana’! Na Daudi hakutumia mavazi ya Sauli ya vita kumshinda Goliathi, alitumia ustadi na silaha ambazo ALIJIFUNZA MWENYEWE KUTOKANA NA IMANI YAKE KWA MUNGU!

Sisemi ni lazima muumini asubiri miaka mingi kabla ya kufanya huduma, hapana, lakini inapaswa mtumishi wa Mungu awalishe waumini na neno la Mungu litokanalo na uhusiano wake na Mungu na muda wake mbele ya Bwana!

RUDI KWA MWANZO

26

JE, UNAPENDA KUWA MTU WA MUNGU?

Je, unataka kuwa mwanamume au mwanamke wa Mungu? Unataka kubarikiwa? Tusikilize neno la Mungu:

“Heri mtu yule… ambaye sheria ya Bwana NDIYO IMPENDEZAVYO, na sheria yake huitafakari MCHANA NA USIKU.” (Zaburi 1:1,2). Je, tunaishi kwa namna kama hiyo? Je, Yesu ni Mwanzo na Mwisho kwetu na tunampenda Yeye na neno lake kuliko yote nyingine? Je, tunakubaliana na Yesu kwamba, “…kinatakiwa kitu kimoja tu” na tumelichagua fungo lililo jema ambalo hataondelewa, kama Mariamu alivyofanya? (Luka 10:42). Je, Neno la Mungu ni thamani kwetu kuliko yote nyingine? Tena tusikilize mtu wa Mungu alilosema katika Zaburi, “…ninayapenda maagizo yako (au tunaweza kusema, ‘neno lako’) KULIKO DHAHABU, naam, dhahabu iliyo safi.” (Zaburi 119:127). Je, haya ni kweli kwetu? Siku hizi wengi wanafundisha juu ya ‘ujasiriamali’ – ni jambo la kuhuzunisha kwamba wengi wanafuata mtazamo huo – wanafuata MAFANIKIO. Wanataka kazi yao ifanikiwe, biashara yao ifanikiwe na kufanikiwa katika kila sehemu ya maisha yao, ingawa Biblia haifundishi ‘yafuate mafanikio’! Biblia inafundisha kwa urahisi sana, “Utafuteni kwanza ufalme wa Mungu na haki yake na hayo yote mtazidishiwa.” (Matt.6:33), na kwa msingi, “tukiwa na chakula na nguo tutaridhika na vitu hivyo.” Neno la Mungu halichochei moyoni mwa watu wa Mungu uchoyo kwa pesa na vitu; halichochei tamaa kwa vitu, pesa au ‘mafanikio’. Watu wengi siku hizi wanatafuta ‘baraka za nje’ kama watu wa Israeli walivyofanya jangwani na wanapoteza kabisa baraka za kiroho, vile vile watu wa Israeli walivyopoteza! Juu ya ‘ujasiriamali’, Paulo anafundisha, “wale watu wanaotamani kuwa na mali kwa huanguka kwenye majaribu na wamenaswa na tamaa nyingi za kipumbavu, zenye kudhuru, zinazowazamisha watu katika uharibifu na maangamizi.” Kinyume cha hicho anafundisha, “Walakini utauwa pamoja na kuridhika NI FAIDA KUBWA.” (1 Tim.6:9,6). Je, inaonekana vipi kwetu? Je, tunampenda neno la Mungu kuliko dhahabu? Tunashauriwa na neno la Mungu ifuatayo, “Mwanangu, kama utayakubali maneno yangu na kuyaweka akiba maagizo yangu ndani mwako,…na kama UTAITAFUTA KAMA FEDHA NA KUITAFUTA SANA KAMA HAZINA ILIYOFICHWA, ndipo utakapoelewa kumcha BWANA na kupata maarifa ya Mungu.” (Mithali 2:1,4,5).

Kama nilivyosema, wengi wanatafuta ‘baraka’, baraka’, ‘baraka’ – lakini wanathamani baraka za ‘nje’ (pesa, biashara. ‘kuboresha’ maisha yao, mafanakio) kuliko neno la Mungu, kama vile watu wa Israeli walivyotaka ‘baraka za nje’ kuliko kumfuata Mungu, kwa hiyo Mungu aliwaambia – vile vile anavyotuambia – “Mtu hataishi kwa mkate ila kwa kila neno litokalo katika kinywa cha Mungu.” (Mtt.4:4). Basi kwa hiyo mtu wa Mungu katika Agano la Kale alikiri, “Nitajifurahisha SANA kwa maagizo yako ambayo NIMEYAPENDA.”. Hata katika shida ilikuwa vile vile; anasema, “Wakuu wakaninena, lakini mtumishi wako ATAZITAFAKARI AMRI ZAKO (au neno lako).” Na tena, “Hiyo ndiyo faraja yangu katika taabu yangu, ya kwamba ahadi yako (neno lako) imenihuisha…Bwana ndiye aliye fungu langu.”. Kwa hiyo anasema, “Neno lako (sheria yako) nalipenda MNO AJABU, ndiyo kutafakari kwangu MCHANA KUTWA!” (Zaburi 119:47, 23, 50, 57, 96). Ushuhuda wetu ni nini sasa? Tukiishi ya namna hiyo – kumpenda Yesu na Neno Lake kuliko yote nyingine – tutakuwa na amani nyingi hata kama hatutafanikiwa katika kila sehemu ya maisha yetu. Kinyume cha hicho, hatakuwa na kitu kutukwaza kwa sababu tunaishi kwa neno la Mungu, kama iliyoandikwa, “Wana amani nyingi waipendayo sheria zako wala hawana la kuwakwaza.” (Zab.119:165).

Sawasawa na Neno la Mungu, siyo wengi wanaomtumikia Bwana Yesu Kristo kweli kweli. Kama ilivyokuwa siku za Paulo, ni vivyo hivyo siku hizi. Paulo anasema juu ya Timotheo, “sina mtu mwingine mwenye nia moja name, atakayeiangalia hali yenu kweli kweli, MAANA WOTE WANATAFUTA VYAO WENYEWE, sivyo vya Kristo Yesu.” (Wafilipi 2:20,21). Je, tunatafuta nini – ‘baraka’, ‘mafanikio’, ‘ujasiriamali’, cheo, faida yetu, sifa, kutawala kama mabwana, ndoto yangu kuwa mwimbaji au kupiga gitaa katika band moja au ndoto nyingine – au kumpendeza Bwana Yesu katika kila kitu na kuongozwa na neno lake.

Kama tukipenda kuwa mwanamume au mwanamke wa Mungu, lazima tuishi kwa neno la Mungu kweli kweli; tusifuate kundi la watu bali tulifuate shauri la Paulo, “UYATAFAKARI HAYO; ukae katika hayo ili kuendelea kwako kuwe dhahiri kwa watu wote, Jitunze nafsi yako na mafundisho yako. Dumu katika mambo hayo, maana kwa kufanya hivyo utajiokoa nafsi yako na wale wakusikiao pia.” (1 Tim.4:15,16.) Maneno ya ajabu!

“Ninalipenda neno lako KULIKO DHAHABU, naam, dhahabu iliyo safi.”

© David Stamen 2014 somabiblia.com

RUDI KWA MWANZO

27

MTU AJULIKANAYE MBINGUNI

“Sala zako na sadaka zako kwa wahitaji zimefika juu na kuwa ukumbusho mbele za Mungu.” (Mat.10:2-4)

Maneno ya ajabu! Ungependa kuwa na ushuhuda kama huo mbele ya Mungu? Malaika alisema maneno haya kwake Kornelio ambaye alikuwa jemadari wa kile kilichojulikana kama kikosi cha Kiitalia. Kornelio hakuwa mhubiri wala mtume wala mchungaji wala nabii wala mwinjilisti! Alikuwa mtu wa kawaida tu. Alikuwa na kazi na familia. Kama jemadari hakika alikuwa na majukumu na shughuli nyingi! Lakini alimwomba Mungu daima! Alichukua muda kuwa peke yake kuomba mbele ya Mungu. Mambo ya kila siku hayakumzuia kwenda mbele ya Mungu kuomba!

Kornelio hakujulikana ulimwenguni lakini alijulikana mbinguni! Ni bora kabisa kujulikana mbinguni kuliko duniani! Je, tunapendelea tujulikane mbele ya watu, duniani, au tujulikane mbinguni, mbele ya Mungu? Usijibu kwa haraka swali hili! Usijibu ovyoovyo! Bali, tunavyoishi ni jibu!

Je, ninajitenga mwenyewe na wengine kwa ajili ya hamu yangu niwe na Mungu tu? Je, kwa kusudi na kwa mkazo tunachukua muda kuwa peke yetu pamoja na Mungu? Je, na tunafanya hivyo siyo kana kwamba ni jambo la kulazimishwa, lakini kwa sababu tumampenda Bwana na astahili tuutafute uso Wake na tujitoe maisha yetu! Je, kwa makusudi na kwa mkazo tunachukua muda kumwomba Mungu kupitia Yesu Kristo kwa ajili ya watu wake na kazi yake? Na je, tunasema sala kana kwamba ingekuwa orodha ya mahitji tu? Au tunao uhusiano na Mungu wa kina, na maombi na maneno yetu mbele ya Mungu yanatokana na uhusiano huo huo? Je, tunachukua muda kujitenga na mambo yote ya ulimwengu huo ili kumwabudu Mungu, kumpenda tu, kumsifu tu, bila kutafuta kitu kingine cho chote kwa ajili yetu? Je, unachoshwa kuwa na Bwana hata nusu saa? Kama tunakwenda mbele ya Bwana kuomba kwa ajili ya mahitaji tu, basi tutakuwa hatuelewi vizuri tabia ya wokovu wetu katika Kristo Yesu. Watu wengi sana hupenda kuimba kanisani na kuongoza sifa na ibada. Siyo nidyo, jamani? Sasa je, unamsifu Bwana na kumsujudu peke yako mahali pa siri ya maisha yako pia? Kama hapana, kwa nini? ‘Mahali pa siri’ ni kwa mfano chumba chako, au porini, au bustani. Haidhuru. Muhimu ni mahali ambapo upo peke yako mbele ya Mwokozi wako tu – mbele ya macho ya Mungu na siyo ya watu!

Kwa msingi thamani ya maisha yangu hayatokani na jinsi nilivyo au jinsi naishavyo mbele ya watu! Bali yanatokana na jinsi nilivyo na jinsi naishavyo mbele ya Mungu, mahali pa siri ya maisha yangu ambapo Mungu tu ananiona! “Sala zako… zimefika juu na kuwa ukumbusho mbele za Mungu.” Kama ukipenda kuwa mtu wa Mungu kweli kweli, lazima uwe na ‘mahali pa siri’ katika maisha yako ya kila siku – pale ambapo Mungu tu anakuona, pale ambapo unamtumikia Mungu tu, peke yako, ambapo hakuna mtu ye yote mwingine akuonaye au ajuaye unalofanya kwa siri! (Mtt.6:4-7; 16-18).

Kwa upande moja, tufanyalo kwa siri ni muhumiu kuliko tufanyalo mbele ya watu! Tunafanyeje kwa siri katika maisha yetu? Je, tunamngojea Mungu, tunautafuta Uso Wake, tumsifu, tumpende, tumsujudu na kumwomba kwa ajili ya watu wake na kazi yake? Je, tunatafuta ile sifa itokayo kwa Mungu na siyo kwa watu? Je, tunajitoa maisha yetu kwake mahali pa siri ili tuwe bila hasira, uchungu, wivu, chuki, malalamiko na manung’nuniko na badaka yake tuwe harufu nzuri ya manukato ya Kristo mbele ya Mungu? (2 Wakor.2:15).

“Kila mmoja wao alikuwa na kinubi, nao walikuwa wameshika mabakuli ya dhahabu yaliyojaa uvumba, ambayo ni maombi ya watakatifu.” (Ufunuo 5:8). Biblia inatufundisha kwamba maombi yetu ni kama uvumba mbele Kiti cha Enzi! Huo ndio ukweli wa maana sana! Hebu tufikiri ukweli huo ili uchochee mioyo yetu tuombe! Kumbuka, malaika alisema, “Sala zako na sadaka zako kwa wahitaji zimefika juu na kuwa ukumbusho mbele za Mungu.”

Unafanya nini kwa siri? Unaangalia nini kwa siri? Unafanya mambo yale ambayo yakusababishe ukue katika Kristo, katika utakatifu, katika imani na katika maisha ya maombi – au mambo yale yanayoharibu maisha yako ya kiroho na hata ya mwili? Maisha yetu ya siri, yaani faraghani, lazima yawe matakatifu.

Wahubiri na wachungaji wengine hupaza sauti sana wanapohubiri wakifikiri hiyo inawakilisha nguvu ya Bwana! Hapana. Wengi kwa sababu ya upungufu wa nguvu ya kiroho katika huduma yao wanapiga kelele wanapohubiri! Nguvu ya huduma yetu inatokana na mahali pa siri (mbele ya Mungu) katika maisha yetu! Ni kweli, huduma inategemea na mwito pia, lakini hata hivyo ni lazima kujitenga kwa ajili ya mwito huo kama Petro alivyosema, “sisi tutatumia muda wetu mrefu kuomba na kulihudumia lile neno.’’ (Mat.6:4).

Na hata mtume Paulo hakupiga mbio kufanya kazi ya Mungu kwa maono yake yenyewe! Alitumikia Bwana kwanza na kuwatumikia watu wa Mungu kanisani kabla ya kwenda kufanya kazi ya mtume! Matendo 13:1,2 inatufundisha jambo la maana sana:

“Katika kanisa huko Antiokia ya Shamu walikuwako manabii na walimu, yaani: Barnaba …na Sauli. Walipokuwa wakimwabudu Bwana na kufunga, Roho Mtakatifu akasema, “Nitengeeni Sauli na Barnaba kwa kazi ile maalumu niliyowaitia.”

Unaona, Paulo hakujitukuza wala hakutazamia watu wamtambue au kumpokea kama mtume muhimu! Alikataa kufanya mapenzi yake yenyewe, na alikataa kufanya kazi ya Mungu kutokana na hamu yake, akili yake au uwezo wake wenyewe. Alibaki kwa unyenyekevu katika kanisa moja kuwahudumia watu wa Mungu, lakini msingi wa maisha yake ulikuwa kuchukua muda kumwabadu Bwana na kufunga mbele Yake mpaka Mungu Mwenyewe alimwita kufanya kazi ya mtume! Hamna watu wa Mungu wengi kama Paulo! Wengine wamalizapo Shule ye Biblia wanafikiri wametayarishwa kufanya huduma ya mchungaji. Hilo ni wazo lisilo na maana! Shule ya Biblia ya kweli ni MAISHA. Ni lazima kujifunza njia za Bwana katika maisha ya kila siku! Wachungaji na wahuburi kadhaa (au hata wengi) hawana kitu cha kiroho kuwaambia washirika kwa sababu wanakosa kuchukua muda kuwa peke yao mbele ya Bwana – “sisi tutatumia muda wetu mrefu kuomba na kulihudumia lile neno.” Kanisa ambalo linao mchungaji wa namna hiyo, hubarikiwa! Watu kama hawa wanawalisha watu wa Mungu na maneno ambayo wanayoyapata kutoka kwake Bwana wakati wanaposali mbele Yake na kuutafuta uso Wake! Wanajitoa kabisa kwake Bwana na wanamngojea. Wengine wanahubiri mawazo ya kibinadamu tu au mambo mapya yanayotoka Ulaya au Amerika! Wanachukua muda kujenga huduma yao badala ya kumtafuta kwenye mahali pa siri.

Kwa sababu mtume Paulo aliishi maisha yake mbele ya Bwana na siyo mbele ya watu, kumbe, alijulikana mbinguni na hata katika ulimwenguni wa kiroho. Tunasoma, “Basi baadhi ya Wayahudi wenye kutangatanga huku na huko wakitoa pepo wachafu wakajaribu kutumia jina la Yesu juu ya wale wenye pepo, walikuwa wakisema, ‘Kwa jina la Yesu, yule anayehubiriwa na Paulo, na kuamuru utoke.’ Palikuwa na wana saba wa mtu mmoja Myahudi jina lake Skewa, aliyekuwa kiongozi wa makuhani, ambao walikuwa wanafanya hivyo. Lakini pepo mchafu akawajibu, ‘Yesu namjua na Paulo pia namjua, lakini ninyi ni nani? Kisha yule mtu aliyekuwa na pepo mchafu akawarukia, akawashambulia vikali, akawashinda nguvu wote …”. (Mat.19:13-16). Tunaona watu wanatumia jina la Bwana bila kumjua Yesu. Paulo alijulikana na Mungu, alijulikana na pepo, na alijulikana na watu! Kama tunafanya kazi ya Mungu ni lazima tujitenge na mambo ya kila siku na kuchukue muda kuwa mbele ya Bwana tujitoeeni kwake katika maombi na kumwabudu, na siyo kujaribu kutimiza ‘maono’ au ‘ndoto’ zetu wenyewe!

“Kornelio Yeye alikuwa mcha Mungu pamoja na wote wa nyumbani mwake, aliwapa watu sadaka nyingi na kumwomba Mungu daima. Siku moja alasiri, yapata saa tisa, aliona maono wazi wazi malaika wa Mungu akimjia na kumwambia, “Kornelio!” Kornelio akamkazia macho kwa hofu akasema, “Kuna nini, Bwana?”

“Sala zako na sadaka zako kwa wahitaji zimefika juu na kuwa ukumbusho mbele za Mungu.” (Mat.10:2-4)

© David Stamen 2015 somabiblia.com

RUDI KWA MWANZO

 

Comments are closed.

 
%d bloggers like this: