RSS

JUU YA FUNDISHO LA ‘ROHO YA KUCHELEWESHA’

HAKUNA ‘ROHO YA KUCHELEWESHA’! USIJIRUHUSU KUDANGANYWA! 

(Nilisoma juu ya mafundisho mapya hayo hivi karibuni. Nilifikiri ni vema niandike kwa ufupi juu ya mafundisho ya kigeni hayo.) 

Biblia haitaji ‘roho ya kucheleweshwa’ (a spirit of delay)! Biblia haitumii expression ‘roho ya kucheleweshwa’. Katika Biblia nzima hamna fundisho lo lote juu ya ‘roho ya ucheleweshi’. Neno la Mungu halifundishi kwamba ‘roho ya ukwamishi’ inaweza kuzuia au kuchelewesha au kukawisha mapenzi ya Mungu katika maisha yako! Neno la Mungu halifundishi kwamba ‘roho ya kucheleweshwa’ inaweza kukwamisha tekelezo la mapenzi ya Mungu katika maisha yako! Hamna fundisho hili! Wala katika Agano la Kale wala katika Agano Jipya, hakuna hata mstari mmoja unaotufundisha lazima ‘tusimame’ na ‘kuikemea’ au ‘kuifunga’ au kuishinda roho ya ucheleweshi au ya ukwamishi fulani kana kwamba ni roho hiyo ambayo inazuia au inachelewesha mapenzi ya Mungu katika maisha yetu! Hakuna aliyefanya hivyo katika Biblia. Fundisho hili linatokana na mawazo ya mioyo ya watu tu (out of the imagination of people’s hearts), halitokani na Biblia. Ni ‘fantasy’ tu, uzushi tu.

Katika maisha ya mwamini kama kipo kitu kinachozuia tekelezo la mapenzi ya Mungu katika maisha yake, kama kipo kitu kinachomzuia asiingie Raha au ahadi za Mungu, kwa mujibu wa neno la Mungu, kimsingi sababu ni kutokuamini au kutokutii (unbelief or disobedience). Waebrania sura ya 3 na 4 zinaweka ukweli huu wazi na bayana – pamoja na mafundisho ya Biblia nzima. Kwa mfano maandiko yanasema, ‘ili msiwe wavivu, bali mkawe wafuasi wa hao wazirithio ahadi KWA IMANI NA UVUMILIVU.’ (Waebr.6:12). 

Unaweza kunukuu mstari wo wote kwenye Biblia katika kujaribu kuthibitisha dai hili (juu ya roho ya kuchelewesha), na nitakuonyesha kwanza, neno la Mungu halitaji wala halifundishi ‘roho ya ucheleweshi’ ni sababu ya shida yo yote, na ya pili, muktadha ya mstari ule unahusu kutokutii au kutokuamini kwa watu wa Mungu, au unahusu mpango, hukumu au hata rehema ya Mungu.

Kwa mfano, wanadai Waisraeli walibaki jangwani muda mrefu kutokana na kazi ya shetani ya kuwashambulia watu wa Mungu na ‘roho ya kucheleweshwa’! This is a fantasy, hiyo ni uzushi. Walizunguka jangwani miaka arobaini kutokana na sababu mmoja tu – kutokuamini / kutokutii kwao! Na alikuwa Mungu, siyo shetani, aliyehukumu Waisraeli wabaki jangwani kwa sababu ya uasi wao (Hesabu 14:22-35)!

Kadhalika, wanadai ‘roho ya kucheleweshwa’ ilifanya kazi yake ili wale wanawali watano wapumbavu wasiwe tayari kukutana na Bwana. Hapana. Hili siyo fundisho la fungu hili! Hawakuweza kuingia kwa sababu HAWAKUCHUKUA MAFUTA na vyombo vyao! Kwa maneno mengine, walikuwa ‘wenye mfano wa utauwa, lakini wakikana nguvu zake,’ kwa hiyo Bwana aliwaambia, ‘Amin, nawaambia, siwajui ninyi.’ Kama tusipoishi kadiri Mungu alivyotuagiza, tutapata hasara maishani mwetu.

Haijalishi mistari wanayoinukuu, tutaweza kuona haihusu ‘a spirit of delay’ / ‘roho ya ucheleweshi’ bali jambo lingine kabisa.

Fundisho hili linavuta watu. Kwa nini? Je, watu hawajui Biblia, hawasomi neno la Mungu, hawajali maandiko yanayoyasema? Kwa nini waamini hawafanyi vile vile watu wa Beroya walivyofanya, yaani, ‘wakayachunguza maandiko kila siku, waone kwamba mambo hayo ndivyo yalivyo.’ Kama wangefanya hivyo, wangetambua kwa upesi fundisho hili halitokei kwenye Biblia!

Labda ipo sababu nyingine pia kwa nini watu watavutwa na fundisho hili. Fundisho hili linaahidi ‘shortcut’ kwa ‘maono’ yako, au ‘matarajio’ yako! Fundisho hili linasema, “Je, umengoja kwa muda mrefu maono au matarajio yako yatimizwe, lakini bado? Kumbe. Ni roho ya ucheleweshi! Ni lazima kushughulika na roho hiyo na kuishinda!” Tatizo kubwa hapo ni hilo – watu hawatofautiani (au hawataki kutofautiana) kati ya HAMU YAO YA BINAFSI (ambayo labda wanayaita ‘maono’ au ‘matarajio’ yao) na mapenzi ya Mungu katika maisha yao. Hamu yao ya binafsi kufanikiwa katika jambo fulani inaweza kuwaongoza kupokea na kuamini fundisho hili. Wanayo hamu kutimiza ‘ndoto’ zao bila kujiuliza, ‘je, jambo hili ni mapenzi ya Mungu kwa ajili ya maisha yangu?’ Na fundisho hili linaahidi shortcut watimize ‘matarajio’ yao.

Ni la maana sana kwamba waandishi wa mafundisho hayo kwa ujumla wanakwepa kutumia maneno ‘mapenzi ya Mungu’! Wanapenedelea kutumia maneno kama ‘matarajio yako’ au ‘maono yako’ au ‘kile ambacho unamini Mungu amekupa ufanye.’ Unaona? Sasa je, wanazungumza juu ya mapenzi ya Mungu kwa maisha yangu, AU juu ya hamu yangu ya binafsi kufanya kitu ambacho labda NINATUMAINI ni mapenzi ya Mungu kwa maisha yangu? Mafundisho hayo yanafungua mlango kwa machanganyiko kubwa sana! Tokeo mmoja ya hayo ni kwamba inawezekana nitajaribu kuishinda ‘roho ya ucheleweshi’ (ambayo haipo) juu ya kitu ambacho siyo mapenzi ya Mungu kwa maisha yangu – inawezekana ni hamu yangu ya binafsi tu, na mimi ni mvivu kumngojea Bwana nitambue nini ni nini, kutambua mapenzi Yake. Ni wengi siku hizi ambao wanataka sana kutekeleza ‘maono’ au ‘ndoto’ au ‘matarajio’ yao bila kujiuliza kweli kweli kama ni mapenzi ya Mungu kwa maisha yao! Na mafundisho ya kigeni hayo yanazidisha machanganyiko hayo hayo.

Kuhusu mapenzi ya Mungu katika maisha yako, fuate neno la Mungu tu, kwa mfano Warumi 12:1,2, inayosema,

“Basi, ndugu zangu, nawasihi, kwa huruma zake Mungu, itoeni miili yenu iwe dhabihu iliyo hai, takatifu, ya kumpendeza Mungu, ndiyo ibada yenu yenye maana. Wala msiifuatishe namna ya dunia hii; bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia zenu, mpate kujua hakika mapenzi ya Mungu yaliyo mema, ya kumpendeza, na ukamilifu.”

Hamna ‘shortcut’. Hamna kuifunga, kuikemea wala kuishindi ‘roho ya ucheleweshi! Ishi kila siku KWA NENO LA MUNGU, na umpende Mungu kwa moyo wako wote na kwa roho yako yote, na kwa nguvu zako zote, kila siku, na Mungu atakuongoza katika mapenzi Yake yaliyo mema, ya kumpendeza, na UKAMILIFU! Na utatambua kuwa Mungu ‘alitubariki kwa baraka zote za rohoni, katika ulimwengu wa roho, ndani yake Kristo’; na ‘yeye aliyeanza kazi njema mioyoni mwako ataimaliza hata siku ya Kristo Yesu,’ na ‘katika mambo yote Mungu hufanya kazi pamoja na wale wampendao katika kuwapatia mema’; na ‘ahadi zote za Mungu zilizopo katika yeye ni Ndiyo; tena kwa hiyo katika yeye ni Amin!’

Mungu alisema kupitia Yeremia maneno haya, ‘“Nabii aliye na ndoto, na aseme ndoto yake; na yeye aliye na neno langu, na aseme NENO LANGU KWA UAMINIFU. MAKAPI ni kitu gani kuliko NGANO? Asema Bwana.” (Yer. 23:28). Sasa kwa nini watu wa Mungu wanapenda kuishi kwa makapi, kumeza makapi ambayo inaharibu maisha ya kiroho yao, badala kuishi kwa ngano, yaani, kwa neno la Mungu? Wanamwamini ‘nabii’ afundishaye mawazo yanayotokana na ubuni wa moyo wake tu bila kuchungza Biblia inayosema!

Kama mafundisho mengine (ya uongo / false teachings) yalivyokuja na yalivyotoweka, vivyo hivyo fundisho hili limekuja na watu wengi walio na ‘masikio ya utafiti’ (2 Tim.4:3) watavutwa na watasikiliza fundisho hili, lakini baada ya muda mfupi litatoweka kabisa kwa sababu fundisho hili ni mawingu bila maji, ni fundisho bila msingi katika Biblia. Watu watakata tama, watachoshwa na fundisho hili na baada ya muda fulani watapokea kwa furaha fundisho lingine la uongo litakalotokea miongoni mwao.

Au na tuishi kwa neno la Mungu!

“Nawaonea wivu, wivu wa Mungu; kwa kuwa naliwaposea mume mmoja, ili nimletee Kristo bikira safi. Lakini nachelea; kama yule nyoka alivyomdanganya Hawa kwa hila yake, asije akawaharibu fikira zenu, mkauacha UNYOFU NA USAFI kwa Kristo.”

—————————————————————————–

Zaidi juu ya mistari wanayotumia:

Wanadai mambo hayajatokea katika maisha yako kwa sababu utimilifu wa wakati umeshawadia lakini ROHO ZA UCHELEWESHAJI zipo kazini KUZUIA neno kutimia kwa wakati uliyokusudiwa maishani mwako! Siyo kweli. Wanatumia mstari gani kuhalalisha wazo hili? Wanatumia, kwa mfano, Wagalatia 4:4 isemayo, “Hata ulipowadia utimilifu wa wakati, Mungu alimtuma Mwanawe ambaye amezaliwa na mwanamke, amezaliwa chini ya sheria.” Lakini mstari huu hauhusu ‘roho za ucheleweshaji’. Kinyume chake, mstari huo unathibitisha kuwa Mungu alimtuma Mwanawe sawasawa na mpango Wake na mapenzi Yake kwa wakati Wake!

Wanasema Yerusalemu hawakumpokea Yesu kwa sababu ‘hukutambua majira ya kujiliwa kwako.’ (Luka 19:41-44). Hiyo ni kweli. Lakini wanaendelea kudai sababu ya shida hii ilikuwa kazi ya ‘roho ya ucheleweshi’ katika ‘ulimwengu wa roho’ ili wasitambue majira yao. Hapana. Biblia inachofundisha ni kinyume chake. Sikiliza Yesu alilosema katika Matayo, “Ee Yerusalemu, Yerusalemu, uwauaye manabii, na kuwapiga kwa mawe wale waliotumwa kwako! Ni mara ngapi nimetaka kuwakusanya pamoja watoto wako, kama vile kuku avikusanyavyo pamoja vifaranga vyake chini ya mabawa yake, LAKINI HAMKUTAKA!” (Mat.23:37). Shida haihusu roho ya kucheleweshwa fulani. Shida ni ugumu wa mioyo ya watu! Shida ni kutokumaini, kutokutii na uasi wa watu. Ukweli ni huu – Wayahudi hawakumwamini Yesu, hawakutaka kutubu, hawakutaka kumpokea Yesu kama mwokozi wao; WALIMKATAA Yesu. Shida ilikuwa hali ya mioyo yao, na hali ya ugumu wa mioyo yao iliwafanya wawe vipofu juu ya wokovu wa Bwana na juu ya mapenzi ya Mungu. Sikilize neno la Mungu, “Leo, kama mtaisikia sauti yake, MSIFANYE MIGUMU MIOYO YENU,… ni AKINA NANI aliowaapia ya kwamba HAWATAINGIA katika raha yake, ila WALE WALIOASI? Basi TWAONA ya kuwa hawakuweza kuingia kwa sababu ya KUTOKUAMINI kwao.” (Waebr.3:15,18,19).

Hebu tusome Mungu alilosema kupitia Yeremia,

“Mavuno YAMEPITA, wakati wa hari UMEKWISHA, wala sisi hatukuokoka.” (Yer.8:20).

Kwa maneno hayo Mungu anataka kusema kwamba baada ya yote Yeye alilolifanya na kulisema, watu wa Wake walichelewa kuokoka, yaani, hawakubadilika. Kwa nini? Kwa sababu ya roho fulani? Hapana. Tusikilize Mungu alilosema juu ya watu Wake katika sura hiyo hiyo,

“Mbona, basi, watu hawa wa Yerusalemu wamegeuka waende nyuma? Hushika udanganyifu sana, HUKATAA kurudi…tazama, WAMELIKATAA neno la Bwana… TULITAZAMIA amani, lakini HAYAKUJA mema yo yote; tulitazamia wakati wa kupona, na tazama, kufadhaika tu!… Mbona wamenikasirisha kwa sanamu zao walizochonga.” (mistari 5,9,15,19).

Kwa nini watu wa Mungu hawakuweza kuingia na kupokea baraka na ahadi za Mungu? Kwa mujibu wa neno la Mungu jibu ni wazi na bayana – hali hiyo ilitokana na kutokuamini na kutokutii kwao na uasi wao. Waisraeli hawakuweza kulaumu kazi ya ‘roho ya kucheleweshwa’ kwa ajili ya ugumu wa mioyo yao! Shida ilikuwa hali ya mioyo yao tu.

Mambo yanategemea na hali ya mioyo yetu! Mungu anakutafuta wewe! Mungu anataka wewe, anataka moyo wako wote uwe Wake! Anataka ‘matarajio’ yako yote uyaweke mbele Zake kama sadaka. Anataka awe kipaumbele chako cha kwanza, na cha mwisho. Abramu alitarajia mtoto wa kiume sana tena sana, LAKINI Mungu alimjia na akamwambia, “Usiogope, Abramu, MIMI ni ngao yako, NA THAWABU YAKO KUBWA SANA.” (Mwanzo 15:1). Mungu aliye hai anataka uhusiano nawe kwa ndani sana! Anataka kuwa thawabu yako kubwa sana kuliko matarajio yako yote! He wants to be your exceeding great reward more than all your hopes and dreams and ambitions. Upo tayari kujitoa kwake Mungu ya namna hiyo?

Tatizo la fundisho hili la roho ya ucheleweshwa ni hili – inakuelekea kuangalia na kutafakari juu ya roho fulani ambayo haipo, badala ya kujenga uhusiano wako na Bwana kutokana na neno Lake. Kwa nini Simeoni na Ana waliweza kutambua wakati wa kuzaliwa kwa Yesu (Luka 2:25-38) bila dalili mahsusi? Kwa sababu walishughulisha na roho ya kucheleweshwa? Hapana! Ni kwa sababu walikwa watu wa kiroho (Simeoni alikuwa mtu mwenye haki, mcha Mungu, AKIITARAJIA FARAJA YA ISRAELI; na Roho Mtakatifu alikuwa juu yake); walitembea na Mungu na kwa hiyo waliweza kutambua mambo kwa macho ya kiroho na kutambua wakati Mungu alipopanga kumtuma Mwanawe! Unaona, yote inategemea na hali ya kiroho ya mioyo yetu na mwenendo wetu mbele ya Mungu, mwenendo wetu wa imani, upendo, utii na saburi.

Kama tukiishi ya namna hiyo, Mungu atayatekeleza mapenzi Yake yaliyo mema, ya kumpendeza, na ukamilifu katika maisha yetu.

“Yeye awezaye kuwalinda ninyi msijikwae, na kuwasimamisha mbele ya utukufu wake bila mawaa katika furaha kuu; Yeye aliye Mungu pekee, Mwokozi wetu kwa Yesu Kristo Bwana wetu; utukufu una yeye, na ukuu, na uwezo, na nguvu, tangu milele, na sasa, na hata milele. Amina.” (Yuda 24,25).

 

Comments are closed.

 
%d bloggers like this: