Kwa nini tunazuiwa kuomba? Pamoja na sababu nyingine zinaonekana kama ni za msingi! ANGALIA HII!
(B) MAOMBI YANAWEZA KUBADILI MAAMUZI YA MUNGU ALIYOYAPANGA KWA TAIFA AU KWA MTU N.K.
Hii tunaipata kwa Nabii Isaya! Tusome maandiko haya kwa makini saaana! ISAYA 38:1 “Siku hizo Hezekia aliugua, akawa katika hatari ya kufa; na Isaya nabii, mwana wa Amozi, akaenda kwa mfalme, akamwambia, ‘BWANA asema hivi, Tengeneza mambo ya nyumba yako; maana utakufa,wala hutapona’.”
Ni ujumbe kutoka kwa nabii! Mungu mwenyewe hapo anasema kwamba “UTAKUFA”, hebu jaribu kufikiri! Ingekuwa wewe Mungu anakwambia hivyo ungefanyaje? Lakini mfalme huyu alijua hata kama Mungu amesema, bado ninaweza kubadili maamuzi yake kwa sasa kwa njia ya maombi! Alichokifanya mfalme ni hiki! ISAYA 38:2 “Basi Hezekia akajigeuza, akaelekeza uso wake ukutani, akamwomba BWANA..Hezekia akalia sana sana.” Hezekia alijua na aliamini kwamba maombi yanaweza kubadili maamuzi ya Mungu kabisa! Baada ya maombi hayo Angalia kilichotokea. ISAYA 38:4, “Ikawa, neno la BWANA likamjia Isaya, kusema, Enenda ukamwambie Hezekia, ‘Mimi nimeyasikia maombi yako, nimeyaona machozi yako; tazama nitaziongeza siku zako…”. Hapo kuna vitu viwili Mungu aliviangalia wakati Hezekia anaomba,
(1) Kuomba kwa imani. “Ikawa, neno la BWANA likamjia Isaya, kusema, ‘Enenda ukamwambie Hezekia, Mimi nimeyasikia maombi yako, nimeyaona machozi yako.” (ISAYA 38:4).
(2) Machozi yaliyoambata na kuomba, japokuwa wako watu huwa wanasema walokole wanalialia, tunalia ili Mungu ayapokee maombi yetu, sisi hatulii kama hao waliliao mapenzi usiku na mchana!
Maombi hapa yaligeuza maamuzi ya Mungu, nafikiri sasa unaweza kuelewa kwa nini tunazuiwa kuomba. Ndugu kama unaomba; hata kama ni nani alitamka kitu gani kwako, au katika ukoo wako kwa kulaani laana zozote zile, unakuta familia nyingine hakuna maendeleo yoyote yale pamoja na bidii zote za kufanya kazi na kusoma! Hakuna kuoa wala kuolewa n.k. Maombi yana uwezo wa kubadilisha laana na kuwa baraka na kufumua fumua kila vitu vibaya vinavyohusika kutukandamiza na kutudidimiza katika maeneo fulani fulani. Hata kama bosi alisema nitakusimamisha kazi, maombi yanaweza kubadili maamuzi ya bosi! Kama maombi yaliweza kugeuza maamuzi ya Mungu sembuse bosi ? Sembuse Rais wa nchi?
Twende kwenye mfano wa pili uone maombi ambavyo yanakitu cha kipekee.
Lucas
June 27, 2020 at 7:30 pm
Asante sana kwa somo zuri, ninebarikiwa
Michael Othiniel
July 9, 2020 at 3:22 am
Ubarikiwe sana