RSS

Category Archives: Uncategorized

MTUMISHI WA MUNGU WA DHATI

– Mtumishi wa Mungu hawatawali washirika wa kanisa.

“Yesu akawaita, akawaambia, ‘Wafalme wa Mataifa huwatawala,…na wakubwa wao huwatumikisha. Lakini kwenu ninyi sivyo; bali mtu anayetaka kuwa mkubwa kwenu, atakuwa mtumishi wenu, na mtu anayetaka kuwa wa kwanza wenu, atakuwa mtumwa wa wote.” (Luka 22:25; Marko 10:42-44).

Mtumishi wa kweli hajifanyi kama ‘Bwana’ juu ya watu wa Mungu – hajiinui juu ya washirika kama ‘rais’ wa watu. Kumbuka, Bwana Yesu, Mwana wa Mungu, alisema ‘KWENU NINYI SIVYO’. Mchungaji huharibu sura ya Yesu machoni pa watu kama akitawala kama ‘mkuu wa kijiji’ juu ya washirika; ameacha tabia ya Yesu kama anajifanya ‘mkubwa’ kanisani. Hayo yote ni kosa kubwa sana. Kama mchungaji akiwatawala watu kwa nguvu, ndipo yeye hafuati Yesu. Paulo aliandika juu ya huduma yake, “Si kwamba tunatawala imani yenu; bali tu WASAIDIZI wa furaha yenu… Kwa maana hatujihubiri wenyewe, bali Kristo Yesu ya kuwa ni Bwana; na sisi wenyewe kuwa tu WATUMISHI WENU kwa ajili ya Yesu.” (2 Wakor.1:24; 4:5).

Mtume Petro aliwaandikia wazee/wachungaji ifuatyo: “lichungeni kundi la Mungu lililo kwenu, na kulisimamia, si kwa kulazimishwa, bali kwa hiari kama Mungu atakavyo; si kwa kutaka fedha ya aibu, bali kwa moyo. WALA SI KAMA WAJIFANYAO MABWANA JUU YA MITAA YAO, bali kwa kujifanya VIELELEZO kwa lile kundi.” (Waebr.13:2,3). Inapaswa mtumishi wa Mungu awe kielelezo kwa washirika na siyo kujifanya ‘Bwana’. Bwana Yesu ametufundisha inapaswa awe ‘mtumishi’ au ‘mtumwa’ wa washirika!

– Kwa sababu ya upendo wake kwa kunid la Bwana, mtumishi wa Mungu yupo tayari kutoa maisha yake kwa ajili ya kundi la Bwana hata kama Yesu Kristo alivyofanya, “nasi tukiwatumaini KWA UPENDO MWINGI, tuliona furaha kuwapa, si Injili ya Mungu tu, BALI NA ROHO ZETU pia, kwa sababu mmekuwa wapendwa wetu.” (1 Wathes.2:8). Kwa hiyo…

– Mtumishi wa Mungu kwelikweli anawatumikia washirika kwa upole and unyenyekevu:

“bali tulikuwa wapole katikati yenu, kama vile mlezi awatunzavyo watoto wake mwenyewe… mimi Paulo mwenyewe nawasihi kwa upole na utaratibu wa Kristo; mimi niliye mnyenyekevu nikiwapo pamoja nanyi” (1 Wathes.2:7; 2 Wakor.10:1).

– Kwa maneno na matendo yake mtumishi wa kweli hachukizi dhamiri za washirika – dhamiri zao zinamshuhudia kwamba mwendo wake ni safi kabisa katika sehemu yote!

“tumekataa mambo ya aibu yaliyositirika, wala hatuenendi kwa hila, wala kulichanganya neno la Mungu na uongo; bali kwa kuidhihirisha iliyo kweli twajionyesha kuwa na haki, DHAMIRI ZA WATU ZIKITUSHUHUDIA MBELE ZA MUNGU…Ninyi ni mashahidi, na MUNGU PIA, jinsi tulivyokaa kwenu ninyi mnaoamini, kwa utakatifu, na kwa haki, bila kulaumiwa;  (2 Wakor.4:2; 1 Wathes.2:10). 

Hakuna sababu kumlaumu! “Tusiwe kwazo la namna yo yote katika jambo lo lote, ili utumishi wetu usilaumiwe.” (2 Wakor.6:3). Na hata Mungu ni shahidi mwendo wake! (1 Wathes.2:5).

– Mtumishi wa kweli wa Mungu HATAFUTI fedha zako. HATAMANI pesa zako wala hatakulazimisha umpe pesa kwa ajili ya huduma au maombi yake.

“Sikutamani fedha wala dhahabu, wala mavazi ya mtu.” (Matendo 20:33). Huyu ni mtumishi wa Mungu kwelikweli.

– Mtumishi wa Mungu HATAFUTI kujifanya mtajiri kupitia huduma yake kwako.

“Lakini Petro akasema, Mimi sina fedha, wala dhahabu, lakini nilicho nacho ndicho nikupacho.” (Mat.3:6). Mtume Petro pamoja na mitume wengine walipokea pesa nyingi sana kwa ajili ya waumini maskini lakini, kumbe, hawakuchukua pesa kwa ajili ya faida yao kujifanya matajiri! Hawakuishi kwenye nyumba ya fahari wala hawakuwa na walinzi wa binafsi. (Au unafakiri Petro au Paulo wangeweza kuwa na magari mengi ya gharama kubwa sana au kuishi katika nyumba ya fahari au kuwa na ndege ya binafsi kama ‘wahubiri’ wengine siku hizi? Je, unafikiri kuishi kwa fahari kama hiyo inawakilisha tabia ya Yesu Kristo?) Mitume wa Bwana walikuwa na moyo safi na walifanya huduma yao bila unyonyaji, “Maana hatukuwa na … maneno ya juujuu ya kuficha choyo; Mungu ni shahidi.” (1 Wathes.2:5). “Basi thawabu yangu ni nini? Ni hii, ya kuwa nihubiripo, nitaitoa Injili bila gharama, bila kutumia kwa utimilifu uwezo wangu nilio nao katika Injili.” (1 Wakor.9:18).

Neno la Mungu ni dhidi wachungaji ambao wanawahudumia watu Wake kwa ajili ya faida zao, kujitajirisha wenyewe. “Bwana MUNGU asema hivi; Ole wao wachungaji wa Israeli, wanaojilisha wenyewe; je! Haiwapasi wachungaji kuwalisha kondoo? …Mnawala walionona, mnajivika manyoya, …lakini hamwalishi kondoo.” Ezekieli 34:2,3.

– Mtumishi wa Mungu HATAFUTI vyake mwenyewe.

“Maana wote wanatafuta vyao wenyewe, sivyo vya Kristo Yesu.” Tutambue, Paulo anasema ‘wote’! Basi, kwa uhakika maana yake ni idadi isiyopungua ‘wengi’! Ina maana, watumishi wengi/wote (ila Timotheo) walitafuta vyao wenyewe! Walitumia huduma yao kwa ajili ya faida yao yenyewe. Jambo la kuhuzunishwa sana! Je, ni tofauti sana siku hizi?

– Mtumishi wa Mungu HATAFUTI kuwapendeza watu, hasemi mambo kwa kusudi la kuvuta watu kanisani kwake ili ajenge kanisa kubwa kwa ajili ya sifa yake.

“Kama ningekuwa hata sasa nawapendeza wanadamu, singekuwa mtumwa wa Kristo.” (Wagal.1:10). “Kama vile tulivyopata kibali kwa Mungu tuwekewe amana Injili, ndivyo tunenavyo; si kama wapendezao wanadamu, bali wampendezao Mungu. Maana hatukuwa na maneno ya kujipendekeza wakati wo wote, kama mjuavyo.” (1 Wathes.2:4,5).

– Mtumishi wa Mungu HATAFUTI sifa ya watu. “Hatukutafuta utukufu kwa wanadamu, wala kwenu, wala kwa wengine.” (1 Wathes.2:6). 

– Mtumishi wa Mungu HAVITAFUTI vitu vyako … wala faida yake! Anatafuta faida ya kiroho ya waumini.

“Maana sivitafuti vitu vyenu, bali nawatafuta ninyi…” 2 Wakor.12:14. Maneno ya ajabu! Mtume wa kweli anajitoa kwa ajili ya faida ya kiroho ya washirika!  Paulo alipenda waumini, siyo ‘vitu vyao’! Hatafuti vitu vyao, pesa zao, sifa zao au utukufu kwa watu! Mtumishi wa Mungu anajitoa kwa ajili ya faida ya wale awahudumiao. Anayo nia moja tu, “Maana nawaonea wivu, wivu wa Mungu; kwa kuwa naliwaposea mume mmoja, ili nimletee Kristo bikira safi.” (2 Wakor.11:2). Naye yupo tayari kujimwaga kwa ajili ya watu wa Mungu ili wapate faida ya kiroho, “Nami kwa furaha nyingi nitatapanya, tena nitatapanywa kwa ajili ya roho zenu. Hata kama kadiri nizidivyo kuwapenda sana, ninapungukiwa kupendwa.” (2 Wakor.12:15).

Maneno ya kuchanga moto! Mtumishi ya Mungu huzidi kuwapenda waumini awahudumiao hata hivyo anapungukiwa kupendwa!

– Mtumishi anamtegemea Mungu kwa ajili ya mahitaji yake.

“Si kwamba nasema haya kwa kuwa nina mahitaji; MAANA NIMEJIFUNZA KUWA RADHI NA HALI YO YOTE NILIYO NAYO. Najua kudhiliwa, tena najua kufanikiwa; KATIKA HALI YO YOTE, na katika mambo yo yote, nimefundishwa KUSHIBA NA KUONA NJAA, kuwa na vingi na kupungukiwa. Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu.” (Wafilipi 4:11-13).

– Mtumishi wa Mungu hufurahi kwa ajili ya waumini wanapotambua ni jambo la haki na la pendo kumsaidia mtumishi ambaye anafanya kazi mbele ya Mungu kwa ajili yao.

“Nalifurahi sana katika Bwana, kwa kuwa sasa mwisho mmehuisha tena fikira zenu kwa ajili yangu, kama vile mlivyokuwa mkinifikiri hali yangu lakini hamkupata nafasi….Lakini mlifanya vema, mliposhiriki nami katika dhiki yangu…. hakuna kanisa lingine lililoshirikiana nami katika habari hii ya kutoa na kupokea, ila ninyi peke yenu. Kwa kuwa hata huko Thesalonike mliniletea msaada kwa mahitaji yangu, wala si mara moja. SI KWAMBA NAKITAMANI KILE KIPAWA, bali nayatamani mazao yanayozidi kuwa mengi, KATIKA HESABU YENU. Lakini ninavyo vitu vyote na kuzidi, tena nimejaa tele; nimepokea kwa mkono wa Epafrodito vitu vile vilivyotoka kwenu, HARUFU YA MANUKATO, sadaka yenye kibali, IMPENDEZAYO MUNGU.”

Ndiyo. Paulo alikuwa na mahitaji na alipokea kile kipawa kwa ajili ya MAHITAJI yake (SIYO KWA AJILI KUMFANYA MTAJIRI) kwa furaha – lakini siyo kutokana na uchoyo au tamani yake apate fedha, lakini alifurahi KWA AJILI YA WAUMINI TU. Katika utoaji wao Paulo alitambua matunda ya pendo katika maisha yao ambayo ni kama harufu ya manukato impendezayo Mungu! Alifurahi kwa ajili ya hayo tu! Tena ni wazi hapo kwamba mtumishi wa Mungu hawalazimishi waumini wamtoe pesa. Anafurahi waumini watoe kipawa kwa hiari kutokana na pendo la Mungu mioyoni mwao!

Ni kweli kabisa, na neno la Mungu linatufundisha kwamba ni jambo la haki na la pendo kuwasaidia watumishi wa Mungu SAWASAWA NA MAHITAJI YAO kama wanajitoa kwa ajili yetu. Lakini ndani ya moyo wa mtumishi wa Mungu kwelikweli hamna uchoyo au tamani kwa pesa, kwa sifa, kwa kujiinua, kwa kujifanya mtajiri au kuishi kwa fahari, wala hawalizimishi watu wa Mungu kumpa pesa.

© 2016  David Stamen    somabiblia.com

KUPAKUA SOMO HILI BONYEZA LINK IFUATAYO:  DALILI KADHAA YA MTUMISHI WA MUNGU

Unaweza kusoma na kusikiliza zaidi kupitia links hapo chini:

https://somabiblia.wordpress.com/uongozi-na-wachungaji-wa-kweli-semina-ya-viongozi/

 
Leave a comment

Posted by on July 15, 2026 in Uncategorized

 

SEMINA MWEZI WA KUMI 2024 DAR ES SALAAM

HAPO CHINI NI AUDIO YA MAHUBIRI YANGU HUKO DAR ES SALAAM SEPTEMBA / OKTOBA 2024

1. ITOENI MIILI YENU IWE DHABIHU ILIYO HAI. SEHEMU 1

2.ITOENI MIILI YENU IWE DHABIHU ILIYO HAI. SEHEMU 2

3. IWENI NA NIA IYO HIYO. SEHEMU 1

4. IWENI NA NIA IYO HIYO. SEHEMU 2

5. DINI INAPINGA MAISHA YA KIROHO

6. LENGO LA UTOAJI KWENYE AGANO JIPYA

7. YATAFAKARINI HAYO

8. KRISTO NDANI YAKO

9. SEMINA YA VIJANA. SEHEMU 1

10. SEMINA YA VIJANA. SEHEMU 2

11. SEMINA YA WACHUNGAJI. SEHEMU 1

12. SEMINA YA WACHUNGAJI. SEHEMU 2

13. KUMJUA YESU

14. HAMNA MADHABAHU DUNIANI SEHEMU 1

15. HAMNA MADHABAHU DUNIANI SEHEMU 2

 

 
Leave a comment

Posted by on October 2, 2024 in Uncategorized

 

KIUMBE KIPYA KATIKA KRISTO!

KIUMBE KIPYA KATIKA KRISTO: SEHEMU 2  (SIKILIZA!)

KIUMBE KIPYA KATIKA KRISTO: SEHEMU 1

 
1 Comment

Posted by on March 26, 2024 in Uncategorized

 

MAMBO YA NDOA

Mafundisho hayo yanazingatia mambo ya ndoa. Kuyasikiliza, bonyeza tu.

MAMBO YA NDOA

 
Leave a comment

Posted by on March 18, 2024 in Uncategorized

 

SINA MASHAKA NA WEWE

SIKILIZA:

SINA MASHAKA NA WEWE – PASIPO IMANI HAIWEZEKANI KUMPENDEZA MUNGU

 
Leave a comment

Posted by on September 3, 2023 in Uncategorized

 

KWA NINI UNAKWENDA KANISANI?

SIKILIZA:

KWA NINI UNAKWENDA KANISANI? 

 
Leave a comment

Posted by on August 31, 2023 in Uncategorized

 

JUU YA MAOMBI SEHEMU 4

SOMO: MAISHA YA MAOMBI KWA MKRISTO (Part 3)

KUWAACHA WATU NA KWENDA KUOMBA!

Hili ni tendo la ajabu sana ambalo Yesu alilifanya! Lilikuwa ni fundisho kwetu! Hebu jaribu kufikiri; Kwa jinsi Yesu ambavyo ana kila kitu, LAKINI PAMOJA NA YESU NA KUWA NA KILA KITU, lakini alijua pasipo maombi yote aliyokuwa nayo HAIWEZEKANI! Yesu mwenyewe alikuwa anajua hapa bila maombi hamna kitu! Alifikia mahali anawaacha makutano halafu anakwenda kuomba. Luka 5:12-16. Hebu tusome mstari wa 16.

“Lakini yeye alikuwa akijiepua,akaenda mahali pasipokuwa na watu,akaomba.”

Hapo Yesu anawakimbia makutano na kuelekea zake kwenye maombi, japokuwa ni ngumu sana kwa baadhi ya watu kuwaacha watu na kwenda kwa kuomba katika mazingira kama haya ya Yesu, kwao ni utukufu. Ikiwa Yesu alifanya hivyo, sisi tunapaswa kufanya hivyo na kuzidi kulingana na maisha yetu na dunia ya leo, lakini leo mtu anasema hana muda wa kuomba, eti kazi zinambana, na kwa sababu nyingine zinazofanana na hizo, lakini bado mtu huyohuyo ambaye anasema hana muda wa kuomba huyo huyo unaweza kumuona katika makundi ya watu au marafiki akiongea muda mrefu, lakini hao hao wanaosema hawana muda wa kuomba ni watu hodari sana kwa kuchat, hana muda wa kuomba lakini ana muda wa kuchat na watu kwa njia ya whatsapp, muda wote anafanya kazi huku yuko whats app! Hana muda wa kuomba lakini ana muda wa kuongea na watu kwenye simu masaa na masaa, hana mua wa kuomba lakini anaangalia movie masaa na masaa; hana muda wa kuomba lakini ana muda wa kuangalia mpira …ninaweza kusema huyu hana muda wa kuongea na Mungu lakini ana muda wa kuongea na watu! Kwa sababu maombi ndiyo kuongea na Mungu.

Kuongea na watu si vibaya; si vibaya kuchat na watu kwa njia mbalimbali za mitandao, lakini ni mbaya kama tuna muda wa kufanya hivyo lakini hatuna muda wa kuomba! Ni mbaya sana! Sana ! Inatakiwa ifikie mahali tunaongea na watu lakini ukifika muda fulani tunajiepua na kwenda mahali kusikokuwa na watu au mahali ambapo tutaweza kuomba bila buguza! Hapa Yesu hakwenda kanisani! Maombi tunaomba popote pale kama mazingira hayaturuhusu kwenda kanisani, tukipata nafasi tu kidogo tu; tunaomba hata kimoyomoyo! Kuomba sio lazima iwe kanisani.

Bila maombi tutajikuta tunaishi maisha ya unafiki! Maisha ya uhitaji wa kupitiliza na kujikuta kwenye madeni wakati wote, ukiondoa maombi hata unahubiri kila siku lazima iko siku utaanguka tu! LAZIMA! Tuache mambo ya kukaa kaa na watu na kuongeaongea muda mwingi tunaumalizia kwa watu. Tena wakati mwingine mambo mengine hayana hata maana, tunaopoteza kuongea na watu ambao hata tukienda kulala hata hawajui yanayotusibu katika usingizi wetu. Hawana sifa ya kuongea na sisi kabla ya kuongea na Mungu wetu! Kama Yesu aliomba mwenye huduma kubwa kuliko huduma yako wewe ambaye unalewa na sifa za watu lakini kuomba hutaki! Sisi tutapona? Shetani alikuwa hana kitu kwa Yesu lakini bado Yesu alikuwa anaomba. Tusidanganywe na sifa zinazotoka vinywani mwa watu.
Tuweke ratiba kwamba! Kuanzia muda fulani ni muda wa maombi. Hapo hata simu ipigwe hakuna kupokea, tunakwenda mahali pasipokuwa na watu kifikra! Yesu alikwenda sehemu halisi! Lakini kama mazingira yetu hayaturuhusu kufanya hivyo, tunapaswa kwenda mbali na watu kifikra! Wakati wa kuomba ikiwezekana zima simu yako au weka silent kama simu yako ndio kila kitu! Nikiwa na maana kuna bible n.k.

Yesu naye tungesema hana muda, kwa sababu pale alikuwa kazini! Lakini alijua umuhimu wa maombi! Kama wewe huna muda usile chakula basi! Kinachokufanya ule nini wakati huna muda?

 
Leave a comment

Posted by on July 11, 2020 in Uncategorized

 

JUU YA MAFUNDISHO NA HISTORIA YA WASABATO

KUSOMA JUU YA MAFUNDISHO NA HISTORIA YA WASABATO NA KULINGANISHA NA MAFUNDISHO YA BIBLIA NA INJILI YA KWELI, TEMBEA KWA:

https://www.wasabato.com

 
Leave a comment

Posted by on June 30, 2020 in Uncategorized

 

JUU YA MAOMBI 3

Hapa sasa tunaona Ibrahimu ambavyo alikuwa anawashawishi malaika waliotumwa na Mungu kwa ajili ya kuiangamiza Sodoma na Gomora. Mwanzo18:32. “Je! Utaharibu mwenye haki pamoja na mwovu? Huenda wakawapo wenye haki hamsini katika mji, utaharibu wala hutaacha mji.Hasha usifanye hivyo,…BWANA akasema, Nikiona katika Sodoma wenye haki hamsini mjini, nitapaacha kwa ajili yao.”

Ibrahimu aliendelea kusema na wale malaika mpaka akafikia hesabu ya watu 10! Na ibrahimu akaishia hapo, kama Ibrahimu angeendelea kusihi bila shaka maangamizo yasingetokea. (Mwa 18:30-32). Zaidi sana walichokifanya malaika ni kumuondoa Lutu na mkewe na wanawe ambao inaonyesha hawakufika 10 kama wangekuwa 10 wasingetolewa ili mji uangamizwe kwa sababu Ibra alifanya maombi na yakajibiwa kwamba kwa idadi ya watu 10 tu na kama hao 10 wangekuwepo Sodoma na Gomora isingeangamizwa, wangeachwa na Mungu angetumia njia nyingine! Maana Alisema kama wamgekuwa 10 asingeuangamiza mji.    

 
2 Comments

Posted by on June 27, 2020 in Uncategorized

 

SOMO JUU YA MAOMBI (Sehemu 2)

Kwa nini tunazuiwa kuomba? Pamoja na sababu nyingine zinaonekana kama ni za msingi! ANGALIA HII!

(B) MAOMBI YANAWEZA KUBADILI MAAMUZI YA MUNGU ALIYOYAPANGA KWA TAIFA AU KWA MTU N.K.

Hii tunaipata kwa Nabii Isaya! Tusome maandiko haya kwa makini saaana! ISAYA 38:1 “Siku hizo Hezekia aliugua, akawa katika hatari ya kufa; na Isaya nabii, mwana wa Amozi, akaenda kwa mfalme, akamwambia, ‘BWANA asema hivi, Tengeneza mambo ya nyumba yako; maana utakufa,wala hutapona’.”

Ni ujumbe kutoka kwa nabii! Mungu mwenyewe hapo anasema kwamba “UTAKUFA”, hebu jaribu kufikiri! Ingekuwa wewe Mungu anakwambia hivyo ungefanyaje? Lakini mfalme huyu alijua hata kama Mungu amesema, bado ninaweza kubadili maamuzi yake kwa sasa kwa njia ya maombi! Alichokifanya mfalme ni hiki! ISAYA 38:2 “Basi Hezekia akajigeuza, akaelekeza uso wake ukutani, akamwomba BWANA..Hezekia akalia sana sana.” Hezekia alijua na aliamini kwamba maombi yanaweza kubadili maamuzi ya Mungu kabisa! Baada ya maombi hayo Angalia kilichotokea. ISAYA 38:4, “Ikawa, neno la BWANA likamjia Isaya, kusema, Enenda ukamwambie Hezekia, ‘Mimi nimeyasikia maombi yako, nimeyaona machozi yako; tazama nitaziongeza siku zako…”. Hapo kuna vitu viwili Mungu aliviangalia wakati Hezekia anaomba,

(1) Kuomba kwa imani. “Ikawa, neno la BWANA likamjia Isaya, kusema, ‘Enenda ukamwambie Hezekia, Mimi nimeyasikia maombi yako, nimeyaona machozi yako.” (ISAYA 38:4).

(2) Machozi yaliyoambata na kuomba, japokuwa wako watu huwa wanasema walokole wanalialia, tunalia ili Mungu ayapokee maombi yetu, sisi hatulii kama hao waliliao mapenzi usiku na mchana!

Maombi hapa yaligeuza maamuzi ya Mungu, nafikiri sasa unaweza kuelewa kwa nini tunazuiwa kuomba. Ndugu kama unaomba; hata kama ni nani alitamka kitu gani kwako, au katika ukoo wako kwa kulaani laana zozote zile, unakuta familia nyingine hakuna maendeleo yoyote yale pamoja na bidii zote za kufanya kazi na kusoma! Hakuna kuoa wala kuolewa n.k. Maombi yana uwezo wa kubadilisha laana na kuwa baraka na kufumua fumua kila vitu vibaya vinavyohusika kutukandamiza na kutudidimiza katika maeneo fulani fulani. Hata kama bosi alisema nitakusimamisha kazi, maombi yanaweza kubadili maamuzi ya bosi! Kama maombi yaliweza kugeuza maamuzi ya Mungu sembuse bosi ? Sembuse Rais wa nchi?
Twende kwenye mfano wa pili uone maombi ambavyo yanakitu cha kipekee.

 
2 Comments

Posted by on June 26, 2020 in Uncategorized