RSS

Category Archives: Biblia Kiswahili

SOMO JUU YA MAOMBI 1

SOMO JUU YA MAOMBI (Sehemu 1)

Wako wakristo ambao tunashindwa kuwa na maisha ya maombi kwa sababu zifuatazo.

(1) Kukosa muda wa kuomba kwa sababu ya majukumu ya muhimu ya hapa na pale.
(2) Mazingira ya mtu anapoishi.
(3) Mwingine hajui faida za maombi wala umuhimu wake.
(4) Mwingine anasema huwa anaishiwa maneno kwa haraka anapokuwa kwenye maombi.
(5) Mwingine hapendi maombi tu!
(6) Shetani.
(7) Mwili.

Katika maombi kuna vikwazo vingi, kwa sababu maombi yana nguvu!

(A) MAOMBI YANAONGEZA UHUSIANO WA MTU NA MUNGU!

Maombi ni mawasiliano baina ya mwanadamu na Mungu au ni njia ambayo tunaweza kuwasiliana na Mungu. Tunafanya mawasiliano na Mungu kwa njia ya maombi, na kama tunavyojua kwamba! Mawasiliano yanaongeza uhusiano wa mtu na mtu, hata wewe ni shahidi katika hili! Unaweza ukawa na ndugu wengi sana au marafiki wengi sana n.k. Lakini yule ambaye atawasiliana na wewe mara kwa mara huyo ndiye anayeukuza ukaribu kupita wengine. Na pia uhusiano wa mtu unaanzishwa kwa mawasiliano na vilevile unaweza ukafa au kupungua kwa kukosa mawasiliano ya mara kwa mara na kuelekezwa kule kwenye mawasiliano ya mara kwa mara! Mawasiliano yamewafanya watu wengi kuwa karibu, kupitia mitandao yetu. Mtu alipoanza mawasilano na wewe kwa njia ya kukutumia ujumbe wa maandishi au wa picha ulipojibu! Mawasilano yakakua mwisho wake ukaribu ukaongezeka kati yako na huyo….

Tunapokuwa tunaomba mara kwa mara uhusiano wetu na Mungu unakuwa kwa kasi sana kuzidi yule asiyeomba, au yule anayeomba mara moja moja au yule anayeomba kwa viwango vya juu zaidi! Na kama tujuavyo, kadiri uhusiano wa mtu na mtu unavyokuwa na kuongekezeka ndivyo wanavyoweza kushirikishana mambo mengi saaaana!

Ndivyo inavyokuwa kwa Mungu kwetu! Kwa sababu mahusiano yetu yanakuwa na kuongezeka! Mungu hataacha kutushirikisha mambo mengi yanayoendelea ili kuyaombea au kuzuia yasitokee au kuwashauri watu n.k. Mungu atatuonyesha hata hatari iliyopo mbele yetu, kwamba! Kuna ajali mbaya itatokea na kusababisha hiki na hiki na jinsi ya kuikwepa n.k. Yakiambatana na maelekezo yake jinsi ya kufanya ambayo yatakuwa na lengo la kujenga na si kubomoa! Utakuwa na furaha na amani wakati woote hata kwenye dhiki za namna gani! Sijui nitumie lugha gani nieleweke jamani: Ili uelewe hili na kulishika kwamba! MAOMBI YANAONGEZA UHUSIANO WA MTU NA MUNGU!

Tuanze maisha ya maombi kuanzia sasa ili uhusiano wetu na Mungu ukue, anzisha mahusiano yako na Mungu kwa kuwasiliana naye mara kwa mara kwa njia ya maombi. Hata kama zamani tulikuwa na bidii ya kuwasiliana na Mungu kwa njia ya maombi halafu tukayakata mawasilano hayo! Bado tunaweza kuyaanzisha upya na kuyakuza! Pia usiache kuwasiliana na Mungu mara kwa mara kwa njia ya maombi kwa sababu kwa kutofanya hivyo utauvunja au utaupunguza uhusianao wako na Mungu!

Marco Bashiri

 
1 Comment

Posted by on June 25, 2020 in Biblia Kiswahili, Maombi, Vita vya Kiroho

 

Tags: , , ,

MWANZO

This slideshow requires JavaScript.

Karibu somabiblia.  Naitwa David Stamen. Hapa unaweza kusikiliza na kusoma jumbe juu ya mafundisho ya Biblia. Pia unaweza kupakua Biblia, kamusi, hadithi na nyimbo kwa Kiswahili, Kiingereza na kimaasai. Yote ni bure. Kusoma  juu ya huduma yangu bonyeza llink ifuatayoHUDUMA YANGU ]  

(FOR THIS PAGE IN ENGLISH: CLICK HERE)

MASOMO MAFUPI YA KUTIA MOYO

MASOMO ] 

[ JUMBE ZA KUSIKILIZA ] 

[ BIBLIA NA KAMUSI ]  [ HADITHI NA NYIMBO ]

ARTICLES IN ENGLISH

VIDEO: FEDHA YAKO NA IPOTELEE MBALI PAMOJA NAWE!

NIFUATE KWENYE FACEBOOK. UTAPATA MASOMO MAPYA MARA YATAKAPOANDIKWA.

—————————————————-
MAPYA: SEMINA YA VIJANA YA SIKU TANO JUU YA UTAKASO. 2018 DAR ES SALAAM

  1. UTAKASO. SEHEMU 1. SHOKA LIMEKWISHA KUWEKWA PENYE MASHINA.
  2. UTAKASO. SEHEMU 2. MWANAKONDOO AIONDOAYE DHAMBI YA ULIMWENGU.
  3. UTAKASO. SEHEMU 3. NAJITAKASA MWENYEWE.
  4. UTAKASO. SEHEMU 4. MSIUPENDE ULIMWENGU.
  5. UTAKASO. SEHEMU YA 5. KUISHI KWA NENO LA MUNGU

JUU YA HALI YA MAKANISA SIKU HIZI NA WAANDISHI MBALIMBALI  (HAPO CHINI):

  1. KANISA NI NINI?  David Stamen
  2. TURUDI TENA KWENYE KUMHUBIRI KRISTO.   Mch. Carlos Ricky Wilson Kirimbai
  3. INJILI YA MAFANIKIO INAVYOLIANGAMIZA TAIFA   Jackson Malugu (Mhariri wa Mwanzonews)
  4. ‘SIKUTAMANI FEDHA WALA DHAHABU, WALA MAVAZI YA MTU’  Mch. Gasper Madumla
  5. MIMI NAPATA SHIDA SANA. MUNGU TU ANIREHEMU KAMA NAKOSEA. Mch. C.R.W. Kirimbai

MASOMO YAPENDEKAYO YA KUSOMA:

  1. MAMBO YA ZAKA, UTOAJI, SADAKA, FUNGU LA KUMI NA PESA     
  2. VITA VYA KIROHO NA JINSI YA KUOMBA 
  3. MAFUNDISHO JUU YA LAANA
  4. VITA VYA KIROHO NA KUOMBA KWELI KWELI.
  5. TUKUSANYIKE SIKU GANI KATI YA JUMAMOSI NA JUMAPILI?
  6. SABABU YA UMASKINI NA UFUKARA NI NINI?
  7. JE, UNATAFUTA NDOTO ZAKO AU MAPENZI YA MUNGU?
  8. SIRI YA MAFANIKIO – YESU HAKUWA MOTIVATIONAL SPEAKER
  9. MAAGANO YA MUNGU
  10. UZIMA WA MILELE NI NINI? INJILI NI NINI?
  11. HILA NA MBINU ZA SHETANI NA JINSI YA KUZISHINDA. VITA VYA KIROHO KWELI KWELI.

 MASOMO NYINGINE YOTE: BOFYA HAPA

JUMBE ZIPENDEKAZO ZA KUSIKILZA (AUDIO):

  1. UFALME WA MUNGU 1: SHOKA LIMEKWISHA KUWEKWA MIZIZI
  2. UFALME WA MUNGU 2:  KUFANYWA KIUMBE KIPYA – KUFANYWA HAKI YA MUNGU!
  3. YESU ANATOSHA / UNATAKA NINI: SEMINA YA CASFETA
  4. YESU NI NJIA: SEMINA YA CASFETA
  5. USIZOELEE KUWA MKRISTO
  6. ENENDA ZAKO WALA USITENDE DHAMBI TENA
  7. UONGOZI NA WAHUBIRI WA KWELI
  8. CHANGAMOTO KWA VIJANA NA KWA WOTE
  9. SISI TU MANUKATO YA KRISTO
  10. MAFUNDISHO JUU YA MAOMBI

 JUMBE (AUDIO) ZOTE: BONYEZA HAPA

                       BIBLIA NA KAMUSI

  1. BIBLIA KWA KISWAHILI NA KIINGEREZA: DOWNLOAD
  2. DOWNLOAD KAMUSI / DICTIONARIES
  3. DOWNLOAD KIMAASAI AGANO JIPYA AUDIO
  4. DOWNLOAD KISWAHILI AGANO JIPYA AUDIO
  5. SOMA NA SIKILIZA BIBLIA KWA KISWAHILI
  6. SOMA NA SIKILIZA BIBLIA KWA KIINGEREZA
  7. DOWNLOAD / PAKUA OSOTUA NGEJUK : Agano Jipya kwa Kimaasai. 

SOMA OSOTUA NGEJUK KWENYE MTANDAO (INTERNET) Inayo Fahirisi.

 NYIMBO, HADITHI ZA BIBLIA NA JESUS FILM                 

  1. NYIMBO ZA KIMAASAI: SIKILIZA NA DOWNLOAD
  2. NYIMBO KWA KISWAHILI NA KIINGEREZA : SIKILIZA / DOWNLOAD
  3. NYIMBO KWA KISWAHILI NA KIINGEREZA : SIKILIZA / DOWNLOAD 
  4. HADITHI ZA BIBLIA KWA KIMAASAI: SIKILIZA / DOWNLOAD
  5. HADITHI ZA BIBLIA KWA KISWAHILI: SIKILIZA  / DOWNLOAD 
  6. JESUS FILM KISWAHILI: ANGALIA VIDEO NA DOWNLOAD 
  7. JESUS FILM KIMAASAI: ANGALIA VIDEO / DOWNLOAD 

NYIMBO MPYA ZA KISASA

KUWASILIANA NAMI, DAVID STAMEN:   kwa email: dsta12@hotmail.co.uk  /  kwa simu: +44 7985653844

Karibu jumbe hizi zote zimeandikwa na zimehuburiwa na mimi, David Stamen. Ninayo hakimiliki kwa zote. Lakini unaweza kupakua au kucopy jumbe hizo kwa ajili ya matumizi yako ya binafsi. Lakini kama ukitaka kuchapisha, kugawa au kutolewa makala au jumbe zangu, unijulishe kabla kuhusu kusudi lako ili nijue juu ya mpango wako. Unapochapa makala yangu, weka jina langu na anwani ya tovuti yangu kama ifuatayo:    © David Stamen somabiblia.com    Siyo halali kuuza makala au jumbe zangu.

SIKILIZA NYIMBO ZA KIKRISTO KWA MFULULIZO. BONYEZA PICHA HAPO CHINI:

   

 

Tags: , , , , , , , , , , , , , , , , , , , , , , , , , , , , , , ,